Ezra 8 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezra 8:1-36

Orodha Ya Viongozi Wa Jamaa Waliorudi Na Ezra

18:1 Ezr 7:7Hawa ndio viongozi wa jamaa pamoja na wale walioandikwa ambao walikuja pamoja nami kutoka Babeli wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:

28:2 1Nya 3:22wa wazao wa Finehasi, alikuwa Gershoni;

wa wazao wa Ithamari, alikuwa Danieli;

wa wazao wa Daudi, alikuwa Hatushi 38:3 1Nya 3:22; Ezr 2:3wa wazao wa Shekania;

wa wazao wa Paroshi, alikuwa Zekaria, na watu 150 walioandikishwa pamoja naye;

48:4 Ezr 2:6wa wazao wa Pahath-Moabu, alikuwa Eliehoenai mwana wa Zerahia na wanaume 200 pamoja naye;

5wa wazao wa Zatu, alikuwa Shekania mwana wa Yahazieli na wanaume 300 pamoja naye;

68:6 Ezr 2:15; Neh 7:20wa wazao wa Adini, alikuwa Ebedi mwana wa Yonathani na wanaume 50 pamoja naye;

7wa wazao wa Elamu, alikuwa Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;

8wa wazao wa Shefatia, alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli na wanaume 80 pamoja naye;

9wa wazao wa Yoabu, alikuwa Obadia mwana wa Yehieli na wanaume 218 pamoja naye;

10wa wazao wa Bani, alikuwa Shelomithi mwana wa Yosifia na wanaume 160 pamoja naye;

11wa wazao wa Bebai, alikuwa Zekaria mwana wa Bebai na wanaume 28 pamoja naye;

12wa wazao wa Azgadi, alikuwa Yohanani mwana wa Hakatani na wanaume 110 pamoja naye;

138:13 Ezr 2:13wa wazao wa Adonikamu, hawa walikuwa wa mwisho ambao majina yao ni Elifeleti, Yeueli, Shemaya na wanaume 60 pamoja nao;

14wa wazao wa Bigwai, walikuwa Uthai na Zakuri na wanaume 70 pamoja nao.

Kurudi Yerusalemu

158:15 Ezr 2:40; 7:7; Mdo 16:13; 20:28; Za 137:1; Mit 27:23; Ebr 13:17; Ezr 7:7; Hes 8:1Niliwakusanya kwenye mto utiririkao kuelekea Ahava, nasi tukapiga kambi pale siku tatu. Wakati nilipokagua kati ya watu na makuhani, sikuwapata Walawi. 16Basi niliwaita Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu waliokuwa viongozi na Yoyaribu na Elnathani waliokuwa wasomi, 178:17 Ezr 2:43nikawatuma kwa Ido kiongozi huko Kasifia. Niliwaambia watakayomwambia Ido na ndugu zake, watumishi wa Hekalu8:17 Yaani Wanethini (pia 8:20). huko Kasifia, ili waweze kutuletea wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu. 188:18 Ezr 5:5Kwa sababu mkono wa neema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea Sherebia, mtu mwenye uwezo kutoka wazao wa Mahli mwana wa Lawi, mwana wa Israeli, na wana wa Sherebia pamoja na ndugu zao wanaume kumi na wanane. 19Naye Hashabia, pamoja na Yeshaya kutoka wazao wa Merari na ndugu zake na wapwa wake wanaume ishirini. 208:20 1Nya 9:2; Ezr 2:43Vilevile walileta watumishi wa Hekalu 220, kikundi ambacho Daudi na maafisa walikuwa wamekiweka kusaidia Walawi. Wote walikuwa wameorodheshwa kwa majina.

218:21 2Nya 9:2; Ezr 2:438:21 2Nya 20:3; Za 27:11; Law 16:29; Za 5:8; 2Nya 20:3; Law 16:29; Isa 58:3-5Kando ya Mto Ahava, hapo nilitangaza kufunga, ili tujinyenyekeshe mbele za Mungu wetu na kumwomba kwa ajili ya kutujalia safari ya amani sisi na watoto wetu, pamoja na mali zetu zote. 228:22 Neh 2:9; Yer 41:16; Kum 31:17; 2Nya 15:2; 1Kor 9:15; 1Nya 28:9; Ezr 7:6-9; Za 33:18-19; Isa 3:10; Rum 8:28; 1Pet 3:12; Za 34:16; 2Nya 15:2Niliona aibu kumwomba mfalme askari na wapanda farasi wa kutulinda njiani kutokana na adui zetu, kwa sababu tulikwisha kumwambia mfalme, “Mkono wa neema wa Mungu wetu uko juu ya kila mmoja anayemtafuta, lakini hasira yake kubwa ni dhidi ya wote wamwachao.” 238:23 2Nya 33:13; Kum 4:29; Mdo 14:23; 1Nya 5:20; Isa 19:22; Yer 29:12-13Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hili, naye akajibu maombi yetu.

24Kisha niliwatenga viongozi wa makuhani kumi na wawili, pamoja na Sherebia, Hashabia na ndugu zao kumi, 258:25 Ezr 7:15-16nami nikawapimia fedha, dhahabu na vifaa ambavyo mfalme, washauri wake, maafisa wake na Israeli wote waliokuwepo walikuwa wamevitoa sadaka kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu. 26Niliwapimia talanta 6508:26 Talanta 650 za fedha ni sawa na tani 25. za fedha, vifaa vingine vya fedha vya uzito wa talanta mia moja,8:26 Talanta 100 za fedha ni sawa na tani 3.75. talanta mia moja za dhahabu, 27mabakuli ishirini ya dhahabu ya thamani ya darkoni elfu moja,8:27 Darkoni 1,000 ni sawa na kilo 8.5. na vyombo viwili vya shaba iliyosuguliwa, ya thamani kama dhahabu.

288:28 Kum 33:8; Law 21:6; 22:2-3; 2Nya 24:14; Hes 4:4; Isa 52:11; 1Nya 23:28Niliwaambia, “Ninyi pamoja na vyombo hivi ni wakfu kwa Bwana. Fedha na dhahabu ni sadaka ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu. 298:29 1Nya 26:20-26; Lk 12:38-39Vilindeni kwa uangalifu mpaka mtakapovipima ndani ya vyumba vya nyumba ya Bwana katika Yerusalemu mbele ya makuhani, viongozi na Walawi pamoja na wakuu wa jamaa za Israeli.” 30Ndipo makuhani na Walawi wakapokea fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu ambavyo vilipimwa na kupelekwa katika nyumba ya Mungu wetu mjini Yerusalemu.

318:31 Ay 5:19-24; Isa 41:10-14; Ezr 7:6-7, 28Tulianza safari kutoka Mto Ahava kwenda Yerusalemu kwenye siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza. Mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye njiani alitulinda dhidi ya adui na wanyangʼanyi. 328:32 Mwa 40:13; Neh 2:11; Isa 56:6; 14:1Kwa hiyo tuliwasili Yerusalemu ambapo tulipumzika kwa siku tatu.

338:33 Neh 3:3, 21-24Katika siku ya nne, ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tulipima fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu, tukakabidhi mikononi mwa kuhani Meremothi mwana wa Uria. Eleazari mwana wa Finehasi alikuwa pamoja naye, pia walikuwako Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui. 34Kila kitu kilihesabiwa kwa idadi na kupimwa kwa uzito, nao uzito wote uliandikwa wakati ule.

358:35 Law 1:3; 2Nya 29:21, 24; 30:24; Ezr 6:17Kisha mateka waliokuwa wamerudi kutoka utumwani wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mungu wa Israeli: mafahali kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, kondoo dume tisini na sita, wana-kondoo sabini na saba na mbuzi dume kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi. Hii yote ilikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa Bwana. 368:36 Ezr 7:21-24; Zek 8:1-23; Es 9:3Pia walikabidhi manaibu wa mfalme na watawala wa Ngʼambo ya Mto Frati maagizo ya mfalme, ambao baadaye walitoa msaada kwa watu na kwa nyumba ya Mungu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以斯拉記 8:1-36

歸回之人

1亞達薛西王年間,與我一起從巴比倫上到耶路撒冷之人的族長和家譜如下: 2非尼哈的子孫有革順以他瑪的子孫有但以理大衛的子孫有哈突3巴錄的後裔、示迦尼的子孫有撒迦利亞及一百五十名同族譜的男子; 4巴哈·摩押的子孫有西拉希雅的兒子以利約乃及二百名男子; 5薩土8·5 薩土」七十士譯本有此名字,希伯來文則無。的子孫有雅哈悉的兒子示迦尼及三百名男子; 6亞丁的子孫有約拿單的兒子以別及五十名男子; 7以攔的子孫有亞他利雅的兒子耶篩亞及七十名男子; 8示法提雅的子孫有米迦勒的兒子西巴第雅及八十名男子; 9約押的子孫有耶歇的兒子俄巴底亞及二百一十八名男子; 10巴尼8·10 巴尼」七十士譯本有此名字,希伯來文則無。的後裔、約細斐的子孫有示羅密及一百六十名男子; 11比拜的後裔有比拜的兒子撒迦利亞及二十八名男子; 12押甲的後裔有哈加坦的兒子約哈難及一百一十名男子; 13稍後歸回的亞多尼干的子孫有以利法列耶利示瑪雅及六十名男子; 14比革瓦伊的子孫有烏太撒布及七十名男子。

以斯拉為聖殿召集利未人

15我把他們召集在流向亞哈瓦的河邊,我們在那裡紮營三天。我察看民眾和祭司,發現他們當中沒有利未人。 16於是,我派人叫來首領以利以謝亞列示瑪雅以利拿單雅立以利拿單拿單撒迦利亞米書蘭及兩位教師約雅立以利拿單17我派他們去見迦西斐雅的首領易多,請他們告訴易多及其做殿役的親族帶一些人來我們上帝的殿裡事奉。 18我們的上帝施恩幫助我們,他們給我們帶來一位能幹的人示利比及其弟兄和兒子共十八人。示利比以色列的兒子利未的後裔抹利的子孫。 19他們還帶來哈沙比雅米拉利的子孫耶篩亞,以及哈沙比雅的弟兄和兒子共二十人。 20此外還有二百二十名殿役,他們都是被點名指派的。從前大衛和眾官員曾指派殿役服侍利未人。

以斯拉帶領百姓禁食

21然後,我在亞哈瓦河邊宣佈禁食,為要在我們的上帝面前謙卑下來,祈求祂保護我們、我們的兒女及財物一路平安。 22我羞於求王派步兵和騎兵沿途幫助我們禦敵,因為我們曾經告訴王:「我們的上帝會施恩幫助尋求祂的人,但會向背棄祂的人發烈怒。」 23因此,我們為這事禁食、尋求我們的上帝,祂應允了我們。

獻給聖殿的禮物

24我選出十二位祭司長:示利比哈沙比雅和他們的十個弟兄。 25王及其謀士和將領,以及所有在場的以色列人獻給我們上帝殿的金銀和器皿,我都秤了交給他們。 26我交給他們的有二十二噸銀子、三點四噸銀器、三點四噸金子、 27共重八公斤半的二十個金碗和兩件貴重如金子的上等精銅器皿。 28我對他們說:「你們和這些器皿是獻給耶和華的,金銀是自願獻給你們祖先的上帝耶和華的禮物。 29你們要好好保管,護送到耶路撒冷耶和華殿的庫房裡,要在祭司長、利未人和以色列的各族長面前過秤。」 30於是,祭司和利未人接過這些稱過的金銀和器皿,要帶去耶路撒冷我們上帝的殿裡。

返回耶路撒冷

31一月十二日,我們從亞哈瓦河邊出發上耶路撒冷。我們的上帝施恩幫助我們,救我們脫離仇敵和路上埋伏之人的攻擊。 32耶路撒冷後,我們休息了三天。 33第四天,我們在我們上帝的殿裡把金銀和器皿過秤,交給烏利亞的兒子米利末祭司。在場的還有非尼哈的兒子以利亞撒利未耶書亞的兒子約撒拔賓內的兒子挪亞底34每樣東西都被數過、稱過,其重量都被記錄下來。

35從流亡之地歸回的人又獻燔祭給以色列的上帝,為全體以色列人獻上十二頭公牛、九十六隻公綿羊和七十七隻綿羊羔,並獻上十二隻公山羊作贖罪祭。這些都是獻給耶和華的燔祭。 36他們將王的諭旨交給王的總督和幼發拉底河西的省長,眾官員都為民眾和上帝殿的工作提供幫助。