Ezra 3 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezra 3:1-13

Madhabahu Yajengwa Tena

13:1 Neh 7:73; Law 23:24Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja. 23:2 Zek 3:1; Ezr 2:2; Mt 1:12; Lk 3:27; Zek 6:11; Hag 2:2; Kut 20:24; Kum 12:5-6; Neh 12:1-8Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu. 33:3 Kut 29:38-42; Hes 28:1-8; Dan 9:25; Ezr 4:4Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni. 43:4 Kut 23:16; Zek 14:16; Hes 29:12-38; Neh 8:14Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa. 53:5 Hes 28:3-11; Kol 2:16; Kut 29:38; Law 23:1-44; Hes 29:39Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana. 6Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.

Kujenga Upya Hekalu

73:7 1Nya 14:1; Isa 35:2; Ezr 6:3; 2Nya 2:10; Mdo 9:36; 12:20; Isa 60:13Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.

83:8 Zek 4:9; Hes 4:3; 1Nya 23:24-27Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana. 93:9 Ezr 2:40Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.

103:10 Zek 6:12; Ezr 6:3; 1Nya 15:27-28; 6:31; Hag 2:153:10 2Nya 5:13; 1Nya 6:31Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli. 113:11 1Nya 16:34; Za 138:8; Yos 6:5-10; Neh 12:24; 2Nya 7:3; Yer 33:11; Lk 1:50; Za 136:1; Kut 15:21Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi:

“Yeye ni mwema;

upendo wake kwa Israeli

wadumu milele.”

Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa. 123:12 Hag 2:3-9Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha. 133:13 Ay 33:26; Yer 48:33Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.

Bibelen på hverdagsdansk

Ezras Bog 3:1-13

Alteret genopbygges

1Da den syvende måned kom, og de hjemvendte havde slået sig ned i deres byer, drog de alle som én op til Jerusalem. 2Zerubbabel og hans slægt tog fat på at genopbygge brændofferalteret under vejledning af Jeshua, Jotzadaks søn, og hans præstekolleger. Først derefter kunne man ofre brændofre efter de forskrifter, som Guds tjener, Moses, havde givet dem. 3Selvom de var bange for de fremmede folk, som havde bosat sig dér i deres fravær, byggede de alteret på dets oprindelige sted og bragte morgen og aften de daglige brændofre til Herren. 4De fejrede løvhyttefesten efter forskrifterne i Toraen og bragte det antal brændofre, som er foreskrevet for hver enkelt dag i løbet af festen.

5Fra da af gennemførte de alle de foreskrevne ofringer: de daglige ofringer, ofrene ved nymånefesterne og ved de øvrige religiøse højtider. Desuden blev der bragt frivillige ofre. 6Den første dag i den syvende måned begyndte præsterne at bringe brændofre til Herren, selvom grundstenen til templet endnu ikke var lagt.

7Med fuldmagt fra kong Kyros ansatte de derpå stenhuggere og tømrere på løn, og de aftalte med folkene i Tyrus og Sidon, at de derfra skulle bringe cedertræ ad søvejen til Jafo og få madvarer, drikkevarer og olivenolie i bytte.

Genopbygningen af templet påbegyndes

8Selve genopbygningen af templet begyndte i den anden måned i det andet år efter ankomsten til Jerusalem. Arbejdsstyrken bestod af alle præster, levitter og øvrige indbyggere i Jerusalem under ledelse af Zerubbabel og Jeshua. De levitter der var 20 år eller derover, blev udpeget til formænd for arbejdsholdene. 9Det overordnede ansvar for selve genopbygningen af templet blev overdraget til den ledende præst, Jeshua, og hans sønner og brødre, og de fik hjælp af Kadmiel af Hodavjas slægt og Henadads sønner samt deres sønner og brødre, som alle var levitter.

10Da byggearbejderne havde lagt fundamentet til templet, iklædte præsterne sig deres dragter og blæste i trompeterne, og de levitter, som var af Asafs slægt, slog på deres bækkener i lovprisning til Herren, sådan som kong David havde foreskrevet. 11De lovsang Herren med ordene: „Herren er god! Hans trofasthed over for Israel varer til evig tid!” Da brød folket ud i et mægtigt jubelråb, og de priste Herren, fordi templets grundvold nu var lagt. 12Mange af de gamle blandt præsterne, levitterne og lederne—de der havde set Salomons storslåede tempel—græd højt, da de så fundamentet blive lagt til det nye tempel. Men andre rundt om var vilde af glæde. 13Man kunne ikke skelne jubelen fra gråden, og støjen kunne høres langt bort.