Hesabu 4 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 4:1-49

Wakohathi

1Bwana akawaambia Mose na Aroni, 24:2 Kut 30:12“Wahesabu Wakohathi walio sehemu ya Walawi kwa koo zao na jamaa zao. 34:3 Hes 1:46; 8:25; 1Nya 23:3, 24-27; Mwa 41:46; Ezr 3:8; Lk 3:23Wahesabu wanaume wote wenye umri wa miaka thelathini hadi hamsini wanaokuja kutumika katika kazi ya Hema la Kukutania.

44:4 Hes 3:28; 7:9“Hii ndiyo kazi ya Wakohathi katika Hema la Kukutania: Watatunza vitu vilivyo vitakatifu sana. 54:5 Kut 25:10, 16; 26:31-33; 1Nya 23:26; Law 16:2; 2Nya 3:14; Mt 27:51Wakati kambi inapohamishwa, Aroni na wanawe wataingia ndani na kushusha lile pazia la kuzuilia na kufunika nalo Sanduku la Ushuhuda. 64:6 Kut 25:5, 13-15; 1Fal 8:7; 2Nya 5:8Kisha watafunika juu yake na ngozi za pomboo,4:6 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. na kutandaza juu yake kitambaa cha rangi ya buluu iliyokolea na kuingiza mipiko mahali pake.

74:7 Law 24:6; Kut 25:30; 39:36; Yer 52:19“Juu ya meza ya mikate ya Wonyesho watatandaza kitambaa cha buluu na waweke sahani juu yake, masinia, bakuli na magudulia kwa ajili ya sadaka za kinywaji; mkate ule ambao upo hapa daima utabaki juu yake. 84:8 Kut 26:26-28Juu ya hivyo vitu watatandaza kitambaa chekundu na kufunika kwa ngozi za pomboo na kuweka mipiko yake mahali pake.

94:9 Kut 25:38“Watachukua kitambaa cha buluu na kufunika kinara cha taa kilicho kwa ajili ya nuru, pamoja na taa zake, mikasi yake, sinia zake, magudulia yake yote yaliyotumika kuwekea mafuta. 10Kisha watakisokotea pamoja na vifaa vyake vyote katika ngozi za pomboo na kukiweka kwenye jukwaa lake.

114:11 Kut 30:1-4“Juu ya madhabahu ya dhahabu watatandaza kitambaa cha buluu na kukifunika kwa ngozi za pomboo na kuweka mipiko yake mahali pake.

124:12 Hes 3:31“Watavichukua vyombo vyote vinavyotumika kuhudumia mahali patakatifu, watavisokotea kwenye kitambaa cha buluu na kufunika kwa ngozi za pomboo, na kuviweka juu ya miti ya kuchukulia.

134:13 Law 1:16; Kut 27:1-8; Hes 3:31“Wataondoa majivu kutoka madhabahu ya shaba na kutandaza kitambaa cha zambarau juu yake. 144:14 Kut 31:9; 27:3, 6; 1Nya 28:17; 2Nya 4:8, 11-16; Hes 7:84; Yer 52:6Kisha wataweka vyombo vyote juu yake vinavyotumika kwa kuhudumia madhabahuni pamoja na vyombo vya kutolea moto, nyuma, miiko na mabakuli ya kunyunyizia. Juu yake watatandaza ngozi za pomboo ya kufunika, na kuweka mipiko mahali pake.

154:15 Hes 3:27; 7:9; Kut 28:43; Hes 1:51; 2Sam 6:6, 7; Kum 31:9; 2Sam 6:6-7, 13; 1Nya 28:12-13“Baada ya Aroni na wanawe kumaliza kazi ya kufunika samani takatifu na vyombo vyake vyote, watu watakapokuwa tayari kungʼoa kambi, Wakohathi watakuja kufanya kazi ya kubeba. Lakini wasije wakagusa vitu vitakatifu la sivyo watakufa. Wakohathi ndio watakaobeba vile vitu vilivyomo katika Hema la Kukutania.

164:16 Law 6:14-23; 10:6; Hes 3:32; Kut 25:6; 29:41“Eleazari mwana wa Aroni, kuhani, ndiye atakayesimamia mafuta kwa ajili ya taa, uvumba wenye harufu nzuri, sadaka za kila siku za nafaka na mafuta ya upako. Ndiye atakayekuwa msimamizi wa maskani yote ya Bwana na kila kitu kilichomo ndani mwake pamoja na samani takatifu na vyombo vyake.”

17Bwana akawaambia Mose na Aroni, 18“Hakikisheni kwamba koo za kabila la Wakohathi hawatengwi kutoka Walawi. 194:19 Hes 3:32Ili wapate kuishi wala wasife wanapokaribia vitu vitakatifu sana, uwafanyie hivi: Aroni na wanawe watakwenda mahali patakatifu na kumgawia kila mtu kazi yake, na kwamba ni nini atakachochukua. 204:20 Kut 19:21; 1Sam 6:19Lakini Wakohathi hawaruhusiwi kuingia ndani ili kuangalia vitu vitakatifu, hata kwa kitambo kidogo, la sivyo watakufa.”

Wagershoni

21Bwana akamwambia Mose, 22“Wahesabu pia Wagershoni kwa jamaa zao na koo zao. 234:23 Hes 4:3; 1Nya 23:3; 24:27Wahesabu wanaume wote wenye umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao huja kutumika katika Hema la Kukutania.

24“Hii ndiyo huduma ya koo za Wagershoni wakati wanapofanya kazi na kubeba mizigo. 254:25 Kut 26:14; 27:10-18; Hes 3:25Watabeba mapazia ya maskani. Hema la Kukutania, kifuniko chake na kifuniko cha nje cha ngozi za pomboo, mapazia ya maingilio ya Hema la Kukutania, 264:26 Kut 27:9, 16; Hes 3:26mapazia ya ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pazia la maingilio, kamba na vifaa vyote vinavyotumika katika huduma yake. Wagershoni watafanya yote yatakiwayo kufanyika na vitu hivi. 27Utumishi wao wote ukiwa ni kuchukua au wa kufanya kazi nyingine, utafanyika chini ya maelekezo ya Aroni na wanawe. Mtawapangia kama wajibu wao yote watakayoyafanya. 284:28 Hes 7:7; Kut 6:23Hii ndiyo huduma ya koo za Wagershoni katika Hema la Kukutania. Wajibu wao utakuwa chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani Aroni.

Wamerari

294:29 Kut 30:12; Mwa 46:11“Wahesabu Wamerari kwa koo zao na jamaa zao. 30Wahesabu wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao watakuja kutumika katika Hema la Kukutania. 314:31 Hes 3:36; Kut 26:15; 27:9-19Huu ndio wajibu wao wanapofanya huduma katika Hema la Kukutania: kubeba miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo na vitako, 324:32 Hes 3:37; Kut 25:9; 1Nya 9:29; Ezr 8:24-30nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema, kamba, vifaa vyake vyote na kila kitu kinachohusiana na matumizi yake. Kila mtu mpangie vitu maalum vya kubeba. 334:33 Kut 28:21Huu ndio utumishi wa koo za Merari kama watakavyofanya kazi katika Hema la Kukutania, chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani, Aroni.”

Kuhesabiwa Kwa Koo Za Walawi

344:34 Hes 4:35-40; 1Kor 12:8-12; Kum 33:25Mose, Aroni na viongozi wa jumuiya wakawahesabu Wakohathi kwa koo zao na jamaa zao. 35Wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 36waliohesabiwa kwa koo zao, walikuwa 2,750. 374:37 Hes 3:27Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wote wale wa koo za Wakohathi ambao walitumika katika Hema la Kukutania. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatana na amri ya Bwana kupitia kwa Mose.

384:38 Mwa 46:11Wagershoni walihesabiwa kwa koo zao na jamaa zao. 39Watu wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 40waliohesabiwa kwa koo zao na jamaa zao, walikuwa 2,630. 41Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wale wa koo za Gershoni ambao walitumika katika Hema la Kukutania. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatana na amri ya Bwana.

42Wamerari walihesabiwa kwa koo zao na jamaa zao. 43Wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 44waliohesabiwa kwa koo zao, walikuwa 3,200. 45Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wale wa koo za Wamerari. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatia amri ya Bwana kupitia kwa Mose.

46Hivyo Mose, Aroni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kwa koo zao na jamaa zao. 474:47 Rum 12:6-8Wanaume wote wenye umri kuanzia miaka thelathini hadi hamsini waliokuja kufanya kazi ya kuhudumu na kubeba Hema la Kukutania 484:48 Hes 3:39walikuwa watu 8,580. 494:49 Hes 1:47; Rum 12:6-8Kwa amri ya Bwana kupitia Mose, kila mmoja aligawiwa kazi yake na kuambiwa kitu cha kubeba.

Hivyo ndivyo walivyohesabiwa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

O Livro

Números 4:1-49

Os coatitas

1Então o Senhor disse a Moisés e a Aarão: 2“Tomem a soma do grupo familiar de Coate, da tribo de Levi. 3Serão contados todos os do sexo masculino, entre 30 e 50 anos, capazes de trabalharem na tenda do encontro.

4Estes são os seus deveres quanto às coisas santas: 5Quando o acampamento for chamado a deslocar-se, Aarão e os filhos entrarão primeiramente na tenda do encontro e descerão o véu, cobrindo a arca do testemunho com ele. 6Seguidamente, cobrirão o próprio véu com a coberta de peles de couro fino4.6 Acerca deste tipo de pele, o termo hebraico tem significado incerto. Pode significar couro à base de pele de um animal mamífero marinho, provavelmente o dugongo, ou significar um tipo fino e duradouro de couro à base de animais que foram domesticados. e, sobre esta, um pano azul. Porão ainda as varas na arca.

7Depois deverão estender igualmente um pano azul sobre a mesa, na qual está exposto o pão da Presença, e colocarão os pratos, as colheres, as taças, os jarros, e também o pão sobre esse tecido. Porão em cima disso tudo um pano carmesim; 8e finalmente uma coberta pele de couro fino. Então enfiarão as varas de transporte nos lados da mesa.

9Depois disso, cobrirão o candelabro com um pano azul, assim como as lâmpadas, os apagadores, os espevitadores e o reservatório de azeite. 10Todo este conjunto de objetos será depois coberto com peles de couro fino, feito o seu acondicionamento, será colocado sobre uma armação, para ser transportado.

11Deverão depois estender um pano azul sobre o altar de ouro, cobri-lo com uma pele de couro fino, e pôr as varas nos seus cantos.

12Todos os outros utensílios do tabernáculo deverão ser acondicionados num tecido azul, cobertos com pele de couro fino, e postos numa armação de transporte.

13Hão de ser tiradas as cinzas do altar e este será coberto com um pano de púrpura. 14Todos os utensílios do altar devem ficar sobre ele; braseiros, garfos, pás, bacias e outros recipientes, e uma coberta de peles de couro fino, estendida sobre eles. Finalmente, as varas de transporte serão enfiadas lateralmente, nos seus lugares.

15Quando Aarão e os seus filhos tiverem terminado esta tarefa, os homens de Coate chegar-se-ão e carregarão os embrulhos, levando-os para onde o acampamento se deslocar. Mas não deverão tocar nos objetos sagrados, senão morrerão. Esta é portanto a sagrada tarefa dos descendentes de Coate na tenda do encontro.

16Eleazar, filho de Aarão, terá a responsabilidade do azeite para a iluminação, do incenso aromático, da oferta diária de cereais, do azeite da unção; na realidade, terá até a supervisão de todo o tabernáculo; tudo ali estará à sua responsabilidade.”

17Então o Senhor disse a Moisés e a Aarão: 18“Atenção que as famílias dos coatitas não se destruam a si mesmas! 19Para que eles não morram quando transportam as coisas santas, farás o seguinte: Aarão e os seus filhos entrarão e indicarão a cada um o que deve transportar. 20No entanto, eles nunca deverão entrar no santuário, nem sequer por um momento, nem olhar para os objetos sagrados; senão morrerão.”

Os gersonitas

21Disse mais o Senhor a Moisés: 22“Toma o número dos gersonitas da tribo de Levi 23todos os homens entre 30 e 50 anos, capazes para o trabalho sagrado com a tenda do encontro. 24Serão estas as suas funções: 25levarão as cortinas do tabernáculo, mais propriamente o conjunto da tenda do encontro, com as cobertas, as peles de couro fino, a cortina da porta; 26e ainda as cortinas do pátio e as da entrada deste; também deverão transportar as suas cordas e todos os acessórios respetivos. 27São plenamente responsáveis por tudo isto que foi referido. Aarão ou os seus filhos deverão indicar-lhes as tarefas; 28mas os gersonitas serão diretamente responsáveis perante Itamar, sacerdote, filho de Aarão.

Os meraritas

29Agora, conta os homens do grupo das famílias descendentes de Merari, da tribo de Levi, 30entre 30 e 50 anos, capazes para o serviço da tenda do encontro. 31Quando a tenda do encontro tiver de ser deslocada, deverão transportar toda a armação, as bases, 32as tábuas, assim como a estrutura envolvente do pátio, com as suas bases, estacas, cordas, e tudo o resto que esteja relacionado com isso e que sirva para a sua conservação. Distribui as tarefas por cada homem, notando o seu nome. 33A divisão de Merari será igualmente responsável perante Itamar, filho de Aarão.”

As divisões de levitas são contadas

34Moisés, Aarão e os outros chefes tomaram o número dos homens da divisão de Coate, 35dos que tinham entre 30 e 50 anos, capazes para o serviço da tenda do encontro; 36e acharam que havia um total de 2750. 37Tudo isto foi feito para dar cumprimento às instruções do Senhor a Moisés.

38-48Idêntica contagem foi feita à divisão de Gerson, totalizando 2630 indivíduos. Quanto à de Merari, contaram-se 3200.

Moisés, Aarão e os chefes de Israel acharam que todos os levitas entre 30 e 50 anos, aptos para o serviço da tenda do encontro e para o seu transporte, constituíam um total de 8580 pessoas. 49Este censo foi realizado em resposta às ordens do Senhor a Moisés, o qual indicou para cada um a sua função e o que devia transportar.