Isaya 32 – NEN & HCV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 32:1-20

Ufalme Wa Haki

132:1 2Nya 31:20; Eze 37:24; Za 72:1-4; Yer 23:5; Isa 28:6; Za 149:2; Isa 6:5Tazama, mfalme atatawala kwa uadilifu

na watawala watatawala kwa haki.

232:2 1Fal 18:4; Isa 4:6; Za 55:8; 23:2; Isa 49:10; Yer 31:9; Za 107:35Kila mtu atakuwa kama kivuli cha kujificha kutokana na upepo

na kimbilio kutokana na dhoruba,

kama vijito vya maji jangwani

na kivuli cha mwamba mkubwa katika ardhi yenye kiu.

332:3 Isa 29:18; 42:7, 16; Kum 29:4Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena,

nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.

432:4 Isa 6:10; 29:24; 35:6Moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu na kuelewa,

nao ulimi wenye kigugumizi utanena kwa ufasaha.

532:5 1Sam 25:25Mpumbavu hataitwa tena muungwana,

wala mtu mbaya kabisa kupewa heshima ya juu.

632:6 Isa 3:15; Mit 19:3; Isa 9:16-17; Mit 24:2; Isa 26:10Kwa kuwa mpumbavu hunena upumbavu,

moyo wake hushughulika na uovu:

Hutenda mambo yasiyo ya kumcha Mungu,

na hueneza habari za makosa kuhusu Bwana;

yeye huwaacha wenye njaa bila kitu,

na wenye kiu huwanyima maji.

732:7 Yer 5:26-28; Dan 12:10; Mik 7:3; Isa 29:19-20; Za 72:4; Isa 29:21Taratibu za mtu mbaya kabisa ni ovu,

hufanya mipango miovu

ili kumwangamiza maskini kwa uongo,

hata wakati ambapo hoja za mhitaji ni za haki.

832:8 1Nya 29:9; Mit 11:25; Isa 14:24Lakini mtu muungwana hufanya mipango ya kiungwana,

na kwa matendo ya kiungwana yeye hufanikiwa.

Wanawake Wa Yerusalemu

932:9 Isa 28:23; Dan 4:4; Amo 6:1; Sef 2:15Enyi wanawake wenye kuridhika sana,

amkeni na mnisikilize.

Enyi binti mnaojisikia kuwa salama,

sikieni lile ninalotaka kuwaambia!

1032:10 Isa 5:5-6; 24:7; 37:30Muda zaidi kidogo ya mwaka mmoja,

ninyi mnaojisikia salama mtatetemeka,

mavuno ya zabibu yatakoma

na mavuno ya matunda hayatakuwepo.

1132:11 Nah 3:5; Mik 1:8; Isa 34:14; 47:2; 3:24Tetemekeni, enyi wanawake wenye kuridhika,

tetemekeni kwa hofu, enyi binti mnaojisikia salama!

Vueni nguo zenu,

vaeni nguo ya gunia viunoni mwenu.

1232:12 Nah 2:7; Isa 16:9Pigeni matiti yenu kwa ajili ya mashamba mazuri,

kwa ajili ya mizabibu iliyozaa vizuri

1332:13 Hos 9:6; 10:8; Isa 23:7; 24:11na kwa ajili ya nchi ya watu wangu,

nchi ambayo miiba na michongoma imemea:

naam, ombolezeni kwa ajili ya nyumba zote za furaha

na kwa ajili ya mji huu wenye kufanya sherehe.

1432:14 Isa 13:22; 27:10; 2:15; 34:13; 6:11; 5:17; Za 104:11Ngome itaachwa,

mji wenye kelele nyingi utahamwa,

ngome ndani ya mji na mnara wa ulinzi vitakuwa ukiwa milele,

mahali pazuri pa punda na malisho ya makundi ya kondoo,

1532:15 Yoe 2:28; Eze 37:9; Za 107:35; Isa 29:17; 11:2mpaka Roho amwagwe juu yetu kutoka juu,

nalo jangwa kuwa shamba lenye rutuba,

na shamba lenye rutuba kuwa kama msitu.

1632:16 Isa 9:7; 28:6; 35:1, 6; 42:11; Za 48:1; Isa 1:26Haki itakaa katika jangwa,

na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba.

1732:17 Za 85:10; 119:165; Rum 14:17; Ebr 12:11Matunda ya haki yatakuwa amani,

matokeo ya haki yatakuwa utulivu

na matumaini milele.

1832:18 Yos 1:13; 11:18; Hos 2:18-23; Amo 9:14Watu wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani,

katika nyumba zilizo salama,

katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.

1932:19 Isa 19:18; 24:10; 28:17; 30:30; Zek 11:2; Ay 40:11Hata kama mvua ya mawe iangushe msitu

na mji ubomolewe kabisa,

2032:20 Mhu 11:1; Isa 30:24; Ay 39:8; Kum 28:12tazama jinsi utakavyobarikiwa,

ukipanda mbegu yako katika kila kijito,

na kuwaacha ngʼombe wako

na punda wajilishe kwa uhuru.

Hindi Contemporary Version

यशायाह 32:1-20

धार्मिकता का राज्य

1देखो, राजा धर्म से शासन करेंगे

और अधिकारी न्याय से शासन करेंगे.

2सब मानो आंधी से छिपने

का स्थान और बौछार के लिये आड़ के समान होगा,

मरुभूमि में झरने

एक विशाल चट्टान की छाया के समान होंगे.

3तब जो देखते हैं, उनकी आंख कमजोर न होगी,

और जो सुनते हैं वे सुनेंगे.

4उतावले लोगों के मन ज्ञान की बातें समझेंगे,

और जो हकलाते हैं वे साफ़ बोलेंगे.

5मूर्ख फिर उदार न कहलायेगा

न कंजूस दानी कहलायेगा.

6क्योंकि एक मूर्ख मूढ़ता की बातें ही करता है,

और उसका मन व्यर्थ बातों पर ही लगा रहता है:

वह कपट और याहवेह के विषय में झूठ बोलता है

जिससे वह भूखे को भूखा और प्यासे को प्यासा ही रख सके.

7दुष्ट गलत बात सोचता है,

और सीधे लोगों को भी अपनी बातों में फंसा देता है.

8किंतु सच्चा व्यक्ति तो अच्छा ही करता है,

और अच्छाईयों पर स्थिर रहता है.

येरूशलेम की स्त्रियां

9हे आलसी स्त्रियों तुम जो निश्चिंत हो,

मेरी बात को सुनो;

हे निश्चिंत पुत्रियो उठो,

मेरे वचन पर ध्यान दो!

10हे निश्चिंत पुत्रियो एक वर्ष

और कुछ ही दिनों में तुम व्याकुल कर दी जाओगी;

क्योंकि दाख का समय खत्म हो गया है,

और फल एकत्र नहीं किए जाएंगे.

11हे निश्चिंत स्त्रियो, कांपो;

कांपो, हे निश्चिंत पुत्रियो!

अपने वस्त्र उतारकर

अपनी कमर पर टाट बांध लो.

12अच्छे खेतों के लिए

और फलदार अंगूर के लिये रोओ,

13क्योंकि मेरी प्रजा,

जो बहुत खुश और आनंदित है,

उनके खेत में झाड़

और कांटे उग रहे हैं.

14क्योंकि राजमहल छोड़ दिया जायेगा,

और नगर सुनसान हो जायेगा;

पर्वत और उनके पहरेदारों के घर जहां है,

वहां जंगली गधे मौज करेंगे, पालतू पशुओं की चराई बन जाएंगे.

15जब तक हम पर ऊपर से आत्मा न उंडेला जाए,

और मरुभूमि फलदायक खेत न बन जाए,

और फलदायक खेत वन न बन जाए.

16तब तक उस बंजर भूमि में याहवेह का न्याय रहेगा,

और फलदायक खेत में धर्म रहेगा.

17धार्मिकता का फल है शांति, उसका परिणाम चैन;

और हमेशा के लिए साहस!

18तब मेरे लोग शांति से,

और सुरक्षित एवं स्थिर रहेंगे.

19और वन विनाश होगा

और उस नगर का घमंड चूर-चूर किया जाएगा,

20क्या ही धन्य हो तुम,

जो जल के स्रोतों के पास बीज बोते हो,

और गधे और बैल को आज़ादी से चराते हो.