Ufalme Wa Haki
132:1 2Nya 31:20; Eze 37:24; Za 72:1-4; Yer 23:5; Isa 28:6; Za 149:2; Isa 6:5Tazama, mfalme atatawala kwa uadilifu
na watawala watatawala kwa haki.
232:2 1Fal 18:4; Isa 4:6; Za 55:8; 23:2; Isa 49:10; Yer 31:9; Za 107:35Kila mtu atakuwa kama kivuli cha kujificha kutokana na upepo
na kimbilio kutokana na dhoruba,
kama vijito vya maji jangwani
na kivuli cha mwamba mkubwa katika ardhi yenye kiu.
332:3 Isa 29:18; 42:7, 16; Kum 29:4Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena,
nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.
432:4 Isa 6:10; 29:24; 35:6Moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu na kuelewa,
nao ulimi wenye kigugumizi utanena kwa ufasaha.
532:5 1Sam 25:25Mpumbavu hataitwa tena muungwana,
wala mtu mbaya kabisa kupewa heshima ya juu.
632:6 Isa 3:15; Mit 19:3; Isa 9:16-17; Mit 24:2; Isa 26:10Kwa kuwa mpumbavu hunena upumbavu,
moyo wake hushughulika na uovu:
Hutenda mambo yasiyo ya kumcha Mungu,
na hueneza habari za makosa kuhusu Bwana;
yeye huwaacha wenye njaa bila kitu,
na wenye kiu huwanyima maji.
732:7 Yer 5:26-28; Dan 12:10; Mik 7:3; Isa 29:19-20; Za 72:4; Isa 29:21Taratibu za mtu mbaya kabisa ni ovu,
hufanya mipango miovu
ili kumwangamiza maskini kwa uongo,
hata wakati ambapo hoja za mhitaji ni za haki.
832:8 1Nya 29:9; Mit 11:25; Isa 14:24Lakini mtu muungwana hufanya mipango ya kiungwana,
na kwa matendo ya kiungwana yeye hufanikiwa.
Wanawake Wa Yerusalemu
932:9 Isa 28:23; Dan 4:4; Amo 6:1; Sef 2:15Enyi wanawake wenye kuridhika sana,
amkeni na mnisikilize.
Enyi binti mnaojisikia kuwa salama,
sikieni lile ninalotaka kuwaambia!
1032:10 Isa 5:5-6; 24:7; 37:30Muda zaidi kidogo ya mwaka mmoja,
ninyi mnaojisikia salama mtatetemeka,
mavuno ya zabibu yatakoma
na mavuno ya matunda hayatakuwepo.
1132:11 Nah 3:5; Mik 1:8; Isa 34:14; 47:2; 3:24Tetemekeni, enyi wanawake wenye kuridhika,
tetemekeni kwa hofu, enyi binti mnaojisikia salama!
Vueni nguo zenu,
vaeni nguo ya gunia viunoni mwenu.
1232:12 Nah 2:7; Isa 16:9Pigeni matiti yenu kwa ajili ya mashamba mazuri,
kwa ajili ya mizabibu iliyozaa vizuri
1332:13 Hos 9:6; 10:8; Isa 23:7; 24:11na kwa ajili ya nchi ya watu wangu,
nchi ambayo miiba na michongoma imemea:
naam, ombolezeni kwa ajili ya nyumba zote za furaha
na kwa ajili ya mji huu wenye kufanya sherehe.
1432:14 Isa 13:22; 27:10; 2:15; 34:13; 6:11; 5:17; Za 104:11Ngome itaachwa,
mji wenye kelele nyingi utahamwa,
ngome ndani ya mji na mnara wa ulinzi vitakuwa ukiwa milele,
mahali pazuri pa punda na malisho ya makundi ya kondoo,
1532:15 Yoe 2:28; Eze 37:9; Za 107:35; Isa 29:17; 11:2mpaka Roho amwagwe juu yetu kutoka juu,
nalo jangwa kuwa shamba lenye rutuba,
na shamba lenye rutuba kuwa kama msitu.
1632:16 Isa 9:7; 28:6; 35:1, 6; 42:11; Za 48:1; Isa 1:26Haki itakaa katika jangwa,
na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba.
1732:17 Za 85:10; 119:165; Rum 14:17; Ebr 12:11Matunda ya haki yatakuwa amani,
matokeo ya haki yatakuwa utulivu
na matumaini milele.
1832:18 Yos 1:13; 11:18; Hos 2:18-23; Amo 9:14Watu wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani,
katika nyumba zilizo salama,
katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.
1932:19 Isa 19:18; 24:10; 28:17; 30:30; Zek 11:2; Ay 40:11Hata kama mvua ya mawe iangushe msitu
na mji ubomolewe kabisa,
2032:20 Mhu 11:1; Isa 30:24; Ay 39:8; Kum 28:12tazama jinsi utakavyobarikiwa,
ukipanda mbegu yako katika kila kijito,
na kuwaacha ngʼombe wako
na punda wajilishe kwa uhuru.
The Kingdom of Righteousness
1See, a king will reign in righteousness
and rulers will rule with justice.
2Each one will be like a shelter from the wind
and a refuge from the storm,
like streams of water in the desert
and the shadow of a great rock in a thirsty land.
3Then the eyes of those who see will no longer be closed,
and the ears of those who hear will listen.
4The fearful heart will know and understand,
and the stammering tongue will be fluent and clear.
5No longer will the fool be called noble
nor the scoundrel be highly respected.
6For fools speak folly,
their hearts are bent on evil:
They practice ungodliness
and spread error concerning the Lord;
the hungry they leave empty
and from the thirsty they withhold water.
7Scoundrels use wicked methods,
they make up evil schemes
to destroy the poor with lies,
even when the plea of the needy is just.
8But the noble make noble plans,
and by noble deeds they stand.
The Women of Jerusalem
9You women who are so complacent,
rise up and listen to me;
you daughters who feel secure,
hear what I have to say!
10In little more than a year
you who feel secure will tremble;
the grape harvest will fail,
and the harvest of fruit will not come.
11Tremble, you complacent women;
shudder, you daughters who feel secure!
Strip off your fine clothes
and wrap yourselves in rags.
12Beat your breasts for the pleasant fields,
for the fruitful vines
13and for the land of my people,
a land overgrown with thorns and briers—
yes, mourn for all houses of merriment
and for this city of revelry.
14The fortress will be abandoned,
the noisy city deserted;
citadel and watchtower will become a wasteland forever,
the delight of donkeys, a pasture for flocks,
15till the Spirit is poured on us from on high,
and the desert becomes a fertile field,
and the fertile field seems like a forest.
16The Lord’s justice will dwell in the desert,
his righteousness live in the fertile field.
17The fruit of that righteousness will be peace;
its effect will be quietness and confidence forever.
18My people will live in peaceful dwelling places,
in secure homes,
in undisturbed places of rest.
19Though hail flattens the forest
and the city is leveled completely,
20how blessed you will be,
sowing your seed by every stream,
and letting your cattle and donkeys range free.