Hesabu 4 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 4:1-49

Wakohathi

1Bwana akawaambia Mose na Aroni, 24:2 Kut 30:12“Wahesabu Wakohathi walio sehemu ya Walawi kwa koo zao na jamaa zao. 34:3 Hes 1:46; 8:25; 1Nya 23:3, 24-27; Mwa 41:46; Ezr 3:8; Lk 3:23Wahesabu wanaume wote wenye umri wa miaka thelathini hadi hamsini wanaokuja kutumika katika kazi ya Hema la Kukutania.

44:4 Hes 3:28; 7:9“Hii ndiyo kazi ya Wakohathi katika Hema la Kukutania: Watatunza vitu vilivyo vitakatifu sana. 54:5 Kut 25:10, 16; 26:31-33; 1Nya 23:26; Law 16:2; 2Nya 3:14; Mt 27:51Wakati kambi inapohamishwa, Aroni na wanawe wataingia ndani na kushusha lile pazia la kuzuilia na kufunika nalo Sanduku la Ushuhuda. 64:6 Kut 25:5, 13-15; 1Fal 8:7; 2Nya 5:8Kisha watafunika juu yake na ngozi za pomboo,4:6 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. na kutandaza juu yake kitambaa cha rangi ya buluu iliyokolea na kuingiza mipiko mahali pake.

74:7 Law 24:6; Kut 25:30; 39:36; Yer 52:19“Juu ya meza ya mikate ya Wonyesho watatandaza kitambaa cha buluu na waweke sahani juu yake, masinia, bakuli na magudulia kwa ajili ya sadaka za kinywaji; mkate ule ambao upo hapa daima utabaki juu yake. 84:8 Kut 26:26-28Juu ya hivyo vitu watatandaza kitambaa chekundu na kufunika kwa ngozi za pomboo na kuweka mipiko yake mahali pake.

94:9 Kut 25:38“Watachukua kitambaa cha buluu na kufunika kinara cha taa kilicho kwa ajili ya nuru, pamoja na taa zake, mikasi yake, sinia zake, magudulia yake yote yaliyotumika kuwekea mafuta. 10Kisha watakisokotea pamoja na vifaa vyake vyote katika ngozi za pomboo na kukiweka kwenye jukwaa lake.

114:11 Kut 30:1-4“Juu ya madhabahu ya dhahabu watatandaza kitambaa cha buluu na kukifunika kwa ngozi za pomboo na kuweka mipiko yake mahali pake.

124:12 Hes 3:31“Watavichukua vyombo vyote vinavyotumika kuhudumia mahali patakatifu, watavisokotea kwenye kitambaa cha buluu na kufunika kwa ngozi za pomboo, na kuviweka juu ya miti ya kuchukulia.

134:13 Law 1:16; Kut 27:1-8; Hes 3:31“Wataondoa majivu kutoka madhabahu ya shaba na kutandaza kitambaa cha zambarau juu yake. 144:14 Kut 31:9; 27:3, 6; 1Nya 28:17; 2Nya 4:8, 11-16; Hes 7:84; Yer 52:6Kisha wataweka vyombo vyote juu yake vinavyotumika kwa kuhudumia madhabahuni pamoja na vyombo vya kutolea moto, nyuma, miiko na mabakuli ya kunyunyizia. Juu yake watatandaza ngozi za pomboo ya kufunika, na kuweka mipiko mahali pake.

154:15 Hes 3:27; 7:9; Kut 28:43; Hes 1:51; 2Sam 6:6, 7; Kum 31:9; 2Sam 6:6-7, 13; 1Nya 28:12-13“Baada ya Aroni na wanawe kumaliza kazi ya kufunika samani takatifu na vyombo vyake vyote, watu watakapokuwa tayari kungʼoa kambi, Wakohathi watakuja kufanya kazi ya kubeba. Lakini wasije wakagusa vitu vitakatifu la sivyo watakufa. Wakohathi ndio watakaobeba vile vitu vilivyomo katika Hema la Kukutania.

164:16 Law 6:14-23; 10:6; Hes 3:32; Kut 25:6; 29:41“Eleazari mwana wa Aroni, kuhani, ndiye atakayesimamia mafuta kwa ajili ya taa, uvumba wenye harufu nzuri, sadaka za kila siku za nafaka na mafuta ya upako. Ndiye atakayekuwa msimamizi wa maskani yote ya Bwana na kila kitu kilichomo ndani mwake pamoja na samani takatifu na vyombo vyake.”

17Bwana akawaambia Mose na Aroni, 18“Hakikisheni kwamba koo za kabila la Wakohathi hawatengwi kutoka Walawi. 194:19 Hes 3:32Ili wapate kuishi wala wasife wanapokaribia vitu vitakatifu sana, uwafanyie hivi: Aroni na wanawe watakwenda mahali patakatifu na kumgawia kila mtu kazi yake, na kwamba ni nini atakachochukua. 204:20 Kut 19:21; 1Sam 6:19Lakini Wakohathi hawaruhusiwi kuingia ndani ili kuangalia vitu vitakatifu, hata kwa kitambo kidogo, la sivyo watakufa.”

Wagershoni

21Bwana akamwambia Mose, 22“Wahesabu pia Wagershoni kwa jamaa zao na koo zao. 234:23 Hes 4:3; 1Nya 23:3; 24:27Wahesabu wanaume wote wenye umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao huja kutumika katika Hema la Kukutania.

24“Hii ndiyo huduma ya koo za Wagershoni wakati wanapofanya kazi na kubeba mizigo. 254:25 Kut 26:14; 27:10-18; Hes 3:25Watabeba mapazia ya maskani. Hema la Kukutania, kifuniko chake na kifuniko cha nje cha ngozi za pomboo, mapazia ya maingilio ya Hema la Kukutania, 264:26 Kut 27:9, 16; Hes 3:26mapazia ya ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pazia la maingilio, kamba na vifaa vyote vinavyotumika katika huduma yake. Wagershoni watafanya yote yatakiwayo kufanyika na vitu hivi. 27Utumishi wao wote ukiwa ni kuchukua au wa kufanya kazi nyingine, utafanyika chini ya maelekezo ya Aroni na wanawe. Mtawapangia kama wajibu wao yote watakayoyafanya. 284:28 Hes 7:7; Kut 6:23Hii ndiyo huduma ya koo za Wagershoni katika Hema la Kukutania. Wajibu wao utakuwa chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani Aroni.

Wamerari

294:29 Kut 30:12; Mwa 46:11“Wahesabu Wamerari kwa koo zao na jamaa zao. 30Wahesabu wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao watakuja kutumika katika Hema la Kukutania. 314:31 Hes 3:36; Kut 26:15; 27:9-19Huu ndio wajibu wao wanapofanya huduma katika Hema la Kukutania: kubeba miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo na vitako, 324:32 Hes 3:37; Kut 25:9; 1Nya 9:29; Ezr 8:24-30nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema, kamba, vifaa vyake vyote na kila kitu kinachohusiana na matumizi yake. Kila mtu mpangie vitu maalum vya kubeba. 334:33 Kut 28:21Huu ndio utumishi wa koo za Merari kama watakavyofanya kazi katika Hema la Kukutania, chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani, Aroni.”

Kuhesabiwa Kwa Koo Za Walawi

344:34 Hes 4:35-40; 1Kor 12:8-12; Kum 33:25Mose, Aroni na viongozi wa jumuiya wakawahesabu Wakohathi kwa koo zao na jamaa zao. 35Wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 36waliohesabiwa kwa koo zao, walikuwa 2,750. 374:37 Hes 3:27Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wote wale wa koo za Wakohathi ambao walitumika katika Hema la Kukutania. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatana na amri ya Bwana kupitia kwa Mose.

384:38 Mwa 46:11Wagershoni walihesabiwa kwa koo zao na jamaa zao. 39Watu wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 40waliohesabiwa kwa koo zao na jamaa zao, walikuwa 2,630. 41Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wale wa koo za Gershoni ambao walitumika katika Hema la Kukutania. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatana na amri ya Bwana.

42Wamerari walihesabiwa kwa koo zao na jamaa zao. 43Wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 44waliohesabiwa kwa koo zao, walikuwa 3,200. 45Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wale wa koo za Wamerari. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatia amri ya Bwana kupitia kwa Mose.

46Hivyo Mose, Aroni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kwa koo zao na jamaa zao. 474:47 Rum 12:6-8Wanaume wote wenye umri kuanzia miaka thelathini hadi hamsini waliokuja kufanya kazi ya kuhudumu na kubeba Hema la Kukutania 484:48 Hes 3:39walikuwa watu 8,580. 494:49 Hes 1:47; Rum 12:6-8Kwa amri ya Bwana kupitia Mose, kila mmoja aligawiwa kazi yake na kuambiwa kitu cha kubeba.

Hivyo ndivyo walivyohesabiwa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

Bibelen på hverdagsdansk

4. Mosebog 4:1-49

Levitternes arbejde med åbenbaringsteltet

1Da sagde Herren til Moses og Aron: 2-3„Optæl hvor mange mandlige efterkommere af Levis søn Kehat, der er mellem 30 og 50 år. Det er dem, der skal arbejde i åbenbaringsteltet 4med de helligste ting:

5Hver gang I er klar til at pakke lejren sammen, skal Aron og hans sønner først gå ind i helligdommen og tage forhænget mellem det hellige og det allerhelligste rum ned og lægge det over pagtens ark. 6Oven på det skal de lægge et kraftigt stykke læder, som igen skal dækkes med purpurfarvet klæde, før de anbringer bærestængerne i guldringene.

7Dernæst skal de brede et purpurfarvet klæde ud over bordet med de hellige brød og anbringe de forskellige fade, skåle og kander, der bruges ved drikofrene, oven på klædet sammen med de brød, der altid ligger fremme. 8Ovenpå igen skal de brede et skarlagenrødt klæde og et kraftigt stykke læder, før de anbringer bærestængerne i bordets guldringe.

9Lysestagen, lamperne, vægesaksene, vægebakkerne og beholderne til olivenolie skal anbringes på bærestativet, hvorefter de dækkes med et purpurfarvet klæde 10og derefter med et stykke kraftigt læder.

11Så skal de brede et purpurfarvet klæde over røgelsesalteret af guld, dække det med et kraftigt stykke læder og anbringe bærestængerne i alterets guldringe. 12Alle de øvrige redskaber, der bruges i helligdommen, skal dækkes med purpurfarvet klæde og kraftigt læder, før de anbringes på bærestativet.

13Brændofferalteret skal også dækkes til med et purpurfarvet klæde, men først skal asken fjernes. 14Alle redskaber, der bruges ved ofringen, skal lægges oven på klædet—både bakker til gløder, kødgafler, skovle og skåle—hvorefter det hele skal dækkes til med kraftigt læder. Til sidst skal bærestængerne anbringes i ringene.

15Når Aron og hans sønner har pakket helligdommens inventar og redskaber sammen, skal kehatitterne træde til og bære det hele til næste lejrplads. Men hvis de rører disse hellige ting, skal de dø. Det er altså kehatitternes opgave at bære helligdommens inventar.

16Arons søn Eleazar er ansvarlig for lampeolien, den hellige røgelse, det daglige afgrødeoffer og salveolien—ja, han skal have overopsynet med åbenbaringsteltet og alt dets inventar og de hellige redskaber.”

17Dernæst sagde Herren til Moses og Aron: 18„I må passe på, at kehatitterne ikke mister livet. 19I skal nøje overholde de forskrifter, jeg her har givet, så de ikke dør under udførelsen af deres opgave. Det er Aron og hans sønner, der skal fortælle kehatitterne, hvad de hver især skal bære. 20Men kehatitterne må først komme ind i helligdommen, efter at det hele er pakket ned, for hvis de ser de hellige ting, skal de dø.”

21Herren sagde nu til Moses: 22-23„Optæl hvor mange mandlige efterkommere af Levis søn Gershon, der er mellem 30 og 50 år. De skal også arbejde ved åbenbaringsteltet. 24-25Det er deres opgave at transportere boligens teltduge, de to tagdækninger af vædderskind og kraftigt læder samt indgangsforhænget. 26Derudover har de til opgave at transportere forgårdens teltvægge og forhænget over indgangen til forgården, som indhegner helligdommen og brændofferalteret. Endelig skal de også transportere diverse snore og værktøj, der bruges ved arbejdet. 27Aron og hans sønner skal uddelegere arbejdet blandt gershonitterne, 28og gershonitterne skal stå til regnskab for deres arbejde over for Arons søn Itamar.

29-30Optæl hvor mange mandlige efterkommere af Levis søn Merari, der er mellem 30 og 50 år. De skal også arbejde ved åbenbaringsteltet. 31Efter at teltet er pakket sammen, er det deres opgave at afmontere og transportere helligdommens vægmoduler, tværstænger, stolper og sokler, 32forgårdens stolper og sokler, samt alle pløkker og barduner—og alt det værktøj, der bruges under arbejdet. Enhver skal være helt klar over, hvori deres opgave består, 33så arbejdet kan gå hurtigt; og Arons søn Itamar skal have overopsynet med det.”

34-37På Herrens befaling foretog Moses og Aron og folkets ledere så en optælling af levitterne. Først lavede de en liste over Kehats slægt, familie for familie, over alle mænd, der var mellem 30 og 50 år, og som havde pligt til at arbejde ved åbenbaringsteltet. Det samlede antal var 2750. 38-41En tilsvarende optælling over Gershons slægt blev til 2630, 42-45og over Meraris slægt 3200. 46-48Det samlede antal mænd mellem 30 og 50 år, der havde pligt til at arbejde ved åbenbaringsteltet, var 8580. 49Aron mønstrede alle disse mænd og forklarede dem deres opgaver, sådan som Herren havde befalet gennem Moses.