Hosea 4 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 4:1-19

Shtaka Dhidi Ya Israeli

14:1 Mit 10:21; 24:2; Mik 6:2; Isa 1:3; Ay 10:2; Yer 2:9; 7:28; 51:5; Hos 2:20Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli,

kwa sababu Bwana analo shtaka

dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi:

“Hakuna uaminifu, hakuna upendo,

hakuna kumjua Mungu katika nchi.

24:2 Isa 59:3; Hos 5:2; 6:2; 7:1; 11:12; Eze 22:2-9; 1Fal 21:16Kuna kulaani tu, uongo na uuaji,

wizi na uzinzi,

bila kuwa na mipaka,

nao umwagaji damu mmoja

baada ya mwingine.

34:3 Yer 4:25, 28; 9:10; Amo 8:8; Isa 15:6; 33:9; Sef 1:3Kwa sababu hii nchi huomboleza,

wote waishio ndani mwake wanadhoofika,

wanyama wa kondeni, ndege wa angani

na samaki wa baharini wanakufa.

44:4 Kum 17:12; Eze 3:26“Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka,

mtu yeyote na asimlaumu mwenzake,

kwa maana watu wako ni kama wale

waletao mashtaka dhidi ya kuhani.

54:5 Eze 7:19; 14:7; Hos 2:2Unajikwaa usiku na mchana,

nao manabii hujikwaa pamoja nawe.

Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:

64:6 Mit 10:21; Hos 2:13; 8:1-12; Mal 2:7-8watu wangu wanaangamizwa

kwa kukosa maarifa,

“Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,

mimi nami nitakukataa wewe

usiwe kuhani kwangu mimi;

kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako

mimi nami sitawajali watoto wako.

74:7 Hab 2:16; Hos 9:11; 13:6Kadiri makuhani walivyoongezeka,

ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu,

walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.

84:8 Isa 56:11; Mik 3:11; Hos 14:1Hujilisha dhambi za watu wangu

na kupendezwa na uovu wao.

94:9 Isa 24:2; Yer 5:31; Hos 8:13; 10:10; 12:2Hata itakuwa: Kama walivyo watu,

ndivyo walivyo makuhani.

Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao

na kuwalipa kwa matendo yao.

104:10 Mik 6:14; Isa 55:2; Hos 7:14; 9:17; Eze 22:9; Law 26:26“Watakula lakini hawatashiba;

watajiingiza katika ukahaba

lakini hawataongezeka,

kwa sababu wamemwacha Bwana

na kujiingiza wenyewe

114:11 Isa 28:7; Hos 5:4; Mit 20:1; Law 10:9; 1Sam 25:36katika ukahaba,

divai ya zamani na divai mpya,

ambavyo huondoa ufahamu

124:12 Yer 2:27; Ufu 17:2; Hab 2:19; Isa 44:20; Hes 15:39; Za 73:27wa watu wangu.

Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti

nao hujibiwa na fimbo ya mti.

Roho ya ukahaba imewapotosha,

hawana uaminifu kwa Mungu wao.

134:13 Isa 1:28; Hos 2:13; 10:9; Yer 2:20; Amo 7:17; Rum 1:28Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima

na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima,

chini ya mialoni, milibua na miela,

ambako kuna vivuli vizuri.

Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba

na wake za wana wenu uzinzi.

144:14 Mwa 38:21; Hos 9:10; Mit 10:21“Sitawaadhibu binti zenu wakati

wanapogeukia ukahaba,

wala wake za wana wenu

wanapofanya uzinzi,

kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya

na kutambikia pamoja na makahaba

wa mahali pa kuabudia miungu:

watu wasiokuwa na ufahamu

wataangamia!

154:15 Hos 9:15; 12:11; Amo 4:4; Yos 7:2“Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli,

Yuda naye asije akawa na hatia.

“Usiende Gilgali,

usipande kwenda Beth-Aveni4:15 Beth-Aveni maana yake Nyumba ya Ubatili (au Uovu), jina lingine la Betheli kwa dhihaka.

Wala usiape,

‘Hakika kama Bwana aishivyo!’

164:16 Isa 5:17; 7:25; Kut 32:9; Yer 31:18Waisraeli ni wakaidi,

kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi.

Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga

kama wana-kondoo

katika shamba la majani?

174:17 Mt 15:14Efraimu amejiunga na sanamu,

ondokana naye!

184:18 Mik 3:11; 7:3Hata wakati wamemaliza vileo vyao

wanaendelea na ukahaba wao,

watawala wao hupenda sana

njia za aibu.

194:19 Hos 12:11; 13:15; Isa 1:29Kisulisuli kitawafagilia mbali

na dhabihu zao zitawaletea aibu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

何西阿書 4:1-19

耶和華指控以色列

1以色列人啊,

你們要留心聽耶和華的話。

祂指控住在這片土地上的居民,說:

「這片土地上的人不忠不信,

毫無良善,不認識上帝。

2他們咒詛、撒謊、兇殺、偷竊、通姦,

為所欲為,血案纍纍。

3所以,這片土地要哀鳴,

所有的居民都要消亡,

田間的野獸、空中的飛鳥、

水裡的魚類也要滅絕。」

4耶和華說:

「誰都不要指控別人,

誰都不要責備別人,

因為我要指控的是你們祭司。

5你們白天黑夜都要跌倒,

先知也要跟你們一起跌倒,

所以我要毀滅你們的母親以色列

6我的子民因不認識我而遭毀滅。

因為你們拒絕認識我,

我也要拒絕讓你們做我的祭司;

因為你們忘記我的律法,

我也要忘記你們的兒女。

7你們祭司越增多,

所犯的罪也越多,

所以我要使你們的尊榮變為羞恥。

8你們祭司藉我子民的贖罪祭自肥,

滿心希望他們犯罪。

9將來,我的子民如何,

你們祭司也如何。

我要照你們的所作所為懲罰你們、報應你們,

10使你們吃卻不得飽足,

行淫卻不得後代4·10 行淫卻不得後代」此處的意思是指責以色列人祭拜迦南人掌管生育的神明。他們以為這樣能帶來更多後代。

因為你們背棄耶和華,

11沉溺酒色,喪失心志。

12「我的子民祈求木頭,

隨從木杖的指引。

淫亂的心使他們走入歧途,

他們不忠不貞,背棄他們的上帝。

13他們在山頂和高崗上的橡樹、

楊樹和栗樹下獻祭燒香,

因為樹蔭怡人。

「所以,你們的女兒賣淫,

你們的兒媳通姦。

14但我不會因此而懲罰她們,

因為你們也與娼妓苟合,

與廟妓一起獻祭。

無知的民族必走向滅亡。

15「雖然以色列如同妓女,對我不忠,

但不要使猶大犯罪。

不要到吉甲去,

不要到伯·亞文4·15 伯·亞文」意思是「罪惡之家」,在此指伯特利。「伯特利」意思是「上帝之家」,但當時已變成祭拜偶像之地。去,

不要憑永活的耶和華起誓。

16以色列桀驁不馴,

如同桀驁不馴的母牛。

耶和華怎能牧養他們,

如同在草場上牧養羊羔呢?

17以法蓮4·17 以法蓮」為北國以色列最大的支派,聖經中有時用來代指北國以色列。本卷書中下同。與偶像為伍,

任由他吧!

18他們酒足興盡之後,

便不住地行淫;

他們的首領戀慕羞恥之事。

19風要把他們捲走,

他們必因所獻的祭而蒙羞。