Hesabu 5 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 5:1-31

Utakaso Wa Kambi

1Bwana akamwambia Mose, 25:2 Law 13:2, 3; 15:2; 21:11; Mt 9:20; Hes 9:6-10; 12:14; Kum 23:10; 2Fal 5:27; 2Nya 26:20; Isa 52:11; Lk 17:12“Waamuru Waisraeli kumtoa nje ya kambi mtu yeyote ambaye ana ugonjwa wa ngozi uambukizao,5:2 Ugonjwa wa ngozi uambukizao hapa ina maana ya ukoma. au anayetokwa na majimaji ya aina yoyote, au ambaye ni najisi kwa utaratibu wa ibada kwa sababu ya maiti. 35:3 Kut 29:45; Law 26:12; 2Kor 6:16; Kut 25:8; Yos 22:19; Eze 37:26-28; Zek 2:10Hii itakuwa ni kwa wote, yaani, wanaume na wanawake; watoeni nje ya kambi ili wasije wakanajisi kambi yao, ambamo ninaishi miongoni mwao.” 4Waisraeli wakafanya hivyo; wakawatoa nje ya kambi. Wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amemwelekeza Mose.

Malipo Kwa Ajili Ya Makosa

5Bwana akamwambia Mose, 65:6 Law 6:2; 5:14–6:7“Waambie Waisraeli, ‘Wakati mwanaume au mwanamke akimkosea mwenzake kwa njia yoyote, na kwa hivyo akawa si mwaminifu kwa Bwana, mtu huyo ana hatia, 75:7 Law 5:5, 16; 6:5; Lk 19:8; Yos 7:19na ni lazima atubu dhambi aliyoifanya. Ni lazima atoe malipo kamili kwa ajili ya kosa lake, aongeze sehemu ya tano juu ya malipo hayo na kutoa yote kwa mtu aliyemkosea. 85:8 Law 5:15; 6:6-7Lakini ikiwa mtu huyo hana jamaa ya karibu ambaye malipo yanaweza kufanywa kwa ajili ya kosa, malipo yatakuwa mali ya Bwana, nayo ni lazima apewe kuhani, pamoja na kondoo dume ambaye anatumika kufanyia upatanisho kwa ajili yake. 95:9 Law 6:17; 7:6-14; Kut 29:28Matoleo yote matakatifu ya Waisraeli wanayoleta kwa kuhani yatakuwa yake. 105:10 Law 7:29-34; 10:13Kila kitu cha mtu kilichowekwa wakfu ni chake mwenyewe, lakini kile atoacho kwa kuhani kitakuwa cha kuhani.’ ”

Jaribio Kwa Ajili Ya Mke Asiye Mwaminifu

11Kisha Bwana akamwambia Mose, 125:12 Kut 20:14; Mit 2:16; 7:10-27; Hos 4:13“Nena na Waisraeli uwaambie: ‘Ikiwa mke wa mtu amepotoka na si mwaminifu kwa mumewe, 135:13 Kut 20:14; Law 18:20; 18:20; 20:10; Mit 30:20kwa kukutana kimwili na mwanaume mwingine, tendo hili likafichika kwa mumewe na unajisi wake usigundulike (kwa kuwa hakuna ushahidi dhidi yake, naye hakukamatwa katika tendo hilo), 145:14 Mit 6:34; 27:4; Wim 8:6; Isa 19:14nazo hisia za wivu zikamjia mumewe na kumshuku mkewe, naye mke yule ni najisi, au mumewe ana wivu na akamshuku ingawa si najisi, 155:15 Kut 16:36; Law 6:20; Eze 21:23; 29:16; Law 5:11; 1Fal 17:18basi atampeleka mkewe kwa kuhani. Huyo mume itampasa apeleke pia sadaka ya unga wa shayiri kiasi cha sehemu ya kumi ya efa5:15 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na kilo moja. kwa niaba ya mkewe. Huyo mwanaume kamwe asimimine mafuta juu ya huo unga wala asiweke uvumba juu yake, kwa sababu ni sadaka ya nafaka kwa ajili ya wivu, sadaka ya ukumbusho ili kukumbushia uovu.

165:16 Yer 17:10; 1Nya 28:9; Ebr 13:4“ ‘Kuhani atamleta huyo mwanamke na kumsimamisha mbele za Bwana. 17Kisha kuhani atachukua sehemu ya maji matakatifu ndani ya gudulia la udongo na kuchanganya na baadhi ya vumbi kutoka sakafu ya Maskani. 185:18 Law 10:6; 1Kor 11:6Baada ya kuhani kumsimamisha huyo mwanamke mbele za Bwana, atazifungua nywele za huyo mwanamke na kuweka sadaka ya ukumbusho mikononi mwake, ile sadaka ya nafaka kwa ajili ya wivu, huku kuhani mwenyewe akishikilia yale maji machungu yaletayo laana. 19Kisha kuhani atamwapiza huyo mwanamke, akimwambia, “Ikiwa hakuna mwanaume mwingine aliyekutana kimwili nawe, wala hujapotoka na kuwa najisi wakati ukiwa umeolewa na mumeo, maji haya machungu yaletayo laana na yasikudhuru. 20Lakini ikiwa umepotoka wakati ukiwa umeolewa na mume wako na umejinajisi mwenyewe kwa kukutana kimwili na mwanaume mwingine asiyekuwa mumeo”; 215:21 Yos 6:26; 1Sam 14:24; Neh 10:29; Mwa 9:25; Isa 65:15; Yer 29:22hapa kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya laana ya kiapo akisema: “Bwana na awafanye watu wako wakulaani na kukukataa, wakati Bwana atakapolifanya paja lako kupooza na tumbo lako kuvimba. 225:22 Za 109:18; Kum 27:15Maji haya yaletayo laana na yaingie ndani ya mwili wako ili tumbo lako livimbe na paja lako lipooze.”5:22 Paja lipooze hapa ina maana ya kuwa tasa au kuharibu mimba.

“ ‘Kisha mwanamke atasema, “Amen. Iwe hivyo.”

235:23 Yer 45:1“ ‘Kuhani ataandika laana hizi kwenye kitabu, kisha atazioshea laana hizo kwenye yale maji machungu. 24Kuhani atamnywesha yule mwanamke yale maji machungu yaletayo laana, nayo maji haya yatamwingia na kumsababishia maumivu makali. 255:25 Law 8:27; Kum 29:24Kuhani atachukua sadaka ya nafaka kwa ajili ya wivu kutoka mikononi mwa huyo mwanamke, naye ataipunga mbele za Bwana na kuileta madhabahuni. 26Kisha kuhani atachota sadaka ya nafaka mkono uliojaa kama sehemu ya kumbukumbu na kuiteketeza juu ya madhabahu, baada ya hayo, atamtaka huyo mwanamke anywe yale maji. 275:27 Isa 43:28; 65:15; Yer 26:6; 29:18; 42:18; 44:12, 22; Zek 8:13Kama amejitia unajisi na kukosa uaminifu kwa mumewe, wakati anapotakiwa anywe maji yale yaletayo laana, yatamwingia na kusababisha maumivu makali; tumbo lake litavimba na paja lake litapooza, naye atakuwa amelaaniwa miongoni mwa watu wake. 285:28 Ay 17:8-9; Za 47:5-6; Rum 5:3-5Hata hivyo, ikiwa huyo mwanamke hakujitia unajisi, naye ni safi, atasafishwa hatia na ataweza kuzaa watoto.

29“ ‘Basi, hii ndiyo sheria ya wivu mwanamke anapopotoka na kujitia unajisi akiwa ameolewa na mumewe, 30au hisia za wivu zinapomjia mwanaume kwa sababu ya kumshuku mkewe. Kuhani atamfanya huyo mwanamke kusimama mbele za Bwana na atatumia sheria hii yote kwa huyo mwanamke. 315:31 Law 5:1; 20:17; Eze 18:4; Rum 2:8-9Mume atakuwa hana hatia ya kosa lolote, bali mwanamke atayachukua matokeo ya dhambi yake.’ ”

Swedish Contemporary Bible

4 Moseboken 5:1-31

Bevara renheten i lägret

1Herren talade till Mose: 2”Befall Israels folk att de måste sända bort alla spetälska från lägret och alla som har flytningar och alla som har blivit orenade genom att röra vid en död människa. 3Detta gäller både män och kvinnor. Skicka iväg dem från lägret så att de inte orenar den plats där jag bor bland dem.” 4Israeliterna gjorde så; de förde dem utanför lägret. Så som Herren hade talat till Mose, så gjorde de.

Ersättning av skuld

5Sedan talade Herren till Mose: 6”Tala om för Israels folk att när någon syndar på något sätt vare sig det är en man eller en kvinna och därmed också sviker Herren, så står den människan i skuld. 7Hon måste bekänna sin synd, ersätta det orätta fullt ut och därtill tjugo procent och ge det sedan till den som han gjort orätt mot. 8Men om det inte finns någon återlösare som gottgörelsen kan ges till, ska den ges till Herren, lämnas till prästen tillsammans med en bagge som försoning. 9Alla heliga gåvor som Israels folk överlämnar till prästen tillfaller denne. 10Alla deras heliga gåvor tillhör prästen, allt de ger honom.”

Att bevisa otrohet

11Herren talade till Mose:

12”Säg till israeliterna att om en man har en hustru som bedrar honom och är otrogen med en annan man 13och har samlag med någon utan att hennes man får veta det och utan att hennes orenhet avslöjas därför att det inte finns några vittnen och hon inte tagits på bar gärning 14och om mannen blir svartsjuk och misstänker sin hustru fastän hon inte orenat sig, 15ska han gå till prästen med sin hustru. Han ska ha med ett offer för henne, tre och en halv liter kornmjöl utan olja och rökelse. Detta misstankeoffer, ett påminnelseoffer, visar skulden.

16Prästen ska föra fram henne inför Herren, 17ta heligt vatten i en lerkruka och blanda detta med jord från golvet i boningen. 18Han ska, efter att ha ställt kvinnan inför Herren, lösa upp hennes hår, placera misstankeoffret, påminnelseoffret, i hennes händer medan han själv håller krukan med det bittra vattnet som ger förbannelse. 19Prästen ska sedan ta ed av henne och säga till henne: ’Om ingen man, förutom din äkta man, har legat med dig, och om du inte bedragit din man som du tillhör och inte orenat dig, ska inte detta bittra vatten som annars orsakar förbannelse skada dig.’ 20Men om du har bedragit din äkta man och orenat dig genom att ligga med någon annan än din man 21– då ska prästen läsa förbannelsen över kvinnan och säga till henne: ’Må Herren då göra dig till en förbannelse och besvärjelse bland ditt folk. Må Herren låta ditt moderliv vissna och din buk svälla upp5:21 Det hebreiska ordets innebörd är osäker.. 22Må detta förbannelsevatten komma in i dig så att ditt underliv vissnar bort och din kropp sväller.’ Kvinnan ska då säga: ’Ja, låt det bli så.’

23Sedan ska prästen skriva ner förbannelsen på ett ark och tvätta av den i det bittra vattnet. 24Prästen ska sedan ge kvinnan att dricka av det bittra vattnet som för med sig förbannelse. Det ska komma in i henne med bitter verkan.

25Sedan ska prästen ta misstankeoffret från kvinnans hand, lyfta upp det inför Herren och bära det till altaret. 26Han ska ta en handfull av det som ett påminnelseoffer och bränna det på altaret och därefter låta kvinnan dricka vattnet. 27När han låtit henne dricka vattnet sker följande: Om hon har orenat sig genom äktenskapsbrott mot sin man kommer vattnet att bli bittert i henne. Hennes kropp kommer att svälla upp och hennes underliv att vissna och hon ska bli en förbannelse bland sitt folk. 28Men om hon är ren och inte har begått äktenskapsbrott, kommer hon inte att lida någon skada och kommer att kunna fortsätta att föda barn.

29Detta är lagen om misstänksamhet när en gift kvinna är otrogen och orenar sig 30eller när en man drabbas av svartsjuka och misstänker sin hustru. Han ska då ställa fram sin hustru inför Herren. Prästen ska handla efter vad som föreskrivs i denna lag. 31Hennes make går fri, men om hustrun är skyldig, får hon stå för följderna av sin synd.”