Hesabu 11 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 11:1-35

Moto Kutoka Kwa Bwana

111:1 Law 10:2; Kut 4:14; 14:11; 16:7; Mao 3:39; Hes 12:2; 21:28; Kum 1:34; Za 78:63; Isa 26:11; Kut 15:23, 24; 16:2, 3, 7; Kum 9:22; 2Fal 1:12Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi. 211:2 Kum 9:19; 1Sam 2:25; 12:23; Za 106:23; Mwa 20:7; Hes 21:7; Yn 2:1Watu walipomlilia Mose, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika. 311:3 Kum 9:20-22; Hes 16:35; Ay 1:16; Isa 10:17Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera,11:3 Tabera maana yake Kunaungua. kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.

Kware Kutoka Kwa Bwana

411:4 Kut 12:38; 16:3; Za 78:18; 1Kor 10:6Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! 511:5 Kut 16:3; Hes 21:5; Flp 3:19; Mt 6:24-34; Rum 8:7Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu. 611:6 Kut 16:14Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”

711:7 Kut 16:31; Mwa 2:12; 2:12Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka. 811:8 Kut 16:16Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni. 911:9 Kut 16:13Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.

10Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Bwana akakasirika mno, naye Mose akafadhaika. 1111:11 Mwa 34:30; Kut 5:22; 18:18; 17:4; Kum 1:12; Yer 15:10, 18; 20:7-18; Mal 3:14; 2Kor 11:28Akamuuliza Bwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu? 1211:12 Isa 40:11; 49:23; 66:11, 12; Hes 14:16; Mwa 12:7; Kut 13:5; Eze 34:23; Yn 10:11; 1The 2:7; Mwa 22:16; 26:3Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao? 1311:13 Kut 12:37; Yn 6:5-9; 2Fal 4:43; Mt 15:33; Mk 8:4Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’ 1411:14 Kut 18:18Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu. 1511:15 Kut 32:32; 1Fal 19:4; Ay 6:9; 7:15-16; 9:21; Isa 38:12; Yn 4:3Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”

1611:16 Kut 3:16; 18:25; 40:2; 24:1, 9Bwana akamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe. 1711:17 Kut 18:18; 19:20; 1Sam 10:6; 2Fal 2:9, 15; 3:12; Isa 32:15; Yoe 2:28; Hag 2:5; Yer 19:1Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.

1811:18 Kut 19:10; 16:7; Mdo 7:39; Za 78:20“Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama. Bwana aliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” Sasa Bwana atawapa nyama, nanyi mtaila. 19Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini, 2011:20 Za 78:29; 106:14-15; Law 26:43; Ay 1:14; 20:13, 23; Yos 24:27; Amu 8:23; 1Sam 10:19; Isa 59:13; Hos 13:11bali kwa mwezi mzima mpaka iwatokee puani, nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataa Bwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?” ’ ”

2111:21 Kut 12:37Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama ya kula kwa mwezi mzima!’ 2211:22 Mt 15:33; 2Fal 7:2; Mk 6:37Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ngʼombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”

2311:23 Isa 50:2; 59:1; Hes 23:19; 1Sam 15:29; Eze 12:25; 24:14Bwana akamjibu Mose, “Je, mkono wa Bwana ni mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema litatimizwa kwa ajili yako au la.”

24Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambalo Bwana alikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema. 2511:25 Kut 19:9; Hes 12:5; 1Sam 10:6, 10; 19:20, 23; Mdo 2:17; Amu 3:10; Kut 34:5; 40:38; 2Fal 2:15; Yoe 2:29; 1Kor 14:1Kisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.

2611:26 1Nya 12:18; Ufu 1:10; 1Sam 20:26; Yer 36:5Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini. 27Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”

2811:28 Kut 17:9; 33:11; Hes 13:8; 26:65; Yos 14:10; Mk 9:38-40; Mdo 26:29; 1Kor 14:5Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”

2911:29 1Sam 10:5; 19:20; 2Nya 24:19; Yer 7:25; 44:4; 1Kor 14:5; Hes 27:18Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!” 30Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.

3111:31 Kut 16:13; Za 78:26-28Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande. 3211:32 Kut 16:36; Eze 45:11Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi.11:32 Homeri 10 ni sawa na kilo 1,000. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote. 3311:33 Za 78:30; 106:15, 29; Hes 14:18; Kum 9:7; Amu 2:12; 2Fal 22:17; Yer 44:3; Eze 8:17; Isa 10:16Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni. 3411:34 Hes 33:16; Kum 9:22Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava,11:34 Kibroth-Hataava maana yake Makaburi ya wenye tamaa nyingi. kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.

3511:35 Hes 33:17; Kum 1:1Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

民数记 11:1-35

以色列人发怨言

1民众因为困难而发怨言,传到耶和华耳中。耶和华听见后便向他们发怒,使火在他们中间燃烧,烧毁了营地的边缘部分。 2民众呼求摩西摩西便向耶和华祷告,火就熄了。 3那地方叫他备拉,因为耶和华的火曾在他们中间燃烧。

4他们中间有一群乌合之众贪恋从前的食物,以色列人也哭着说:“要是有肉吃多好啊! 5还记得在埃及的时候,我们不花钱就可以吃鱼,还有黄瓜、西瓜、韭菜、葱和蒜。 6我们现在毫无胃口,眼前除了吗哪外,什么都没有。” 7吗哪的形状像芫荽籽,又像珍珠。 8-9每天晚上露水降在营地上时,吗哪也随着降下来。早晨民众到四周捡吗哪,把吗哪磨碎或捣碎后,放在锅里煮,再做成饼,味道就像油饼。 10听见民众都在自己帐篷门口哭泣,惹耶和华发怒,摩西感到难过, 11就对耶和华说:“你为什么为难仆人?我做了什么令你不悦的事,你竟把管理这些民众的重担放在我身上? 12难道他们是我的骨肉,是我生的吗?为什么你要我像父亲呵护儿子一样,把他们抱到你应许给他们祖先的地方呢? 13他们都哭着向我要肉吃,我去哪里找肉给他们吃呢? 14管理民众的责任实在是太重了,我一个人担当不起啊! 15你既然这样对待我,求你施恩杀了我吧,别让我受苦了!”

16耶和华对摩西说:“你给我招聚七十个以色列人的长老——你所了解的首领,把他们带到会幕,让他们站在你身边。 17我要在那里降临,对你说话,把降在你身上的灵也赐给他们,让他们为你分担管理民众的责任,免得你独自承担。 18你要叫民众洁净自己,到明天就会有肉吃。因为我听见了他们哭着要肉吃、说埃及的日子更好,我必给他们肉吃。 19他们将不止吃一天、两天、五天、十天或二十天, 20而是要吃整整一个月,直到肉从他们鼻孔里喷出来,令他们厌腻。因为他们厌弃我,在我面前哭诉,后悔离开埃及。” 21摩西说:“和我同行的,仅男子就有六十万,你还说要让他们吃整整一个月的肉! 22就是把牛羊都宰了,把海里的鱼都捕来,恐怕也不够他们吃!” 23耶和华说:“难道我的臂膀能力不够吗?你很快将看见我的话会不会应验。”

24摩西就出去把耶和华的话转告民众,又选了七十位长老,叫他们站在会幕周围。 25耶和华在云中降临,对摩西说话,把降在摩西身上的灵也赐给七十位长老。灵一降在他们身上,他们就说起预言来,但只说了这一次。 26七十位长老中的伊利达米达没有到会幕去,但耶和华的灵也降在他们身上,他们就在营中说起预言来。 27有一个青年跑去禀告摩西说:“伊利达米达正在营中说预言。” 28摩西拣选的助手——的儿子约书亚就说:“我主摩西,请你禁止他们。” 29摩西说:“你是怕我的权威受影响吗?愿耶和华的子民都成为先知!愿耶和华把祂的灵降在他们身上!” 30之后,摩西以色列的长老都返回营中。

耶和华赐下鹌鹑

31耶和华刮起一阵风,把鹌鹑从海面刮到营地四周,达一米之厚,方圆数公里。 32民众花了两天一夜的时间去捕捉鹌鹑,每人至少捉了一吨。他们把鹌鹑摊在营地的周围。 33他们口中的肉还没嚼烂,耶和华的怒气就已向他们发作,降下了大灾。 34因此,那地方叫基博罗·哈他瓦11:34 基博罗·哈他瓦”意思是“贪欲之墓”。,因为那些贪食者埋葬在那里。 35民众从基博罗·哈他瓦前往哈洗录,在哈洗录住了下来。