Hosea 13 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 13:1-16

Hasira Ya Bwana Dhidi Ya Israeli

113:1 Mit 18:12; Amu 8:1; 12:1; Hos 11:2Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka,

alikuwa ametukuzwa katika Israeli.

Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali

naye akafa.

213:2 Isa 46:6; Yer 10:4; 44:8; Isa 44:17-20; Hos 8:4; 1Fal 19:18Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi;

wanajitengenezea sanamu

kutokana na fedha yao,

vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari,

vyote kazi ya fundi stadi.

Inasemekana kuhusu hawa watu,

“Hutoa dhabihu za binadamu

na kubusu sanamu za ndama.”

313:3 Hos 6:4; Ay 13:25; Dan 2:35; Za 68:213:3 Isa 17:13Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi,

kama umande wa alfajiri utowekao,

kama makapi yapeperushwayo

kutoka sakafu ya kupuria nafaka,

kama moshi utorokao kupitia dirishani.

413:4 Yer 2:6; Isa 43:10; 45:21-22; Hos 2:20; 12:9; Kut 20:3; Za 18:46“Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu,

niliyewaleta ninyi toka Misri.

Msimkubali Mungu mwingine ila mimi,

hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.

513:5 Kum 1:19; 2:7; 32:10; 8:15; 32:10Niliwatunza huko jangwani,

katika nchi yenye joto liunguzalo.

613:6 Mit 30:7-9; Yer 7:5; Eze 28:5; Kum 32:18; Isa 17:10; Hos 2:13; 4:7Nilipowalisha, walishiba,

waliposhiba, wakajivuna,

kisha wakanisahau mimi.

713:7 Ay 10:16; Yer 4:7; Mao 3:10Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba,

kama chui nitawavizia kando ya njia.

813:8 2Sam 17:8; Za 17:12; 50:22; Mao 3:10; Hos 2:12Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,

nitawashambulia na kurarua vifua vyenu.

Kama simba nitawala;

mnyama pori atawararua vipande vipande.

913:9 Yer 2:17-19; Kum 33:29“Ee Israeli, umeangamizwa,

kwa sababu wewe u kinyume nami,

kinyume na msaidizi wako.

1013:10 2Fal 17:4; 1Sam 8:6; Hos 7:7; 8:4Yuko wapi mfalme wako,

ili apate kukuokoa?

Wako wapi watawala wako katika miji yako yote

ambao ulisema kuwahusu,

‘Nipe mfalme na wakuu’?

1113:11 Yos 24:20; 1Sam 13:14; Hes 11:20; 1Fal 14:10; Hos 10:7Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme

na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.

1213:12 Kum 32:34; Ay 14:7Kosa la Efraimu limehifadhiwa,

dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.

1313:13 Isa 13:8; Mik 4:9-10; Isa 66:9; 2Fal 19:3Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia,

lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima;

wakati utakapowadia hatatoka

katika tumbo la mama yake.

1413:14 1The 4:14-17; Za 16:10; 49:15; Eze 37:12-13; 1Kor 15:54-55; Ufu 21:4“Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi,

nitawakomboa kutoka mautini.

Yako wapi, ee mauti, mateso yako?

Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako?

“Sitakuwa na huruma,

1513:15 Ay 1:19; Eze 19:12; Yer 20:5; 51:36; Hos 4:19hata ingawa Efraimu atastawi

miongoni mwa ndugu zake.

Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja,

ukivuma kutoka jangwani,

chemchemi yake haitatoa maji

na kisima chake kitakauka.

Ghala lake litatekwa

hazina zake zote.

1613:16 2Fal 8:12; 15:16; 17:5; Hos 7:14; 10:2, 14; Isa 13:16; Amo 1:13Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao,

kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao.

Wataanguka kwa upanga;

watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini,

wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”

Het Boek

Hosea 13:1-15

Gods boosheid over Israël

1Wanneer Israël vroeger sprak, beefden de volken van angst, want Israël was een dappere held. Maar de Israëlieten gingen Baäl aanbidden en hun vonnis was geveld. 2En ook nu nog blijven zij voortdurend zondigen. Zij gieten zilveren afgodsbeelden, gemaakt door kundige edelsmeden. ‘Offer hieraan!’ zeggen zij en zij kussen deze kalveren. 3Daarom zullen zij verdwijnen als de ochtendmist, als dauw die in alle vroegte verdampt, als kaf dat wordt weggeblazen door de wind, als rook die het raam uitvliegt.

4‘Ik alleen ben de Here, uw God, al vanaf de tijd waarin Ik u uit Egypte heb geleid. U hebt geen andere God dan Mij en er is geen andere verlosser. 5Ik heb voor u gezorgd in de dorre, droge woestijn. 6Maar toen u uw buik had volgegeten, werd u trots en vergat Mij. 7Daarom zal Ik Mij als een leeuw op u storten. Of Ik ga als een panter aan de kant van de weg op de loer liggen. 8Ik zal u aanvallen als een berin die van haar jongen is beroofd en u aan stukken scheuren en verslinden als een leeuw. 9O Israël, als Ik u vernietig, wie kan u dan nog redden? 10Waar is uw koning? Waarom roept u hem niet te hulp? Waar zijn alle leiders van het land? Vroeger riep u: “Geef ons een koning en regeringsleiders!” Waar zijn zij nu? 11In mijn woede gaf Ik u koningen en nam hen uit boosheid weer weg. 12Israëls zonden zijn geoogst en opgeslagen tot het moment van het vonnis. 13Hij mag opnieuw worden geboren, maar is als een kind dat liever in de moederschoot blijft. Wat dwaas en onverstandig! 14Zou Ik hem verlossen uit het dodenrijk of loskopen van de dood? Dood, waar zijn uw verschrikkingen? Dodenrijk, wat voor kwaad kunt u nog doen? Ik ken geen medelijden meer. 15Hij werd de vruchtbaarste onder zijn broeders genoemd, maar de oostenwind, de wind van de Here, zal hard over hem waaien en zijn land verwoesten. Zijn bronnen zullen opdrogen en de oases verdorren, hij zal sterven van dorst.’