Isaya 15 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 15:1-9

Unabii Dhidi Ya Moabu

115:1 Hes 21:28; 22:3-6; Kum 23:6; Hes 17:12; Yer 51:58; 48:24; 2Fal 3:25Neno kuhusu Moabu:

Ari iliyo Moabu imeangamizwa:

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

Kiri iliyo Moabu imeangamizwa,

imeharibiwa kwa usiku mmoja!

215:2 Yer 48:35; Law 21:5; Ay 1:20; Hes 21:20; Isa 16:12; 2Sam 10:4; Law 13:40Diboni anakwea hadi kwenye hekalu lake,

mpaka mahali pake pa juu ili walie,

Moabu anaombolezea Nebo na Medeba.

Kila kichwa kimenyolewa

na kila ndevu limeondolewa.

315:3 Mao 2:11; Mik 1:8; Isa 3:24; Yos 2:8; Yer 48:38; Isa 14:31; Eze 7:18; Yer 47:2Wamevaa nguo za magunia barabarani,

juu ya mapaa na kwenye viwanja

wote wanaomboleza,

wamelala kifudifudi kwa kulia.

415:4 Hes 32:3; 21:23-25; Yos 13:26Heshboni na Eleale wanalia,

sauti zao zinasikika hadi Yahazi.

Kwa hiyo watu wenye silaha wa Moabu wanapiga kelele,

nayo mioyo yao imezimia.

515:5 Isa 16:11; Yer 48:31; 48:3-5; 4:20; Mwa 13:10; Hes 21:29Moyo wangu unamlilia Moabu;

wakimbizi wake wanakimbilia Soari,

hadi Eglath-Shelishiya.

Wanapanda njia ya kwenda Luhithi,

wanakwenda huku wanalia;

barabarani iendayo Horonaimu

wanaombolezea maangamizi yao.

615:6 Isa 19:5-7; Za 37:2; Hos 4:3; Yer 48:34; Isa 16:8; 33:9; 14:17; Yer 14:5Maji ya Nimrimu yamekauka

na majani yamenyauka;

mimea imekauka wala hakuna

kitu chochote kibichi kilichobaki.

715:7 Isa 30:6; Yer 48:36Kwa hiyo mali waliyoipata na kujiwekea akiba

wamezichukua na kuvuka Bonde la Mierebi.

815:8 Hes 21:16Mwangwi wa kilio chao umefika hadi mpakani mwa Moabu,

kilio chao cha huzuni kimefika hadi Eglaimu,

maombolezo yao hadi Beer-Elimu.

915:9 2Fal 17:25; Eze 25:8-11Maji ya Dimoni yamejaa damu,

lakini bado nitaleta pigo jingine juu ya Dimoni:

simba juu ya wakimbizi wa Moabu

na juu ya wale wanaobaki katika nchi.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Isaías 15:1-9

Profecía contra Moab

16:6-12Jer 48:29-36

1Profecía contra Moab:

La ciudad moabita de Ar está arruinada,

¡destruida en una noche!

La ciudad moabita de Quir está arruinada,

¡destruida en una noche!

2Acuden los de Dibón al templo,

a sus altares paganos, para llorar.

Moab está gimiendo

por Nebo y por Medeba.

Rapadas están todas las cabezas,

y afeitadas todas las barbas.

3Todos, deshechos en llanto,

van por las calles, vestidos de luto;

¡gimen en los techos y en las plazas!

4Hesbón y Elalé claman a gritos,

hasta Yahaza se escuchan sus clamores.

Por eso gritan los valientes de Moab,

y flaquea su entereza.

5Mi corazón grita por Moab;

sus fugitivos huyen hasta Zoar,

hasta Eglat Selisiyá.

Suben llorando por la cuesta de Luhit;

ante el desastre, gritan desesperados

por el camino de Joronayin.

6Se han secado las aguas de Nimrín;

se ha marchitado la hierba.

Ya no hay vegetación,

no ha quedado nada verde.

7Por eso se llevaron,

más allá del arroyo de los Sauces,

las muchas riquezas que amasaron.

8Su grito desesperado

va recorriendo la frontera de Moab.

Llega su gemido hasta Eglayin,

y aun llega hasta Ber Elín.

9Llenas están de sangre las aguas de Dimón,

y aún más plagas le añadiré:

enviaré un león contra los moabitas fugitivos

y contra los que permanezcan en la tierra.