Isaya 13 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 13:1-22

Unabii Dhidi Ya Babeli

113:1 Isa 14:28; 21:9; 48:14; Ufu 14:8; Mwa 10:10; Mal 1:1; Isa 14:4; 46:1-2Neno kuhusu Babeli ambalo Isaya mwana wa Amozi aliliona:

213:2 Za 20:5; 50:2; Yer 51:27; 51:58; 50:2; Isa 24:12; 45:2; 24:2Twekeni bendera juu ya mlima usio na kitu,

wapazieni sauti,

wapungieni mkono waingie

katika malango ya wenye heshima.

313:3 Yer 51:11; Yoe 3:11; Za 149:2; Isa 21:2; Kum 5:28; Ay 40:11Nimewaamuru watakatifu wangu;

nimewaita mashujaa wangu waitimize hasira yangu:

wale wanaoshangilia ushindi wangu.

413:4 Yoe 3:14; Za 46:6; Isa 42:13; 47:4; Yer 50:41Sikilizeni kelele juu ya milima,

kama ile ya umati mkubwa wa watu!

Sikilizeni, makelele katikati ya falme,

kama mataifa yanayokusanyika pamoja!

Bwana Mwenye Nguvu Zote anakusanya

jeshi kwa ajili ya vita.

513:5 Yos 6:17; Isa 5:26; 34:2; 54:16; 10:25; 34:2; Yer 50:25Wanakuja kutoka nchi za mbali sana,

kutoka miisho ya mbingu,

Bwana na silaha za ghadhabu yake,

kuangamiza nchi yote.

613:6 Amo 5:18; Eze 30:2; Yak 5:1; Isa 2:12; 14:31; 10:3; 15:2Ombolezeni, kwa maana siku ya Bwana i karibu,

itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mwenyezi.13:6 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania.

713:7 Eze 21:7; Yos 2:11; 2Fal 19:26; Ay 4:3; Yer 47:3Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea,

moyo wa kila mtu utayeyuka.

813:8 Nah 2:10; Yoe 2:6; Za 31:13; Isa 21:4; Za 48:5; Kut 15:14; Mwa 3:16; Yn 16:21Hofu itawakamata,

uchungu na maumivu makali yatawashika,

watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa.

Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake,

nyuso zao zikiwaka kama moto.

913:9 Isa 2:12; Yer 6:23; 51:2; Isa 9:19; 66:16; Yer 25:31; Yoe 3:2Tazameni, siku ya Bwana inakuja,

siku katili, yenye ghadhabu na hasira kali,

kuifanya nchi kuwa ukiwa

na kuwaangamiza wenye dhambi waliomo ndani yake.

1013:10 Kut 10:22; Ufu 8:12; Amo 5:20; Zek 14:7; Ay 9:7; Mt 24:29; Isa 5:30; 24:23Nyota za mbinguni na makundi ya nyota

havitatoa mwanga wake.

Jua linalochomoza litatiwa giza

na mwezi hautatoa nuru yake.

1113:11 Isa 3:11; 26:21; 65:6-7; 49:25-26; Za 125:3; Mit 16:18; Dan 5:23; 4:37; Eze 28:2Nitauadhibu ulimwengu kwa ajili ya uovu wake,

waovu kwa ajili ya dhambi zao.

Nitakomesha majivuno ya wenye kiburi,

na nitakishusha kiburi cha watu wakatili.

1213:12 Isa 4:1; Mwa 10:29Nitawafanya wanadamu kuwa adimu kuliko dhahabu safi,

watakuwa wachache sana kuliko dhahabu ya Ofiri.

1313:13 Hag 2:6; Za 102:26; Isa 9:19; 14:16; 34:4; Mt 24:7; Ay 9:5; 9:6; Mk 13:8Kwa hiyo nitazifanya mbingu zitetemeke,

nayo dunia itatikisika kutoka mahali pake

katika ghadhabu ya Bwana Mwenye Nguvu Zote,

katika siku ya hasira yake iwakayo.

1413:14 Nah 3:7; Yn 10:11; Yer 51:9; 46:16; 4:9; Mit 6:5; Isa 17:13; 21:15; 33:3; Mt 9:36Kama swala awindwaye,

kama kondoo wasio na mchungaji,

kila mmoja atarudi kwa watu wake mwenyewe,

kila mmoja atakimbilia nchi yake ya kuzaliwa.

1513:15 Yer 50:25; 51:4; Isa 14:19Yeyote atakayetekwa atapasuliwa tumbo,

wote watakaokamatwa watauawa kwa upanga.

1613:16 Nah 3:10; Hes 16:27; 13:16; Mwa 34:29; 2Fal 8:12Watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande

mbele ya macho yao;

nyumba zao zitatekwa

na wake zao watatendwa jeuri.

1713:17 2Fal 18:14-16; Mit 19:24-25; Yer 51:11; 50:9, 41Tazama, nitawachochea Wamedi dhidi yao,

ambao hawajali fedha

wala hawafurahii dhahabu.

1813:18 Za 7:12; Isa 41:2; Yer 49:26Mishale yao itawaangusha vijana,

hawatakuwa na huruma kwa watoto wachanga

wala hawataangalia watoto kwa huruma.

1913:19 Dan 4:30; Za 137:8; Ufu 14:8; Mwa 19:24-25; Rum 9:29; Isa 47:5; Dan 2:37-38Babeli, johari ya falme,

utukufu wa kiburi cha Wababeli,13:19 Wababeli hapa maana yake ni Wakaldayo.

itaangushwa na Mungu

kama Sodoma na Gomora.

2013:20 Isa 14:23; 34:10-15; 2Nya 17:11; Yer 51:29, 37-43, 62Hautakaliwa na watu kamwe

wala watu hawataishi humo kwa vizazi vyote.

Hakuna Mwarabu atakayepiga hema lake huko,

hakuna mchungaji atakayepumzisha makundi yake huko.

2113:21 Za 74:14; Ufu 18:2; Yer 14:6; Law 11:16-18; Kum 14:15-17; 2Nya 11:15Lakini viumbe wa jangwani watalala huko,

mbweha watajaza nyumba zake,

bundi wataishi humo

nao mbuzi-mwitu watarukaruka humo.

2213:22 Isa 34:14; Kum 32:25; Yer 48:16; 9:11; Isa 25:2; 32:14; Yer 50:39; Mal 1:3Fisi watalia ndani ya ngome zake,

mbweha ndani ya majumba yake ya kifahari.

Wakati wake umewadia,

na siku zake hazitaongezwa.

Het Boek

Jesaja 13:1-22

De dagen van Babel zijn geteld

1Dit is de profetie die God aan Jesaja, de zoon van Amoz, over Babel gaf.

2Laat de vlaggen en de vaandels wapperen als de vijand tot de aanval overgaat. Roep naar hen, Israël, en geef een teken wanneer zij optrekken tegen Babel om de paleizen van de rijken en de machthebbers te vernietigen. 3Ik, de Here, heb mijn heilige legers bevel gegeven, Ik heb mijn helden opgeroepen mijn vonnis te voltrekken, ze juichen over mijn overwinning.

4Luister eens naar het rumoer in de bergen! Luister naar het geluid van het marcherende leger! Het is het lawaai en de roep van vele volken. Vanuit verre landen heeft de Here van de hemelse legers hen daar gebracht. 5Zij zijn de wapens die zijn hand tegen u, o Babel, hanteert. Zij dragen zijn toorn met zich mee en zullen uw hele land met de grond gelijk maken. 6Jammer, want de tijd van de Here is nu gekomen, de tijd dat de Almachtige u verwoest. 7Uw armen zijn verlamd door angst. De moedigste harten smelten en zijn bang. 8De angst grijpt u met pijnlijke scheuten, zoals de weeën een zwangere vrouw overvallen. U kijkt elkaar radeloos aan, de schrik staat op uw gezicht te lezen. 9Want kijk, de dag van de Here is in aantocht, de vreselijke dag van zijn verbolgenheid en vurige toorn. Het land zal worden vernietigd, evenals alle zondaars. 10De hemelen boven hen zullen donker zijn. De sterren, de zon en de maan zullen geen licht geven. 11En Ik zal de wereld straffen voor haar kwaad, alle inwoners voor hun zonden. Ik zal de arrogantie van de trotse man en de hooghartigheid van de rijke neerslaan. 12Mensen zullen schaars zijn als goud, zeldzamer dan het goud van Ofir. 13Want Ik zal de hemelen door elkaar schudden in mijn vreselijke toorn en de aarde zal van haar plaats worden gebracht. 14De legers van Babel zullen vluchten totdat zij uitgeput zijn. Zij trekken terug naar hun eigen land als een hert dat wordt achtervolgd door honden. Zij dwalen rond als schapen die alleen zijn gelaten door hun herder. 15Wie niet vlucht, zal neergestoken worden. 16Hun kinderen zullen voor hun ogen worden verpletterd, hun huizen geplunderd, hun vrouwen verkracht. 17Want Ik zal de Meden tegen Babel opzetten en geen enkel bedrag in zilver of goud zal hen kunnen afkopen. 18De aanvallende legers zullen geen medelijden hebben met de jonge mensen van Babel, met babyʼs of met kinderen. 19Zo zal Babel, het luisterrijkste van alle koninkrijken, de bloem van de Chaldese cultuur, net zo volledig worden verwoest als Sodom en Gomorra, toen de Here vuur uit de hemel stuurde. 20Babel zal voor eeuwig worden vernietigd. Generatie na generatie zal voorbij gaan, maar het land zal nooit meer worden bewoond. De nomaden zullen er zelfs geen kamp opslaan. En de herders zullen hun schapen er niet laten overnachten. 21Wilde woestijndieren zullen het bewonen en huilende beesten zullen zich in de vervallen huizen ophouden. Er zullen struisvogels leven en geesten zullen er komen om te dansen. 22Hyenaʼs en jakhalzen zullen in de paleizen rondlopen. De dagen van Babel zijn geteld, de dag van de verwoesting is nabij.