Hesabu 12 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 12:1-16

Miriamu Na Aroni Wampinga Mose

112:1 Kut 15:20; 2:21Miriamu na Aroni walianza kuzungumza dhidi ya Mose kwa sababu ya mke wake Mkushi, kwa kuwa alikuwa ameoa Mkushi. 212:2 Hes 16:3; 11:1; Mwa 29:33; Mik 6:4; 2Fal 19:4; Za 94:9; Eze 35:12Waliuliza, “Je, Bwana amesema kupitia Mose peke yake? Je, hajasema kutupitia sisi pia?” Naye Bwana akasikia hili.

312:3 Mt 11:29; 1Tim 6:11; 2Tim 2:25; Za 149:4; 1Pet 3:4(Basi Mose alikuwa mtu mnyenyekevu sana, mnyenyekevu kuliko mtu mwingine yeyote katika uso wa dunia.)

4Ghafula Bwana akawaambia Mose, Aroni na Miriamu, “Njooni katika Hema la Kukutania, ninyi nyote watatu.” Kwa hiyo wote watatu wakaenda. 512:5 Kut 13:21; Hes 11:25; Kut 34:5Kisha Bwana akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye ingilio la Hema, akawaita Aroni na Miriamu. Wakati wote wawili waliposogea mbele, 612:6 1Sam 3:7, 21; Mwa 15:1; 20:3; 46:2; Mt 27:19; Ebr 1:1; 1Fal 3:5; Mwa 46:2; Ay 33:15; Lk 1:11; 1:22; Mt 1:20Bwana akasema, “Sikilizeni maneno yangu:

“Akiwapo nabii wa Bwana miongoni mwenu,

nitajifunua kwake kwa maono,

nitanena naye katika ndoto.

712:7 Kum 34:5; Yos 1:1-2; Za 105:26; Ebr 3:2, 5Lakini sivyo kwa mtumishi wangu Mose;

yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote.

812:8 Amu 14:12; 1Fal 10:1; Za 17:15; 49:4; 140:13; Mit 1:6; Dan 5:12; Kut 20:4; 24:2; Ay 19:26; Isa 6:1Kwake nitanena naye uso kwa uso,

waziwazi wala si kwa mafumbo;

yeye ataona umbo la Bwana.

Kwa nini basi ninyi hamkuogopa

kuzungumza kinyume cha mtumishi wangu Mose?”

912:9 Kut 4:14; Mwa 17:22Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao, akawaacha.

1012:10 Kut 4:6; 40:2; Kum 24:9; Law 13:11; 2Fal 5:1, 27; 2Nya 16:12; 21:12Wakati hilo wingu liliinuka kutoka juu ya Hema, Miriamu akawa tayari ana ukoma, mweupe kama theluji. Aroni akamgeukia, akaona ana ukoma. 1112:11 2Sam 19:19; 24:10Kisha Aroni akamwambia Mose, “Tafadhali, bwana wangu, usituhesabie dhambi hii ambayo tumeifanya kwa upumbavu. 1212:12 Za 88:4; Efe 2:1-5; Kol 2:13; 1Tim 5:6Usimwache awe kama mtoto mchanga aliyezaliwa akiwa mfu, ambaye nusu ya mwili wake imeharibika hapo atokapo katika tumbo la mama yake.”

1312:13 Kut 15:26; Za 6:2; 147:3; Isa 1:6; 30:26; 53:5; Yer 17:14; Hos 6:1Hivyo Mose akamlilia Bwana akisema, “Ee Mungu, nakuomba umponye!”

1412:14 Kum 25:9; Ay 17:6; 30:9-10; Isa 50:6; Law 13:46; Hes 5:2-3; Ebr 12:9; 2Nya 26:20, 21Bwana akamjibu Mose, “Je, kama baba yake angemtemea usoni, asingeona aibu kwa siku saba? Mfungie nje ya kambi kwa siku saba; baada ya hapo anaweza kurudishwa kambini.” 1512:15 Law 14:8; 13; Kum 24:9Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba, nao watu hawakuendelea na safari mpaka aliporudishwa kambini.

1612:16 Hes 10:12; 11:35; 15:32; Mwa 21:21Baada ya hayo, watu waliondoka Haserothi, wakapiga kambi katika Jangwa la Parani.

Swedish Contemporary Bible

4 Moseboken 12:1-15

Mirjam och Aron kritiserar Mose

1Då började Mirjam och Aron att kritisera Mose därför att han tagit en kushitisk kvinna till hustru. 2De sa: ”Är det bara genom Mose som Herren har talat? Har han inte talat genom oss också?”

Herren hörde det. 3Mose var den mest ödmjuka människa som fanns på jorden. 4Herren sa genast till Mose, Aron och Mirjam: ”Gå ut alla tre till uppenbarelsetältet!” Då gick de tre dit. 5Herren steg ner till dem i en molnpelare och ställde sig vid ingången till tältet. Han kallade på Aron och Mirjam. De steg då fram 6och han sa:

”Hör nu mina ord!

Om det finns en profet bland er

uppenbarar jag mig själv för honom

genom syner och drömmar.

7Men inte så med min tjänare Mose.

Han har förtroende här i mitt hus

8och med honom talar jag ansikte mot ansikte

i klartext och inte i gåtor.

Han får se Herrens gestalt.

Hur vågar ni då kritisera min tjänare Mose?”

9Herrens vrede brann mot dem och han lämnade dem. 10När molnet flyttade sig från tältet, var Mirjam alldeles snövit av spetälska. Aron vände sig mot henne och fick se hennes spetälska. 11Då sa Aron till Mose: ”O, min herre, straffa oss inte för den synd vi begått! Vi har handlat dåraktigt. 12Låt henne inte bli som ett dödfött foster som kommer halvruttet ur moderlivet!”

13”Gud, jag ber dig, gör henne frisk igen!” ropade då Mose till Herren. 14Och Herren sa till Mose: ”Om hennes far hade spottat henne i ansiktet, skulle hon ju ha fått bära sin skam i sju dagar. Låt henne nu hålla sig utanför lägret i sju dagar och sedan kan hon få komma tillbaka.”

15Mirjam blev alltså utestängd från lägret i sju dagar. Folket väntade med att gå vidare tills hon kom tillbaka.