Ezra 3 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezra 3:1-13

Madhabahu Yajengwa Tena

13:1 Neh 7:73; Law 23:24Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja. 23:2 Zek 3:1; Ezr 2:2; Mt 1:12; Lk 3:27; Zek 6:11; Hag 2:2; Kut 20:24; Kum 12:5-6; Neh 12:1-8Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. 33:3 Kut 29:38-42; Hes 28:1-8; Dan 9:25; Ezr 4:4Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni. 43:4 Kut 23:16; Zek 14:16; Hes 29:12-38; Neh 8:14Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa. 53:5 Hes 28:3-11; Kol 2:16; Kut 29:38; Law 23:1-44; Hes 29:39Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana. 6Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.

Kujenga Upya Hekalu

73:7 1Nya 14:1; Isa 35:2; Ezr 6:3; 2Nya 2:10; Mdo 9:36; 12:20; Isa 60:13Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.

83:8 Zek 4:9; Hes 4:3; 1Nya 23:24-27Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana. 93:9 Ezr 2:40Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.

103:10 Zek 6:12; Ezr 6:3; 1Nya 15:27-28; 6:31; Hag 2:153:10 2Nya 5:13; 1Nya 6:31Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli. 113:11 1Nya 16:34; Za 138:8; Yos 6:5-10; Neh 12:24; 2Nya 7:3; Yer 33:11; Lk 1:50; Za 136:1; Kut 15:21Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi:

“Yeye ni mwema;

upendo wake kwa Israeli

wadumu milele.”

Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa. 123:12 Hag 2:3-9Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha. 133:13 Ay 33:26; Yer 48:33Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.

Swedish Contemporary Bible

Esra 3:1-13

Templet återuppbyggs

(3:1—6:22)

Folkets ledare bygger upp altaret

1När den sjunde månaden kom och israeliterna bodde i sina städer, samlades folket som en man i Jerusalem. 2Jeshua, Josadaks son, och hans bröder prästerna och Serubbabel, Shealtiels son, och hans bröder började då bygga upp Israels Guds altare igen, för att offra brännoffer där, enligt föreskrifterna i gudsmannen Moses lag. 3De byggde altaret på dess gamla plats, för de var rädda för folken i landet3:3 de var rädda för folken i landet – grundtextens innebörd är osäker., och man offrade brännoffer till Herren både morgon och kväll.

4De firade lövhyddefesten enligt föreskrifterna, med det bestämda antalet brännoffer för varje dag. 5Sedan offrade de det dagliga brännoffret och brännoffer för nymånadsfesten och Herrens andra helgade högtider, och alla de offer som frivilligt bars till Herren. 6Den första dagen i sjunde månaden började de offra brännoffer till Herren, trots att grunden till Herrens tempel ännu inte var lagd.

Tempelbygget påbörjas

7De betalade stenhuggare och snickare med pengar och folket från Sidon och Tyros med mat, dryck och olja, för att de sjövägen skulle föra cederträ från Libanon till Jafo, som kung Kyros av Persien hade gett dem tillstånd till.

8Andra året efter deras ankomst till Guds hus i Jerusalem, i andra månaden, påbörjades arbetet av Serubbabel, Shealtiels son, Jeshua, Josadaks son, och deras bröder präster och leviter och alla som kommit från fångenskapen till Jerusalem. De leviter som var tjugo år eller äldre tillsatte de som förmän för arbetet med Herrens hus. 9Jeshua, med sina söner och bröder, och Kadmiel och hans söner, dvs. Hodavjas släkt, åtog sig gemensamt ledningen för dem som arbetade på Guds hus, liksom Henadads söner och deras söner och bröder, leviterna.

10När byggnadsarbetarna lade grunden till Herrens tempel, intog prästerna sina platser, klädda i prästdräkter, med trumpeter, och leviterna, Asafs ättlingar, med cymbaler, för att prisa Herren på det sätt som Israels kung David befallt. 11De lovsjöng och prisade Herren:

”Han är god,

och hans nåd mot Israel varar för evigt.”

Hela folket jublade högt och prisade Gud för att grunden till Herrens hus hade blivit lagd. 12Men många av prästerna och leviterna och familjeöverhuvudena som var så gamla att de hade sett det förra templet3:12 Grundtexten är svårförståelig och översättningen osäker., grät högt när de såg grunden läggas till detta tempel, medan många andra jublade och ropade av glädje. 13Ingen kunde skilja mellan det stora glädjeropet och gråten, för folket ropade så högt att det kunde höras vida omkring.