Isaya 28 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 28:1-29

Ole Wa Efraimu

128:1 Isa 7:2; Law 10:9; Amo 6:6; Isa 10:5; 9:9; Hos 7:5; Isa 5:11; 8:7Ole kwa lile taji la maua, kiburi cha walevi wa Efraimu,

kwa ua linalosinyaa, uzuri wa utukufu wake,

uliowekwa kwenye kichwa cha bonde lenye rutuba:

kwa ule mji, kiburi cha wale walioshushwa na mvinyo!

228:2 Isa 30:30; 40:10; Yos 10:11; Eze 13:11; Isa 29:6; 8:7; Dan 9:26Tazama, Bwana anaye mmoja aliye na uwezo na nguvu.

Kama dhoruba ya mvua ya mawe na upepo uharibuo,

kama mvua inyeshayo kwa nguvu na mafuriko yashukayo,

atakiangusha chini kwa nguvu.

328:3 Ay 40:12; Isa 5:5Lile taji la maua, kiburi cha walevi cha Efraimu,

kitakanyagwa chini ya nyayo.

428:4 Wim 2:13; Nah 3:12; Hos 9:10Lile ua linalosinyaa, uzuri wa utukufu wake,

uliowekwa kwenye kichwa cha bonde lenye rutuba,

litakuwa kama tini iliyoiva kabla ya mavuno:

mara mtu aionapo, huichuma na kuila.

528:5 Zek 9:16; Eze 21:26; Isa 10:20; 1:9; 29:18; Yer 13:18; Eze 16:12; Isa 62:3Katika siku ile, Bwana Mwenye Nguvu Zote

atakuwa taji la utukufu,

taji zuri la maua

kwa mabaki ya watu wake.

628:6 Amu 9:44-45; 2Sam 14:20; 2Nya 32:8; Yn 5:30; Isa 11:2-4Atakuwa roho ya haki

kwa yeye aketiye katika kiti cha hukumu,

chanzo cha nguvu

kwa wale wazuiao vita langoni.

728:7 Law 10:9; Isa 56:10-12; Efe 5:18; Za 107:27; Isa 24:2; 3:12; 22:13; 9:15Hawa pia wanapepesuka kwa sababu ya mvinyo,

wanayumbayumba kwa sababu ya kileo:

Makuhani na manabii wanapepesuka kwa sababu ya kileo,

wanachanganyikiwa kwa sababu ya mvinyo;

wanapepesuka wanapoona maono,

wanajikwaa wanapotoa maamuzi.

828:8 Yer 48:26Meza zote zimejawa na matapishi

wala hakuna sehemu hata ndogo

isiyokuwa na uchafu.

928:9 Yer 6:10; 1Pet 2:2; Za 32:8; Ebr 5:12-13; Yer 31:34; Isa 30:20; 48:17; 54:13“Yeye anajaribu kumfundisha nani?

Yeye anamwelezea nani ujumbe wake?

Je, ni kwa watoto walioachishwa kunyonya?

Je, ni wale ambao ndipo tu wametolewa matitini?

1028:10 Isa 29:13Kwa maana ni:

Amri juu ya amri, amri juu ya amri,

kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni;

hapa kidogo, kule kidogo.”

1128:11 Yer 5:15; 1Kor 14:21; Mwa 11:7; Eze 3:5; Isa 33:19Sawa kabisa, kwa midomo migeni

na kwa lugha ngeni,

Mungu atasema na watu hawa,

1228:12 Yos 1:13; Mt 11:28-29; 2Nya 14:7; Kut 14:14; Ay 11:18; Isa 11:10wale ambao aliwaambia,

“Hapa ni mahali pa kupumzika,

waliochoka na wapumzike,”

na, “Hapa ni mahali pa mapumziko,”

lakini hawakutaka kusikiliza.

1328:13 Mt 21:44; Isa 8:14-15Hivyo basi, neno la Bwana kwao litakuwa:

Amri juu ya amri, amri juu ya amri,

kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni,

hapa kidogo, kule kidogo:

ili waende na kuanguka chali,

wakijeruhiwa, wakinaswa na kukamatwa.

1428:14 Isa 1:10; 2Nya 36:16Kwa hiyo sikieni neno la Bwana, enyi watu wenye dharau

mnaotawala watu hawa wa Yerusalemu.

1528:15 Dan 11:22; Isa 9:15; 10:26; Ay 5:23; Isa 8:19; Amu 9:35; Isa 29:15; Yer 23:24Ninyi mnajisifu, “Tumefanya agano na mauti,

tumefanya mapatano na kuzimu.

Wakati pigo lifurikalo litakapopita,

haliwezi kutugusa sisi,

kwa kuwa tumefanya uongo kuwa kimbilio letu

na miungu ya uongo kuwa mahali petu pa kujificha.”

1628:16 Zek 12:3; Efe 2:20; Rum 9:33; 1Pet 2:6; Isa 54:4; 14:32; Za 118:22; Isa 8:14-15; Dan 2:34-45; Mdo 4:11; Yer 51:26; 1Kor 3:11Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenyezi asemavyo:

“Tazama, ninaweka jiwe katika Sayuni,

jiwe lililojaribiwa,

jiwe la pembeni la thamani kwa ajili ya msingi thabiti.

Yeye atumainiye kamwe hatatiwa hofu.

1728:17 Isa 5:16; Za 11:7; 2Fal 21:13; Yos 10:11Nitaifanya haki kuwa kamba ya kupimia

na uadilifu kuwa timazi;

mvua ya mawe itafagia kimbilio lenu, huo uongo,

nayo maji yatafurikia mahali penu pa kujificha.

1828:18 Isa 63:18; Dan 8:13; Isa 7:7Agano lenu na kifo litabatilishwa,

patano lenu na kuzimu halitasimama.

Wakati pigo lifurikalo litakapowakumba,

litawaangusha chini.

1928:19 2Fal 24:2; Ay 18:11; Za 5:3Kila mara lijapo litawachukua,

asubuhi baada ya asubuhi,

wakati wa mchana na wakati wa usiku,

litawakumba tangu mwanzo hadi mwisho.”

Kuuelewa ujumbe huu

utaleta hofu tupu.

2028:20 Isa 59:6Kitanda ni kifupi mno kujinyoosha juu yake,

nguo ya kujifunikia ni nyembamba mno

mtu hawezi kujifunikia.

2128:21 2Sam 5:20; Mwa 38:29; 1Nya 14:11-16; Lk 19:41-44; Yos 9:3; Isa 65:7Bwana atainuka kama alivyofanya kwenye Mlima Perasimu,

ataghadhibika kama alivyofanya katika Bonde la Gibeoni:

ili kufanya kazi yake, kazi yake ya ajabu,

ili kutimiza kazi yake, kazi yake ngeni.

2228:22 Isa 10:22; Yer 29:18; 2Nya 36:16; Mao 2:15; Sef 2:15Sasa acheni dharau zenu,

la sivyo minyororo yenu itakuwa mizito zaidi.

Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, ameniambia

habari za maangamizi yaliyoamriwa dhidi ya nchi yote.

2328:23 Isa 32:9Sikilizeni msikie sauti yangu,

tegeni masikio na msikie niyasemayo.

2428:24 Mhu 3:2Wakati mkulima alimapo ili apande,

je, hulima siku zote?

Je, huendelea kubomoa ardhi

na kusawazisha udongo?

2528:25 Kut 9:32; Mt 23:23; Eze 4:9Akiisha kusawazisha shamba,

je, hatapanyi mbegu za bizari na kutawanya jira?

Je, hapandi ngano katika sehemu yake,

shayiri katika eneo lake,

na nafaka nyingine katika shamba lake?

2628:26 Za 94:10Mungu wake humwelekeza

na kumfundisha njia iliyo sahihi.

2728:27 Isa 21:10; Ay 41:30; Isa 10:5Iliki haipurwi kwa nyundo,

wala gurudumu la gari halivingirishwi juu ya jira;

iliki hupurwa kwa fimbo,

na jira kwa ufito.

2828:28 Isa 21:10Nafaka lazima isagwe ili kutengeneza mkate,

kwa hiyo mtu haendelei kuipura daima.

Ingawa huendesha magurudumu ya gari lake la kupuria juu yake,

farasi wake hawasagi.

2928:29 Yer 32:19; Za 92:5; Rum 11:33; Isa 9:5Haya yote pia hutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote,

mwenye mashauri ya ajabu, na anayepita wote kwa hekima.

King James Version

Isaiah 28:1-29

1Woe to the crown of pride, to the drunkards of Ephraim, whose glorious beauty is a fading flower, which are on the head of the fat valleys of them that are overcome with wine!28.1 overcome: Heb. broken 2Behold, the Lord hath a mighty and strong one, which as a tempest of hail and a destroying storm, as a flood of mighty waters overflowing, shall cast down to the earth with the hand. 3The crown of pride, the drunkards of Ephraim, shall be trodden under feet:28.3 under…: Heb. with feet 4And the glorious beauty, which is on the head of the fat valley, shall be a fading flower, and as the hasty fruit before the summer; which when he that looketh upon it seeth, while it is yet in his hand he eateth it up.28.4 eateth: Heb. swalloweth

5¶ In that day shall the LORD of hosts be for a crown of glory, and for a diadem of beauty, unto the residue of his people, 6And for a spirit of judgment to him that sitteth in judgment, and for strength to them that turn the battle to the gate.

7¶ But they also have erred through wine, and through strong drink are out of the way; the priest and the prophet have erred through strong drink, they are swallowed up of wine, they are out of the way through strong drink; they err in vision, they stumble in judgment. 8For all tables are full of vomit and filthiness, so that there is no place clean.

9¶ Whom shall he teach knowledge? and whom shall he make to understand doctrine? them that are weaned from the milk, and drawn from the breasts.28.9 doctrine: Heb. the hearing? 10For precept must be upon precept, precept upon precept; line upon line, line upon line; here a little, and there a little:28.10 must be: or, hath been 11For with stammering lips and another tongue will he speak to this people.28.11 stammering…: Heb. stammerings of lip28.11 will…: or, he hath spoken 12To whom he said, This is the rest wherewith ye may cause the weary to rest; and this is the refreshing: yet they would not hear. 13But the word of the LORD was unto them precept upon precept, precept upon precept; line upon line, line upon line; here a little, and there a little; that they might go, and fall backward, and be broken, and snared, and taken.

14¶ Wherefore hear the word of the LORD, ye scornful men, that rule this people which is in Jerusalem. 15Because ye have said, We have made a covenant with death, and with hell are we at agreement; when the overflowing scourge shall pass through, it shall not come unto us: for we have made lies our refuge, and under falsehood have we hid ourselves:

16¶ Therefore thus saith the Lord GOD, Behold, I lay in Zion for a foundation a stone, a tried stone, a precious corner stone, a sure foundation: he that believeth shall not make haste. 17Judgment also will I lay to the line, and righteousness to the plummet: and the hail shall sweep away the refuge of lies, and the waters shall overflow the hiding place.

18¶ And your covenant with death shall be disannulled, and your agreement with hell shall not stand; when the overflowing scourge shall pass through, then ye shall be trodden down by it.28.18 trodden…: Heb. a treading down to it 19From the time that it goeth forth it shall take you: for morning by morning shall it pass over, by day and by night: and it shall be a vexation only to understand the report.28.19 to…: or, when he shall make you to understand doctrine 20For the bed is shorter than that a man can stretch himself on it: and the covering narrower than that he can wrap himself in it. 21For the LORD shall rise up as in mount Perazim, he shall be wroth as in the valley of Gibeon, that he may do his work, his strange work; and bring to pass his act, his strange act. 22Now therefore be ye not mockers, lest your bands be made strong: for I have heard from the Lord GOD of hosts a consumption, even determined upon the whole earth.

23¶ Give ye ear, and hear my voice; hearken, and hear my speech. 24Doth the plowman plow all day to sow? doth he open and break the clods of his ground? 25When he hath made plain the face thereof, doth he not cast abroad the fitches, and scatter the cummin, and cast in the principal wheat and the appointed barley and the rie in their place?28.25 the principal…: or, the wheat in the principal place, and barley in the appointed place28.25 rie: or, spelt28.25 place: Heb. border? 26For his God doth instruct him to discretion, and doth teach him.28.26 For…: or, And he bindeth it in such sort as his God doth teach him 27For the fitches are not threshed with a threshing instrument, neither is a cart wheel turned about upon the cummin; but the fitches are beaten out with a staff, and the cummin with a rod. 28Bread corn is bruised; because he will not ever be threshing it, nor break it with the wheel of his cart, nor bruise it with his horsemen. 29This also cometh forth from the LORD of hosts, which is wonderful in counsel, and excellent in working.