Hosea 11 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 11:1-12

Upendo Wa Mungu Kwa Israeli

111:1 Kut 4:22; Mt 2:15; Yer 2:2; Eze 16:22; Hos 12:9; 13:4“Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda,

nilimwita mwanangu kutoka Misri.

211:2 Hos 2:13; 4:13; 2Fal 17:15; Isa 65:7; Yer 18:15Lakini kadiri nilivyomwita Israeli,

ndivyo walivyokwenda mbali nami.

Walitoa dhabihu kwa Mabaali

na kufukiza uvumba kwa vinyago.

311:3 Kum 1:31; 32:11; Kut 15:26; Yer 30:17Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea,

nikiwashika mikono;

lakini hawakutambua

kuwa ni mimi niliyewaponya.

411:4 Yer 31:2-3, 20; Law 26:13; Kut 16:32; Za 78:25Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu,

kwa vifungo vya upendo;

niliondoa nira shingoni mwao

nami nikainama kuwalisha.

511:5 Yer 8:4-6; Hos 7:16; 10:6; Kut 13:17“Je, hawatarudi Misri,

nayo Ashuru haitawatawala

kwa sababu wamekataa kutubu?

611:6 Hos 13:16; Mao 2:9Panga zitametameta katika miji yao,

zitaharibu makomeo ya malango yao

na kukomesha mipango yao.

711:7 Yer 3:6-7; 8:5; Isa 26:10Watu wangu wamedhamiria kuniacha.

Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana,

kwa vyovyote hatawainua.

811:8 Mwa 14:8; 19:25; Hos 6:4; Mao 3:32; Yer 7:29; Za 25:6; 1Fal 3:26“Efraimu, ninawezaje kukuacha?

Ee Israeli, ninawezaje kukutoa?

Nitawezaje kukutendea kama Adma?

Nitawezaje kukufanya kama Seboimu?

Moyo wangu umegeuka ndani yangu,

huruma zangu zote zimeamshwa.

911:9 Kum 13:17Sitatimiza hasira yangu kali,

wala sitageuka na kumharibu Efraimu.

Kwa kuwa mimi ndimi Mungu,

wala si mwanadamu,

Aliye Mtakatifu miongoni mwenu.

Sitakuja kwa ghadhabu.

1011:10 Hos 3:5; 6:1-3; Isa 31:4; 42:13; Za 18:45Watamfuata Bwana;

atanguruma kama simba.

Wakati angurumapo,

watoto wake watakuja wakitetemeka

kutoka magharibi.

1111:11 Isa 11:11; Mwa 8:8; Eze 28:26; 34:25-28Watakuja wakitetemeka

kama ndege wakitoka Misri,

kama hua wakitoka Ashuru.

Nitawakalisha katika nyumba zao,”

asema Bwana.

Dhambi Ya Israeli

1211:12 Hos 4:2; 10:13; Kum 7:9Efraimu amenizunguka kwa uongo,

nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.

Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu,

hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.

King James Version

Hosea 11:1-12

1When Israel was a child, then I loved him, and called my son out of Egypt. 2As they called them, so they went from them: they sacrificed unto Baalim, and burned incense to graven images. 3I taught Ephraim also to go, taking them by their arms; but they knew not that I healed them. 4I drew them with cords of a man, with bands of love: and I was to them as they that take off the yoke on their jaws, and I laid meat unto them.11.4 take off: Heb. lift up

5¶ He shall not return into the land of Egypt, but the Assyrian shall be his king, because they refused to return. 6And the sword shall abide on his cities, and shall consume his branches, and devour them, because of their own counsels. 7And my people are bent to backsliding from me: though they called them to the most High, none at all would exalt him.11.7 none…: Heb. together they exalted not

8How shall I give thee up, Ephraim? how shall I deliver thee, Israel? how shall I make thee as Admah? how shall I set thee as Zeboim? mine heart is turned within me, my repentings are kindled together. 9I will not execute the fierceness of mine anger, I will not return to destroy Ephraim: for I am God, and not man; the Holy One in the midst of thee: and I will not enter into the city. 10They shall walk after the LORD: he shall roar like a lion: when he shall roar, then the children shall tremble from the west. 11They shall tremble as a bird out of Egypt, and as a dove out of the land of Assyria: and I will place them in their houses, saith the LORD. 12Ephraim compasseth me about with lies, and the house of Israel with deceit: but Judah yet ruleth with God, and is faithful with the saints.11.12 saints: or, most holy