Hagai 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hagai 1:1-15

Wito Wa Kuijenga Nyumba Ya Bwana

11:1 Ezr 4:24; 5:1-3; 2:2; 3:2; 1Nya 3:19; 6:15; Mt 1:12-13Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua1:1 Yoshua kwa Kiebrania ni Yeshua, maana yake ni Yehova ni wokovu. mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:

21:2 Isa 13:4; 29:13Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’ ”

31:3 Ezr 5:1Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai: 41:4 2Sam 7:2; Yer 33:12“Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”

51:5 Mao 3:40; Hag 2:15-18Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu. 61:6 Law 26:20; Isa 5:10; 9:20; 55:2; Amo 4:8; Hag 2:16; Zek 8:10Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”

7Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu. 81:8 Ay 22:3; Yer 13:11; 1Nya 14:1; Za 132:13-14; Kut 29:43Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana. 91:9 Kum 28:38; Isa 5:10; Neh 13:11; Za 103:16; Eze 22:21“Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe. 101:10 Kum 28:24; Mwa 27:28; 1Fal 17:1; 2Nya 6:26; Yer 3:3; Law 26:19; Yoe 1:18-19Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake. 111:11 Kum 11:26; 28:22; Rut 1:1; 1Fal 17:1; Hag 2:17; Isa 5:6; 7:25; Hes 18:12Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”

121:12 Isa 1:9; 50:10; 55:11; Mt 28:20; Kum 31:12; Hag 2:2; Ezr 5:2; Mhu 12:13; Ay 36:11Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.

131:13 Hes 14:9; 27:21; 2Nya 15:2; 36:15; Mwa 26:3; Rum 8:31; Isa 41:10; Mt 28:20Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana. 141:14 Ezr 5:2; Za 110:3; 2Nya 36:22; Hag 2:21; 1Nya 6:15; 1Kor 15:58Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao, 151:15 Hag 2:10, 20; Ezr 4:24katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

哈該書 1:1-15

耶和華命令百姓重建聖殿

1大流士王執政第二年六月一日,耶和華藉著先知哈該撒拉鐵的兒子猶大省長所羅巴伯約撒答的兒子大祭司約書亞說:

2「萬軍之耶和華說,『這些百姓說,重建耶和華殿的時候還沒到。』」 3因此,耶和華對先知哈該說: 4「這殿還是一片廢墟,你們卻住在華麗的房子裡。 5萬軍之耶和華說,你們要認真反省自己的行為。 6你們種多收少,吃不飽,喝不足,穿不暖,掙來的工錢卻放在漏口袋中。」

7萬軍之耶和華說:「你們要認真反省自己的行為。 8你們要上山伐木,重建這殿,好讓我歡喜並得到尊崇。這是耶和華說的。 9你們盼望豐收,結果收的很少;你們把收成帶回家,我卻把它們吹走。這是什麼緣故?萬軍之耶和華告訴你們,『因為你們都忙於建自家的房子,任由我的殿一片廢墟。 10所以,天不降雨露,地無出產。 11我讓旱災臨到大地、群山、五穀、葡萄、橄欖等地裡的出產以及人畜,使你們一切的勞碌付諸東流。』」

12撒拉鐵的兒子猶大省長所羅巴伯約撒答的兒子大祭司約書亞和所有的餘民1·12 餘民」指「從流亡之地歸回的人」。聽到他們的上帝耶和華藉先知哈該所講的話,都順服耶和華的話。百姓都敬畏耶和華。 13耶和華的使者哈該向百姓傳達耶和華的話,說:「耶和華說,『我與你們同在。』」 14耶和華感動撒拉鐵的兒子猶大省長所羅巴伯約撒答的兒子大祭司約書亞和所有的餘民,他們就動工建造他們的上帝萬軍之耶和華的殿, 15時值大流士王執政第二年六月二十四日。