Hesabu 36 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 36:1-13

Urithi Wa Binti Za Selofehadi

136:1 Hes 26:30; Mwa 50:23; Hes 26:28; 27:2Viongozi wa jamaa ya ukoo wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase, waliokuwa wametoka katika koo za wazao wa Yosefu, walikuja na kuzungumza mbele ya Mose na viongozi, wakuu wa jamaa ya Waisraeli. 236:2 Hes 33:54; 26:33; Yos 17:3-4Wakasema, “Bwana alipomwamuru bwana wangu kuwapa Waisraeli nchi kama urithi kwa kura, alikuamuru kutoa urithi wa ndugu yetu Selofehadi kwa binti zake. 3Sasa ikiwa wataolewa na watu wa makabila mengine ya Kiisraeli, itakuwa kwamba urithi wao utaondolewa kutoka urithi wa mababu zetu na kuongezwa katika urithi wa kabila ambalo dada hao wameolewa. Kwa hiyo sehemu ya urithi tuliyogawiwa itachukuliwa kutoka kwetu. 436:4 Law 25:10Wakati mwaka wa Yubile kwa Waisraeli utafika, urithi wao utaongezwa kwa lile kabila ambalo wameolewa, na mali yao itaondolewa kutoka urithi wa kabila la mababu zetu.”

536:5 Hes 27:7Ndipo kwa agizo la Bwana Mose akatoa amri ifuatayo kwa Waisraeli: “Kile wazao wa kabila la Yosefu wanachosema ni kweli. 6Hivi ndivyo Bwana anavyoamuru kwa binti za Selofehadi: Wanaweza kuolewa na mtu yeyote wampendaye, mradi tu waolewe miongoni mwa koo za kabila za baba yao. 736:7 Law 25:23; 1Fal 21:3Hakuna urithi katika Israeli utakaohamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila jingine, kwa kuwa kila Mwisraeli atatunza ardhi ya kabila lake aliyoirithi kutoka kwa baba zake. 836:8 1Nya 23:22Kila binti atakayerithi ardhi katika kabila lolote la Israeli ni lazima aolewe na mtu kutoka kabila na ukoo wa baba yake, ili kila Mwisraeli amiliki urithi wa baba zake. 9Hakuna urithi uwezao kuhamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila jingine, kwa kuwa kila kabila la Israeli litatunza nchi linayorithi.”

10Kwa hiyo binti za Selofehadi wakafanya kama Bwana alivyomwamuru Mose. 1136:11 Hes 27:1Binti za Selofehadi, ambao ni Mahla, Tirsa, Hogla, Milka na Noa, wakaolewa na waume, wana wa ndugu za baba yao. 1236:12 1Nya 7:15Waliolewa ndani ya koo za wazao wa Manase mwana wa Yosefu, na urithi wao ukabaki katika ukoo na kabila la baba yao.

1336:13 Law 7:38; 27:34; Hes 22:1; 26:3; 31:12; Kum 33:4; Neh 9:12-14; Yn 1:17; 7:19Haya ndiyo maagizo na masharti ambayo Bwana aliwapa Waisraeli kupitia Mose katika tambarare za Moabu, karibu na Yordani ngʼambo ya Yeriko.

Bibelen på hverdagsdansk

4. Mosebog 36:1-13

Lov angående kvinders arveret

1Familieoverhovederne i Gileads slægt kom nu til Moses og folkets ledere med et problem. De sagde: 2„Herren har befalet dig at lade Israels folk fordele landet ved lodtrækning, og du har givet os besked på at overdrage vores slægtning Zelofhads jord til hans døtre. 3Men hvis de nu gifter sig med mænd fra en anden stamme, vil deres jordstykke tilfalde den stamme, og vores område vil i så fald blive formindsket, 4uden at vi kan gøre os håb om at få den mistede jord tilbage i det førstkommende jubelår.”

5Derfor bekendtgjorde Moses på Herrens befaling følgende ordning for kvinders arvelod: „Disse mænd fra Manasses stamme har ret. 6Derfor siger Herren, at Zelofhads døtre kun må gifte sig inden for deres egen stamme. 7Derved undgår vi, at deres jordstykke kommer på andre stammers hænder, hvilket ville være forkert, for der må ikke overdrages jord fra en stamme til en anden. 8-9Enhver arveberettiget kvinde skal derfor gifte sig inden for sin egen stamme, så hendes arvelod forbliver på stammens hænder.”

10-12Zelofhads døtre, som hed Mala, Tirtza, Hogla, Milka og Noa, gjorde, som Herren havde befalet Moses. De giftede sig med mænd fra deres egen stamme, Manasses stamme. På den måde forblev deres jord på stammens hænder.

13Alle disse bud og forskrifter gav Herren til Israels folk gennem Moses, mens de lå i lejr på Moabs sletter ved Jordanfloden over for Jeriko.