Isaya 52 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 52:1-15

152:1 Isa 51:9; Es 6:8; Ufu 21:2; Yoe 3:17; Zek 3:4; Isa 49:18; Kut 28:2, 40; Neh 1:1Amka, amka, ee Sayuni,

jivike nguvu.

Vaa mavazi yako ya fahari,

ee Yerusalemu, mji mtakatifu.

Asiyetahiriwa na aliye najisi

hataingia kwako tena.

252:2 Zek 2:7; Isa 29:4; 10:27; Za 81:9; 9:14Jikungʼute mavumbi yako,

inuka, uketi kwenye kiti cha enzi, ee Yerusalemu.

Jifungue minyororo iliyo shingoni mwako,

ee Binti Sayuni uliye mateka.

352:3 Za 44:12; Isa 45:13; 1:27; 1Pet 1:18Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana:

“Mliuzwa pasipo malipo,

nanyi mtakombolewa bila fedha.”

452:4 Mwa 46:6; Isa 10:24Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi:

“Hapo kwanza watu wangu walishuka Misri kuishi,

hatimaye, Ashuru wakawaonea.

552:5 Eze 36:20; Rum 2:24; Isa 37:23“Basi sasa nina nini hapa?” asema Bwana.

“Kwa kuwa watu wangu wamechukuliwa pasipo malipo,

nao wale wanaowatawala wanawadhihaki,”

asema Bwana.

“Mchana kutwa

jina langu limetukanwa bila kikomo.

652:6 Isa 49:23; Kut 6:3; Isa 41:26; 10:20Kwa hiyo watu wangu watalijua Jina langu;

kwa hiyo katika siku ile watajua

kwamba ndimi niliyetangulia kulisema.

Naam, ni mimi.”

752:7 2Sam 18:26; Rum 10:15; 1Kor 15:24-25; Lk 2:14; Isa 42:11; 40:9; Efe 6:15Tazama jinsi miguu ya wale waletao habari njema

ilivyo mizuri juu ya milima,

wale wanaotangaza amani,

wanaoleta habari njema,

wanaotangaza wokovu,

wauambiao Sayuni,

“Mungu wako anatawala!”

852:8 Sef 3:9; Eze 3:17; 1Sam 14:16; Isa 56:10; Yer 6:17; Hes 10:36; Zek 8:3Sikiliza! Walinzi wako wanapaza sauti zao,

pamoja wanapaza sauti zao kwa furaha.

Wakati Bwana atakaporejea Sayuni,

wataliona kwa macho yao wenyewe.

952:9 Za 98:4; Isa 35:2; Za 74:3; Isa 48:20; Ezr 9:9; Lk 2:25; Isa 51:3Pazeni sauti ya nyimbo za furaha pamoja,

enyi magofu ya Yerusalemu,

kwa maana Bwana amewafariji watu wake,

ameikomboa Yerusalemu.

1052:10 Lk 2:30; Za 67:2; Isa 66:18; 2Nya 32:8; Za 44:3; Isa 30:30; Yos 4:24Mkono mtakatifu wa Bwana umefunuliwa

machoni pa mataifa yote,

nayo miisho yote ya dunia itaona

wokovu wa Mungu wetu.

1152:11 Yer 50:8; 2Kor 6:17; Hes 8:6; 2Tim 2:9; Isa 1:16; 2Nya 36:10; Isa 48:20Ondokeni, ondokeni, tokeni huko!

Msiguse kitu chochote kilicho najisi!

Tokeni kati yake mwe safi,

ninyi mchukuao vyombo vya Bwana.

1252:12 Kut 14:19; 12:11; Mik 2:13; Yn 10:4Lakini hamtaondoka kwa haraka,

wala hamtakwenda kwa kukimbia;

kwa maana Bwana atatangulia mbele yenu,

Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi nyuma yenu.

Mateso Na Utukufu Wa Mtumishi

1352:13 Isa 53:3; Mdo 3:13; Yos 1:8; Isa 20:3; 57:15; Flp 2:9Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa hekima;

atatukuzwa, na kuinuliwa juu, na kukwezwa sana.

1452:14 Law 26:32; Ay 2:12; 16:16; 18:20; 2Sam 10:4Kama walivyokuwa wengi

walioshangazwa naye,

kwani uso wake ulikuwa umeharibiwa sana

zaidi ya mtu yeyote

na umbo lake kuharibiwa

zaidi ya mfano wa mwanadamu:

1552:15 Ebr 9:13; Rum 15:21; Efe 3:4-5; Za 107:42; Amu 18:19; Law 14:7; 16:14-15hivyo atayashangaza mataifa mengi,

nao wafalme watafunga vinywa vyao kwa sababu yake.

Kwa kuwa yale ambayo hawakuambiwa, watayaona,

nayo yale wasiyoyasikia, watayafahamu.

Swedish Contemporary Bible

Jesaja 52:1-15

Herren ska föra hem sitt folk

1Vakna, vakna,

klä dig i din styrka, Sion!

Klä dig i din högtidsskrud,

Jerusalem, du heliga stad!

Ingen oomskuren eller oren

får komma in där.

2Skaka dammet av dig,

res dig, inta din plats, Jerusalem!

Bryt loss kedjorna från din hals,

du fångna dotter Sion!

3För så säger Herren:

”Ni såldes för ingenting,

och utan pengar ska ni köpas fria.”

4Så säger Herren Gud:

”För länge sedan begav sig mitt folk till Egypten för att bo där en tid.

Sedan blev de förtryckta av Assyrien.

5Och vad har jag nu här? säger Herren.

Mitt folk har förts bort för ingenting,

de som härskar över dem skränar, säger Herren,

och man hånar mitt namn dag efter dag.

6Därför ska mitt folk få lära känna mitt namn,

och därför ska de den dagen inse att jag är den som talar. Jag är här.”

7Så härligt det är att höra budbärarens steg

när han kommer över bergen

med goda nyheter,

förkunnar fred,

bär goda nyheter om räddning

och säger till Sion:

”Din Gud är kung!”

8Hör, dina vakter ropar

och gläds tillsammans.

Med egna ögon ser de

Herren återvända till Sion.

9Brist ut i jubel, Jerusalems ruiner,

för Herren har tröstat sitt folk,

och han har friköpt Jerusalem!

10Herren har visat

sin makt och helighet för alla folk.

Hela jorden ska se vår Guds räddning.

11Bort, bort! Gå ut därifrån!

Rör inte det som är orent!

Gå ut och rena er,

ni som bär Herrens kärl!

12Ni ska inte ge er iväg i hast,

ni går ju inte ut som flyktingar,

för Herren går framför er,

Israels Gud går sist i ert tåg.

Herrens lidande tjänare52:13—53:12 Avsnittet är svårförståeligt och många detaljer i översättningen osäkra, t.ex. enligt Septuaginta: häpna i v. 15 är ett ord vars betydelse är oviss.

13”Se, min tjänare ska ha framgång.

Han ska bli upphöjd, mäktig och ärad.

14Många ska förundras över dig.

Han var så vanställd

att hans utseende knappast ens var mänskligt.

15Men nu får han många folk att häpna,

och kungar ska förstummas inför honom.

De ska se något som ingen förr berättat för dem,

och förstå något som de inte hört talas om.”