Hesabu 11 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 11:1-35

Moto Kutoka Kwa Bwana

111:1 Law 10:2; Kut 4:14; 14:11; 16:7; Mao 3:39; Hes 12:2; 21:28; Kum 1:34; Za 78:63; Isa 26:11; Kut 15:23, 24; 16:2, 3, 7; Kum 9:22; 2Fal 1:12Basi watu wakalalamika kwa habari ya taabu zao masikioni mwa Bwana, naye alipowasikia, hasira yake ikawaka. Ndipo moto kutoka kwa Bwana ukawaka miongoni mwao na kuteketeza baadhi ya viunga vya kambi. 211:2 Kum 9:19; 1Sam 2:25; 12:23; Za 106:23; Mwa 20:7; Hes 21:7; Yn 2:1Watu walipomlilia Mose, akamwomba Bwana, nao moto ukazimika. 311:3 Kum 9:20-22; Hes 16:35; Ay 1:16; Isa 10:17Hivyo mahali pale pakaitwa Tabera,11:3 Tabera maana yake Kunaungua. kwa sababu moto kutoka kwa Bwana uliwaka miongoni mwao.

Kware Kutoka Kwa Bwana

411:4 Kut 12:38; 16:3; Za 78:18; 1Kor 10:6Umati wa watu wenye zogo waliokuwa miongoni mwao walitamani sana chakula kingine, Waisraeli wakaanza kulia tena na kusema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! 511:5 Kut 16:3; Hes 21:5; Flp 3:19; Mt 6:24-34; Rum 8:7Tunakumbuka wale samaki tuliokula huko Misri bila gharama, pia yale matango, matikitimaji, mboga, vitunguu, na vitunguu saumu. 611:6 Kut 16:14Lakini sasa tumepoteza hamu ya chakula; hatuoni kitu kingine chochote isipokuwa hii mana!”

711:7 Kut 16:31; Mwa 2:12; 2:12Mana ilifanana kama mbegu za giligilani, nayo ilikuwa na rangi ya manjano iliyopauka. 811:8 Kut 16:16Hao watu walikwenda kukusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia ya mkono au kuitwanga kwenye vinu. Waliipika vyunguni au kutengeneza maandazi. Ladha yake ilikuwa kama kitu kilichotengenezwa kwa mafuta ya zeituni. 911:9 Kut 16:13Umande ulipoanguka kambini wakati wa usiku, pia mana ilianguka pamoja nao.

10Mose akasikia watu wa kila jamaa wakilia, kila mmoja kwenye mlango wa hema lake. Bwana akakasirika mno, naye Mose akafadhaika. 1111:11 Mwa 34:30; Kut 5:22; 18:18; 17:4; Kum 1:12; Yer 15:10, 18; 20:7-18; Mal 3:14; 2Kor 11:28Akamuuliza Bwana, “Kwa nini umeleta taabu hii juu ya mtumishi wako? Nimekufanyia nini cha kukuchukiza hata ukaweka mzigo huu wa watu hawa wote juu yangu? 1211:12 Isa 40:11; 49:23; 66:11, 12; Hes 14:16; Mwa 12:7; Kut 13:5; Eze 34:23; Yn 10:11; 1The 2:7; Mwa 22:16; 26:3Je, watu hawa wote mimi ndiye niliyewatungisha mimba? Je, ni mimi niliyewazaa? Kwa nini unaniambia niwachukue mikononi mwangu, kama vile mlezi abebavyo mtoto mchanga, hadi kwenye nchi uliyowaahidi baba zao? 1311:13 Kut 12:37; Yn 6:5-9; 2Fal 4:43; Mt 15:33; Mk 8:4Nitapata wapi nyama kwa ajili ya watu wote hawa? Wanaendelea kunililia wakisema, ‘Tupe nyama tule!’ 1411:14 Kut 18:18Mimi siwezi kuwabeba watu hawa wote peke yangu, mzigo ni mzito sana kwangu. 1511:15 Kut 32:32; 1Fal 19:4; Ay 6:9; 7:15-16; 9:21; Isa 38:12; Yn 4:3Kama hivi ndivyo unavyonitendea, uniue sasa hivi, yaani kama nimepata kibali machoni pako, wala usiniache nione maangamizi yangu mwenyewe.”

1611:16 Kut 3:16; 18:25; 40:2; 24:1, 9Bwana akamwambia Mose: “Niletee wazee sabini wa Israeli, unaowafahamu kama viongozi na maafisa miongoni mwa watu. Walete katika Hema la Kukutania, ili waweze kusimama huko pamoja nawe. 1711:17 Kut 18:18; 19:20; 1Sam 10:6; 2Fal 2:9, 15; 3:12; Isa 32:15; Yoe 2:28; Hag 2:5; Yer 19:1Nami nitashuka na kusema nawe huko. Nami nitachukua sehemu ya Roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao. Watakusaidia kubeba mzigo wa watu hao ili usije ukaubeba peke yako.

1811:18 Kut 19:10; 16:7; Mdo 7:39; Za 78:20“Waambie hao watu: ‘Jiwekeni wakfu wenyewe kwa ajili ya kesho, wakati mtakapokula nyama. Bwana aliwasikia mlipolia, mkisema, “Laiti tungekuwa na nyama tule! Tulikuwa na hali nzuri zaidi katika nchi ya Misri!” Sasa Bwana atawapa nyama, nanyi mtaila. 19Hamtaila kwa siku moja tu, au siku mbili, au tano, kumi au siku ishirini, 2011:20 Za 78:29; 106:14-15; Law 26:43; Ay 1:14; 20:13, 23; Yos 24:27; Amu 8:23; 1Sam 10:19; Isa 59:13; Hos 13:11bali kwa mwezi mzima mpaka iwatokee puani, nanyi mtaichukia kabisa, kwa kuwa mmemkataa Bwana, ambaye yupo miongoni mwenu, nanyi mmelia mbele zake, mkisema, “Hivi kwa nini tulitoka Misri?” ’ ”

2111:21 Kut 12:37Lakini Mose alisema, “Mimi niko hapa miongoni mwa watu 600,000 wanaotembea kwa miguu, nawe umesema, ‘Nitawapa nyama ya kula kwa mwezi mzima!’ 2211:22 Mt 15:33; 2Fal 7:2; Mk 6:37Je, wangeweza kupata nyama ya kuwatosha hata kama makundi ya kondoo na ya ngʼombe yangechinjwa kwa ajili yao? Je, wangetosheka hata kama samaki wote wa baharini wangevuliwa kwa ajili yao?”

2311:23 Isa 50:2; 59:1; Hes 23:19; 1Sam 15:29; Eze 12:25; 24:14Bwana akamjibu Mose, “Je, mkono wa Bwana ni mfupi sana? Sasa utaona kama jambo nililolisema litatimizwa kwa ajili yako au la.”

24Kwa hiyo Mose akatoka na kuwaambia watu lile ambalo Bwana alikuwa amesema. Akawakusanya wazee wao sabini, akawasimamisha kuzunguka Hema. 2511:25 Kut 19:9; Hes 12:5; 1Sam 10:6, 10; 19:20, 23; Mdo 2:17; Amu 3:10; Kut 34:5; 40:38; 2Fal 2:15; Yoe 2:29; 1Kor 14:1Kisha Bwana akashuka katika wingu na kunena na Mose, naye akachukua sehemu ya Roho iliyokuwa juu ya Mose na kuiweka juu ya wale wazee sabini. Roho aliposhuka juu yao, wakatoa unabii, lakini hawakufanya hivyo tena.

2611:26 1Nya 12:18; Ufu 1:10; 1Sam 20:26; Yer 36:5Lakini, watu wawili, ambao majina yao ni Eldadi na Medadi, walibaki kambini. Walikuwa wameorodheshwa miongoni mwa wale wazee sabini, lakini hawakutoka kwenda kwenye Hema. Lakini Roho pia alishuka juu yao, nao wakatabiri huko kambini. 27Mwanaume mmoja kijana alikimbia na kumwambia Mose, “Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”

2811:28 Kut 17:9; 33:11; Hes 13:8; 26:65; Yos 14:10; Mk 9:38-40; Mdo 26:29; 1Kor 14:5Yoshua mwana wa Nuni, ambaye alikuwa msaidizi wa Mose tangu ujana wake, akajibu akasema, “Mose bwana wangu, wanyamazishe!”

2911:29 1Sam 10:5; 19:20; 2Nya 24:19; Yer 7:25; 44:4; 1Kor 14:5; Hes 27:18Lakini Mose akajibu, “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Ningetamani watu wote wa Bwana wangekuwa manabii na kwamba Bwana angeweka Roho yake juu yao!” 30Ndipo Mose na wale wazee wa Israeli wakarudi kambini.

3111:31 Kut 16:13; Za 78:26-28Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande. 3211:32 Kut 16:36; Eze 45:11Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi.11:32 Homeri 10 ni sawa na kilo 1,000. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote. 3311:33 Za 78:30; 106:15, 29; Hes 14:18; Kum 9:7; Amu 2:12; 2Fal 22:17; Yer 44:3; Eze 8:17; Isa 10:16Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni. 3411:34 Hes 33:16; Kum 9:22Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava,11:34 Kibroth-Hataava maana yake Makaburi ya wenye tamaa nyingi. kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.

3511:35 Hes 33:17; Kum 1:1Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.

La Bible du Semeur

Nombres 11:1-35

Les premières crises

Les Israélites se plaignent

1Un jour, le peuple adressa d’amères plaintes à l’Eternel. Lorsqu’il les entendit, il se mit en colère et déchaîna la foudre contre eux. Déjà, le feu dévorait une extrémité du camp.

2Le peuple implora Moïse à grands cris ; celui-ci pria l’Eternel, et le feu s’arrêta. 3On appela ce lieu Tabeéra, parce que le feu de l’Eternel s’était embrasé contre le peuple.

4Il y avait parmi le peuple un ramassis d’individus qui furent saisis de toutes sortes de désirs. Alors les Israélites, à leur tour, recommencèrent à pleurer en disant : Ah ! Si seulement nous pouvions manger de la viande ! 5Nous regrettons le poisson qu’on mangeait pour rien en Egypte ! Et les concombres ! Et les melons ! Et les poireaux ! Et les oignons ! Et l’ail ! 6A présent, nous dépérissons. Nous sommes privés de tout, rien que de la manne, toujours de la manne !

7La manne ressemblait à de la graine de coriandre, elle était transparente comme de la résine de bdellium11.7 Voir Ex 16.31.. 8Le peuple se dispersait pour la ramasser ; puis on la broyait à la meule ou la pilait au mortier, et on la faisait cuire dans des pots pour en faire des galettes qui avaient un goût de gâteau à l’huile. 9Elle se déposait la nuit sur le camp avec la rosée11.9 Voir Ex 16.13-15..

10Chaque famille se lamentait à l’entrée de sa tente. Moïse entendit le peuple pleurer, et l’Eternel entra dans une grande colère. Moïse en fut très affecté. 11Il dit à l’Eternel : Pourquoi fais-tu du mal à ton serviteur ? Pourquoi ne m’accordes-tu pas ta faveur ? Comment peux-tu m’imposer la charge de tout ce peuple ? 12Est-ce moi qui ai conçu tout ce peuple ? Est-ce moi qui l’ai mis au monde pour que tu me dises : « Porte-le sur ton cœur comme une nourrice porte le bébé qu’elle allaite, et cela jusqu’au pays que tu as promis à ses ancêtres » ? 13Où trouverai-je de la viande pour la distribuer à tous ces gens qui pleurent autour de moi en disant : « Donne-nous de la viande à manger ! » 14Je ne suis pas capable de porter, à moi seul, la responsabilité de tout ce peuple. C’est trop lourd pour moi ! 15Si tu veux bien m’accorder une faveur, prends ma vie plutôt que de me traiter ainsi, et que je n’aie plus à contempler mon malheur.

Les soixante-dix responsables du peuple adjoints à Moïse

16L’Eternel répondit à Moïse : Rassemble-moi soixante-dix hommes choisis parmi les responsables d’Israël, des hommes que tu sais être des responsables et des chefs du peuple, et amène-les devant la tente de la Rencontre. Qu’ils se tiennent là avec toi. 17Alors je descendrai m’entretenir là avec toi, je prendrai de l’Esprit qui est sur toi et je le leur donnerai, pour qu’ils portent avec toi la charge de ce peuple, de sorte que tu n’auras plus à la porter seul. 18Tu diras au peuple : « Purifiez-vous pour demain, et vous mangerez de la viande, puisque vous avez pleuré aux oreilles de l’Eternel en disant : “Ah ! Si seulement nous pouvions manger de la viande ! Nous étions si bien en Egypte !” Eh bien, l’Eternel va vous donner de la viande à manger. 19Pas un seul jour, ni deux jours, ni cinq jours, ni dix jours, ni même vingt jours, 20mais durant tout un mois vous en mangerez, jusqu’à ce qu’elle vous sorte par les narines et que vous en ayez la nausée. Car vous avez méprisé l’Eternel qui est au milieu de vous, et vous avez pleuré devant lui, en disant : “Pourquoi donc avons-nous quitté l’Egypte ?” »

21Moïse répondit : Ce peuple dont je fais partie compte six cent mille hommes de pied, et toi tu leur promets, pour un mois entier, de la viande à manger ! 22Abattra-t-on pour eux des brebis et des bœufs pour qu’ils en aient suffisamment ? Et même si on leur pêchait tous les poissons de la mer, en auraient-ils assez ?

23L’Eternel lui répondit : Le bras de l’Eternel serait-il trop court ? Tu verras sans tarder si, oui ou non, ma parole se réalise devant toi.

L’Esprit de Dieu se pose sur les soixante-dix responsables du peuple

24Moïse sortit et rapporta au peuple les paroles de l’Eternel, puis il rassembla soixante-dix hommes choisis parmi leurs responsables, et les plaça autour de la tente. 25L’Eternel descendit dans la nuée et lui parla ; il prit de l’Esprit qui reposait sur lui et le donna à ces soixante-dix responsables. Quand l’Esprit se fut posé sur eux, ils se mirent à parler sous son inspiration, comme des prophètes – c’est l’unique fois que cela leur arriva.

26L’Esprit vint également demeurer sur deux hommes qui se trouvaient dans le camp, et qui s’appelaient Eldad et Médad. L’Esprit vint reposer sur eux car ils figuraient parmi les inscrits, bien qu’ils ne se soient pas rendus à la tente, et, dans le camp, ils se mirent à parler sous l’inspiration de Dieu. 27Un jeune homme courut avertir Moïse : Eldad et Médad sont en train de parler sous l’inspiration de Dieu dans le camp !

28Alors Josué, fils de Noun, qui était l’assistant de Moïse depuis sa jeunesse, intervint en disant : Moïse, mon maître, empêche-les de faire cela !

29Moïse lui répondit : Serais-tu jaloux pour moi ? Que l’Eternel, au contraire, accorde son Esprit à tous les membres de son peuple pour qu’ils deviennent tous des prophètes !

30Puis Moïse regagna le camp avec les responsables d’Israël.

31Un vent envoyé par l’Eternel entraîna des cailles par-dessus la mer et les fit s’abattre autour du camp, sur un rayon d’une journée de marche. Elles recouvraient le sol jusqu’à un mètre de hauteur. 32Le peuple fut debout toute cette journée et toute la nuit, et encore tout le lendemain, pour ramasser les cailles. Personne n’en prit moins d’une tonne11.32 En hébreu, il s’agit de dix homers. Le homer contenait environ 360 litres.. Ils les étalèrent tout autour du camp.

33Ils avaient encore la viande à la bouche quand la colère de l’Eternel éclata contre le peuple, et il le frappa d’une grave épidémie. 34On appela cet endroit Qibroth-Hattaava (Tombeaux de la convoitise), car c’est là qu’on enterra beaucoup de gens, qui avaient cédé à la convoitise11.34 L’apôtre Paul fait allusion à cet épisode dans 1 Co 10.6.. 35De Qibroth-Hattaava le peuple se mit en marche pour Hatséroth, où il s’installa.