Hesabu 33 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 33:1-56

Vituo Katika Safari Ya Waisraeli

133:1 Kut 17:1; 40:36; Hes 1:1; Kut 4:16; 6:26Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni. 233:2 Kut 17:4Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:

333:3 Hes 10:2; Mwa 47:11; Yos 5:10; Kut 14:8; 1:11; 12:37; 12:2; 13:4; Za 105:38; Isa 52:12; Kut 14:8Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote, 433:4 Kut 4:23; 2Nya 24:24; Yer 15:3; Eze 14:21; Kut 12:12; Isa 19:1; Sef 2:11; Ufu 12:8waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.

533:5 Kut 12:37Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.

633:6 Kut 13:20; Mwa 33:17; Yos 13:27; Za 60:6Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.

733:7 Kut 13:17, 18; 14:2, 9Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.

833:8 Kut 14:2; 14:22; 15:23Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.

933:9 Kut 15:27Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.

1033:10 Kut 16:1Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.

1133:11 Kut 16:1; 17:1Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.

12Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.

13Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.

1433:14 Kut 15:22; 17:2Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.

1533:15 Kut 17:1; 19:1Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.

1633:16 Hes 11:34Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.

1733:17 Hes 11; 35; Kum 9:22Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.

1833:18 Hes 12:16; Kum 1:1Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.

19Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.

2033:20 Yos 10:29; 12:15; 15:42; 21:13; 2Fal 8:22; 19:8; 23:31; 1Nya 6:57; 2Nya 21:10; Isa 37:8; Yer 52:1Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.

21Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.

22Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.

23Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.

24Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.

25Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.

26Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.

27Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.

28Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.

29Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.

3033:30 Kum 10:6Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.

3133:31 Kum 10:6Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.

3233:32 Mwa 36:27; Kum 10:6; 1Nya 1:42Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.

3333:33 Kum 10:7Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.

34Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.

3533:35 Kum 2:8; 1Fal 9:26; 22:48Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.

3633:36 Hes 13:21; 20:1; Kum 32:51; Yos 15:1Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.

3733:37 Hes 20:22; Mwa 36:16; Hes 20:16Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu. 3833:38 Hes 27:13; Kut 16:35; Hes 20:25-28; Kum 10:6; 32:50Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri. 39Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.

4033:40 Mwa 10:18; Hes 21:1; Mwa 12:9; Amu 1:16Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.

41Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.

42Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.

4333:43 Hes 21:10Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.

4433:44 Hes 21:11Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.

4533:45 Hes 32:34Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.

4633:46 Yer 48:22; Eze 6:14Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.

4733:47 Hes 27:12; 32:3; Kum 32:49Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.

4833:48 Hes 27:12; 26:3; Mwa 13:10; Hes 22:1; Yos 12:9Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko. 4933:49 Yos 12:3; 13:20; Eze 25:9; Hes 21:16Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.

5033:50 Hes 33:48; 34:2Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose, 5133:51 Kum 7:1; 9:1; Yos 3:17“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani, 5233:52 Law 26:1; Za 106:34-36; Kut 23:24; 34:12-17; Kum 7:2-5, 25, 26; Yos 11:12; 23:7; Amu 2:2wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada. 5333:53 Kum 11:31; 17:14; Yos 1:11; 21:43; Za 24:1; Ay 14:11; Dan 4:35Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki. 5433:54 Law 16:8; Hes 36:2; 26:54; 35:8; Yos 18:10Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.

5533:55 Yos 23:13; Amu 2:3; Za 106:36; Isa 55:13; Eze 2:6; 28:24; Mik 7:4; 2Kor 12:7; Kut 23:33; Mwa 17:8; Kum 1:7; Za 78:55; 105:11“ ‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi. 5633:56 Hes 14:28Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’ ”

New International Reader’s Version

Numbers 33:1-56

The Places Where Israel Camped During Their Journey

1Here are the places where the Israelites camped during their journey. When they came out of Egypt, they marched in groups like an army. Moses and Aaron led them. 2The Lord commanded Moses to record their journey. Here are the places where they camped.

3The Israelites started out from Rameses on the 15th day of the first month. It was the day after the Passover Feast. They marched out boldly in plain sight of all the Egyptians. 4The Egyptians were burying all their oldest sons. The Lord had struck them down. He had done it when he punished their gods.

5The Israelites left Rameses and camped at Sukkoth.

6They left Sukkoth and camped at Etham. Etham was on the edge of the desert.

7They left Etham and turned back to Pi Hahiroth. It was east of Baal Zephon. They camped near Migdol.

8They left Pi Hahiroth. Then they passed through the Red Sea into the desert. They traveled for three days in the Desert of Etham. Then they camped at Marah.

9They left Marah and went to Elim. Twelve springs and 70 palm trees were there. So they camped at Elim.

10They left Elim and camped by the Red Sea.

11They left the Red Sea and camped in the Desert of Sin.

12They left the Desert of Sin and camped at Dophkah.

13They left Dophkah and camped at Alush.

14They left Alush and camped at Rephidim. But there was no water there for the people to drink.

15They left Rephidim and camped in the Desert of Sinai.

16They left the Desert of Sinai and camped at Kibroth Hattaavah.

17They left Kibroth Hattaavah and camped at Hazeroth.

18They left Hazeroth and camped at Rithmah.

19They left Rithmah and camped at Rimmon Perez.

20They left Rimmon Perez and camped at Libnah.

21They left Libnah and camped at Rissah.

22They left Rissah and camped at Kehelathah.

23They left Kehelathah and camped at Mount Shepher.

24They left Mount Shepher and camped at Haradah.

25They left Haradah and camped at Makheloth.

26They left Makheloth and camped at Tahath.

27They left Tahath and camped at Terah.

28They left Terah and camped at Mithkah.

29They left Mithkah and camped at Hashmonah.

30They left Hashmonah and camped at Moseroth.

31They left Moseroth and camped at Bene Jaakan.

32They left Bene Jaakan and camped at Hor Haggidgad.

33They left Hor Haggidgad and camped at Jotbathah.

34They left Jotbathah and camped at Abronah.

35They left Abronah and camped at Ezion Geber.

36They left Ezion Geber and camped at Kadesh. Kadesh was in the Desert of Zin.

37They left Kadesh and camped at Mount Hor. It was on the border of Edom. 38Aaron the priest went up Mount Hor when the Lord commanded him to. That’s where he died. It happened on the first day of the fifth month. It was the 40th year after the Israelites came out of Egypt. 39Aaron was 123 years old when he died on Mount Hor.

40The Canaanite king of Arad lived in the Negev Desert in Canaan. He heard that the Israelites were coming.

41They left Mount Hor and camped at Zalmonah.

42They left Zalmonah and camped at Punon.

43They left Punon and camped at Oboth.

44They left Oboth and camped at Iye Abarim. It was on the border of Moab.

45They left Iye Abarim and camped at Dibon Gad.

46They left Dibon Gad and camped at Almon Diblathaim.

47They left Almon Diblathaim and camped in the mountains of Abarim near Nebo.

48They left the mountains of Abarim and camped on the plains of Moab. That area was by the Jordan River across from Jericho. 49They camped there along the Jordan River from Beth Jeshimoth to Abel Shittim.

50On the plains of Moab the Lord spoke to Moses. He spoke to him by the Jordan River across from Jericho. The Lord said, 51“Speak to the Israelites. Tell them, ‘Go across the Jordan River into Canaan. 52Drive out all those living in the land. The statues of their gods are made out of stone and metal. Destroy all those statues. And destroy all the high places where they are worshiped. 53Take the land as your own. Make your homes in it. I have given it to you. 54Cast lots when you divide up the land. Do it based on the number of people in each tribe and family. Give a larger share to a larger group. And give a smaller group a smaller share. The share they receive by casting lots will belong to them. Give out the shares based on the number of people in Israel’s tribes.

55“ ‘But suppose you do not drive out the people living in the land. Then those you allow to remain there will become like needles in your eyes. They will become like thorns in your sides. They will give you trouble in the land where you will live. 56Then I will do to you what I plan to do to them.’ ”