Isaya 34 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 34:1-17

Hukumu Dhidi Ya Mataifa

134:1 Isa 43:9; Kum 4:26; 32:1; Za 24:1; Isa 33:13Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize;

sikilizeni kwa makini,

enyi kabila za watu!

Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake,

ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!

234:2 Isa 13:5; Zek 5:3; Isa 10:25; 30:25Bwana ameyakasirikia mataifa yote;

ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote.

Atawaangamiza kabisa,

atawatia mikononi mwa wachinjaji.

334:3 Yoe 2:20; Amo 4:10; Eze 38:22; Isa 5:25; Za 110:6; Eze 5:17; 14:19Waliouawa watatupwa nje,

maiti zao zitatoa uvundo,

milima itatota kwa damu zao.

434:4 2Pet 3:10; Yoe 2:31; Eze 32:7-8; Ay 9:7; Ufu 6:13; Isa 13:13; Mt 24:29; Ay 8:12; Mk 13:15; Isa 15:6; Ebr 1:12Nyota zote za mbinguni zitayeyuka

na anga litasokotwa kama kitabu,

jeshi lote la angani litaanguka

kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu,

kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.

534:5 Yer 49:7; 46:10; Zek 13:7; 2Sam 8:13-14; Yos 6:17; Kum 32:41-42; Amo 3:14-15; Yer 47:6; Eze 21:5; 2Nya 28:17; Amo 1:11-12; 6:11; Mal 1:4Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni,

tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu,

wale watu ambao nimeshawahukumu,

kuwaangamiza kabisa.

634:6 Kum 32:41; Law 3:9; Mwa 36:33; Isa 30:25; Yer 25:34; Ufu 19:17Upanga wa Bwana umeoga katika damu,

umefunikwa na mafuta ya nyama:

damu ya kondoo na mbuzi,

mafuta kutoka figo za kondoo dume.

Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra,

na machinjo makuu huko Edomu.

734:7 Hes 23:22; Za 68:30; 2Sam 1:22Nyati wataanguka pamoja nao,

ndama waume na mafahali wakubwa.

Nchi yao italowana kwa damu,

nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.

834:8 Isa 2:12; 1:24; 59:18; Yoe 3:4; Eze 25:12-17; Amo 1:6-10Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi,

mwaka wa malipo,

siku ya kushindania shauri la Sayuni.

934:9 Mwa 19:24Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami,

mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho,

nchi yake itakuwa lami iwakayo!

1034:10 Ufu 14:10-11; 19:3; Yer 49:18; Mal 1:3; Isa 13:20; Eze 29:12; 35:3Haitazimishwa usiku wala mchana,

moshi wake utapaa juu milele.

Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa,

hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.

1134:11 Law 11:16-18; Ufu 18:2; Mao 2:8; Amo 7:8; Kum 14:15-17; Yoe 3:19; 2Fal 21:13Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki,

bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo.

Mungu atanyoosha juu ya Edomu

kamba ya kupimia ya machafuko matupu,

na timazi ya ukiwa.

1234:12 Isa 41:11-12; Za 107:10; Ay 12:21; Isa 40:23; Eze 24:5; Yer 39:6Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote

kitakachoitwa ufalme huko,

nao wakuu wao wote watatoweka.

1334:13 Hos 9:6; Isa 32:13; 13:22; Yer 9:11; Isa 7:19; Za 44:19Miiba itaenea katika ngome za ndani,

viwawi na michongoma itaota

kwenye ngome zake.

Itakuwa maskani ya mbweha,

makao ya bundi.

1434:14 Za 74:14; Isa 13:22; Ufu 18:2Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi,

nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana;

huko viumbe vya usiku vitastarehe pia

na kujitafutia mahali pa kupumzika.

1534:15 Za 17:8; Kum 14:13Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai,

atayaangua na kutunza makinda yake

chini ya uvuli wa mabawa yake;

pia huko vipanga watakusanyika,

kila mmoja na mwenzi wake.

1634:16 Isa 30:8; Dan 7:10; Isa 1:20; 58:14; 48:13Angalieni katika gombo la Bwana na msome:

Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana,

hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake.

Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza,

na Roho wake atawakusanya pamoja.

1734:17 Za 78:55; Isa 17:14; Yer 13:25Huwagawia sehemu zao,

mkono wake huwagawanyia kwa kipimo.

Wataimiliki hata milele

na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

Hoffnung für Alle

Jesaja 34:1-17

Gottes unerbittliches Gericht über die Völker

1Ihr Völker, kommt her und passt gut auf! Alle Welt soll es hören, ja, die ganze Erde und was auf ihr lebt: 2Der Herr ist zornig über alle Völker, ihre Heere werden seinen schrecklichen Zorn zu spüren bekommen. Er hat sie dem Untergang geweiht, abgeschlachtet sollen sie werden. 3Dann liegen die Leichen herum, und niemand beerdigt sie. Widerlicher Verwesungsgestank erfüllt die Luft. Das Blut der Erschlagenen durchtränkt die Berge. 4Die Gestirne vergehen, der Himmel wird zusammengerollt wie eine Schriftrolle. Die Sterne fallen herab wie dürre Weinblätter, wie trockene Blätter vom Feigenbaum.

5Der Herr sagt: »Mein Schwert im Himmel ist berauscht vom Blut34,5 Wörtlich: ist vollgetrunken. – Dieser bildliche Ausdruck ist nicht sicher zu deuten.. Es fährt auf das Land Edom nieder und vollstreckt mein Urteil. Dieses Volk habe ich dem Untergang geweiht.« 6Das Schwert des Herrn trieft von ihrem Blut und Fett, so wie es beim Schlachten vom Blut der Lämmer und Böcke trieft, wie es bedeckt ist vom Nierenfett der Schafböcke. Denn in Bozra, der Hauptstadt von Edom, feiert der Herr ein Opferfest. Ja, in ganz Edom ist großer Schlachttag. 7Die Menschen werden niedergemetzelt wie Büffel, Rinder und Stiere. Ihr Blut durchtränkt das ganze Land, der Boden trieft von ihrem Fett. 8Das alles wird geschehen, wenn der Herr mit seinen Feinden abrechnet.

In diesem Jahr zahlt er ihnen alles Unrecht heim, das sie an Zion verübt haben. 9Dann wird das Wasser der Bäche in Edom zu Pech, und der Boden verwandelt sich in Schwefel. Das ganze Land steht in Flammen wie eine Fackel, 10Tag und Nacht erlischt das Feuer nicht. Unaufhörlich steigt schwarzer Rauch zum Himmel auf. Generationen kommen und gehen, doch dieses Land bleibt verwüstet für alle Zeiten. Nie mehr wird ein Mensch diese öde Gegend durchstreifen. 11Eulen und Igel hausen dort, Käuzchen und Raben lassen sich nieder. Gott nimmt genau Maß, um das Land zu verwüsten. Er steckt die Grenzen ab, um es für immer unbewohnbar zu machen. 12Keine Fürsten rufen je wieder ein Königtum aus, von den vornehmen Herren bleibt niemand übrig. 13An den Mauern der Paläste ranken Dornen empor, Nesseln und Disteln überwuchern die alten Festungen. Schakale wohnen in den Ruinen, und Strauße siedeln sich an. 14Hyänen und andere Wüstentiere hausen dort, Dämonen begegnen einander, und Gespenster34,14 Wörtlich: Lilit. – Vermutlich der Name eines dämonischen Wesens in der antiken Mythologie. lassen sich nieder. 15Schlangen nisten dort, legen Eier und brüten sie aus, bis die Jungen schlüpfen. Auch Aasgeier zieht es in großer Zahl dorthin.

16Forscht im Buch des Herrn und lest nach: Nicht eines dieser Wesen fehlt, alle finden sich in Edom. Denn der Herr selbst hat es befohlen, und sein Geist bringt sie dort zusammen. 17Eigenhändig wird er das Land vermessen und jedem Tier durch das Los sein Gebiet zuweisen. Dann besitzen sie es für alle Zeiten, eine Generation nach der anderen wird darin wohnen.