Ezekieli 7 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 7:1-27

Mwisho Umewadia

1Neno la Bwana likanijia kusema: 27:2 Amo 8:2-10; Ufu 20:8; Mao 4:18“Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa nchi ya Israeli: Mwisho! Mwisho umekuja juu ya pembe nne za nchi. 37:3 Eze 18:30; Mwa 6:13Sasa mwisho umekuja juu yenu nami nitamwaga hasira yangu dhidi yenu. Nitawahukumu sawasawa na matendo yenu na kuwalipiza kwa ajili ya desturi zenu zote za kuchukiza. 47:4 Yer 13:14; Eze 5:11; 23:49Sitawaonea huruma wala sitawarehemu, hakika nitalipiza kwa ajili ya matendo yenu na desturi zenu za machukizo miongoni mwenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

57:5 2Fal 21:12“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Maafa! Maafa ambayo hayajasikiwa yanakuja. 67:6 Eze 39:8Mwisho umewadia! Mwisho umewadia! Umejiinua wenyewe dhidi yenu. Umewadia! 77:7 Sef 1:14; Mal 3:2; 1Pet 4:17; Ay 18:20; Isa 2:12; Amo 5:18-20; Eze 12:23Maangamizi yamekuja juu yenu, ninyi mnaoishi katika nchi. Wakati umewadia, siku imekaribia, kuna hofu kuu ya ghafula, wala si furaha, juu ya milima. 87:8 Hos 5:10; Nah 1:6; Eze 36:19; 14:19; 20:8, 21; 9:8; Isa 42:25Ninakaribia kumwaga ghadhabu yangu juu yenu na kumaliza hasira yangu dhidi yenu, nitawahukumu sawasawa na matendo yenu na kuwalipiza kwa ajili ya desturi zenu zote za machukizo. 97:9 Yer 21:9; Isa 9:13; Eze 5:11; 22:31; Za 39:10Sitawaonea huruma wala sitawarehemu; nitawalipiza sawasawa na matendo yenu na desturi zenu za machukizo miongoni mwenu. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana ambaye huwapiga kwa mapigo.

107:10 Za 89:32; Isa 10:5“Siku imefika! Imewadia! Maangamizi yamezuka ghafula, fimbo imechanua majivuno yamechipua! 117:11 Yer 16:6; Sef 1:18; Isa 58:4; Za 55:9Jeuri imeinuka kuwa fimbo ya kuadhibu uovu, hakuna hata mmoja wa hao watu atakayeachwa, hata mmoja wa kundi lile, hakuna utajiri, hakuna chenye thamani. 127:12 Isa 5:13-14; Eze 30:3; Isa 24:2Wakati umewadia, siku imefika. Mnunuzi na asifurahi wala muuzaji asihuzunike, kwa maana ghadhabu iko juu ya kundi lote. 137:13 Law 25:24-25Muuzaji hatajipatia tena ardhi aliyoiuza wakati wote wawili wangali hai, kwa kuwa maono kuhusu kundi lote hayatatanguka. Kwa sababu ya dhambi zao, hakuna hata mmoja atakayeokoa maisha yake. 147:14 Ay 39:24; Yer 25:38Wajapopiga tarumbeta na kuweka kila kitu tayari, hakuna hata mmoja atakayekwenda vitani, kwa maana ghadhabu yangu iko juu ya kundi lote.

157:15 Kum 32:25; Yer 14:18; Mao 1:20; Eze 5:12; 33:27“Nje ni upanga, ndani ni tauni na njaa, wale walioko shambani watakufa kwa upanga, nao wale waliomo mjini njaa na tauni vitawala. 167:16 Mwa 8:8; Isa 59:11; 10:20; Ezr 9:15; Yer 9:19; 41:16; 42:17Wale wote watakaopona na kutoroka watakuwa milimani, wakiomboleza kama hua wa mabondeni, kila mmoja kwa sababu ya dhambi zake. 177:17 2Fal 19:26; Isa 13:7; Dan 6:5; Yer 43:7; Eze 21:7; 22:14Kila mkono utalegea na kila goti litakuwa dhaifu kama maji. 187:18 Isa 15:2-3; Amo 8:10; Za 55:5; Yer 6:26; 4:8; 49:3; 48:37Watavaa nguo ya gunia na kufunikwa na hofu. Nyuso zao zitafunikwa na aibu na nywele za vichwa vyao zitanyolewa. 197:19 Isa 42:25; Sef 1:18; Hos 4:5; Eze 3:20; Mit 11:4; Yoe 1:15; Eze 13:5; 14:3Watatupa fedha yao barabarani, nayo dhahabu yao itakuwa najisi. Fedha yao na dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana. Hawatashibisha njaa yao au kujaza matumbo yao kwa hiyo fedha wala dhahabu, kwa sababu imewaponza wajikwae dhambini. 207:20 Eze 5:11; 16:17; Yer 7:30; 10:3; Isa 2:20Walijivunia vito vyao vizuri na kuvitumia kufanya sanamu za machukizo na vinyago vya upotovu. Kwa hiyo nitavifanya vitu hivyo kuwa najisi kwao. 217:21 2Fal 24:13; Hes 14:3Nitavitia vyote mikononi mwa wageni kuwa nyara na kuwa vitu vilivyotekwa mikononi mwa watu waovu wa dunia, nao watavinajisi. 227:22 Yer 2:27; 19:13; Eze 39:23-24; Za 74:7-8Nitageuza uso wangu mbali nao, nao waovu wa dunia watapanajisi mahali pangu pa thamani, wanyangʼanyi watapaingia na kupanajisi.

237:23 2Fal 21:16; Isa 1:15; Za 10:8; Eze 11:6; 22:9; Mwa 6:11“Andaa minyororo, kwa sababu nchi imejaa umwagaji wa damu na mji umejaa udhalimu. 247:24 Mao 2:7; Eze 24:21; 28:7; 2Nya 7:20Nitaleta taifa ovu kuliko yote ili kumiliki nyumba zao, nitakomesha kiburi cha wenye nguvu na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi. 257:25 Yer 6:14; 8:11; Eze 13:10-16Hofu ya ghafula itakapokuja, watatafuta amani, lakini haitakuwepo. 267:26 Kum 29:21; 31:17; Yer 4:20; 18:18; Amo 8:11; Mik 3:6; Mal 2:7-9; Isa 47:11; 3:11; Eze 18:20; Za 109:19Maafa juu ya maafa yatakuja, tetesi ya mabaya juu ya tetesi ya mabaya. Watajitahidi kupata maono kutoka kwa nabii, mafundisho ya sheria toka kwa kuhani yatapotea, vivyo hivyo shauri kutoka kwa wazee. 27Mfalme ataomboleza, mwana wa mfalme atavikwa kukata tamaa, nayo mikono ya watu wa nchi itatetemeka. Nitawashughulikia sawasawa na matendo yao na kwa kanuni zao wenyewe nitawahukumu. Ndipo watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以西结书 7:1-27

以色列的结局近了

1耶和华对我说: 2“人子啊,主耶和华对以色列这样说,‘结局到了,以色列全境的结局到了! 3以色列,你的结局到了,我的怒气必倾倒在你身上,我必按你的行为审判你,照你的一切恶行报应你。 4我必不顾惜你,也不怜悯你,我必按你的恶行报应你。这样,你必知道我是耶和华。’”

5主耶和华说:“看啊,灾祸来了,一场空前的灾祸来了! 6结局到了,结局到了,你的结局到了! 7以色列境内的居民啊,恶运降临了!时候已到,日子已近,山上一片恐慌,欢乐荡然无存。 8我快要向你倾倒我的烈怒,发出我的怒气。我必按你的行为审判你,照你一切的恶行报应你。 9我必不顾惜你,也不怜悯你,我必按你的恶行报应你。这样,你就知道惩罚你的是我耶和华。

10“看啊,看啊,日子到了,大祸临头了!杖已经发芽,傲慢已经开花。 11暴行成了惩罚邪恶的杖,以色列人必没有一个能够存留,他们的财富和尊荣必不复存在。 12时候到了,日子近了,买主不要欢乐,卖主也不要忧愁,因为烈怒临到了所有的人。 13即使卖主活着,也无法赎回他所卖的,因为关乎每一个人的异象必然应验,他们因为犯罪一个也不能保存性命。

14“他们吹响了号角,做好了一切准备,却无人出战,因为我的烈怒临到了所有的人。 15城外有战祸,城内有饥荒瘟疫;城外的必丧身刀下,城内的必死于饥荒瘟疫。 16侥幸逃到山上的,都必像谷中哀鸣的鸽子,为自己的罪恶哭泣。 17他们必吓得两手发软,双腿战抖。 18他们必身披麻衣,战栗发抖。他们必剃光头发,满面羞愧。 19他们必把银子抛在街上,视金子为污秽之物。在耶和华发烈怒的日子,金银不能拯救他们,也不能填饱他们的肚腹,满足他们的心,因为金银使他们跌入罪恶中。 20他们以华美的饰物为骄傲,并用它制造丑恶可憎的神像,因此,我必使这一切变成他们眼中的污秽之物。 21我必使这一切成为外族人手中的猎物,恶人手中的战利品,被任意糟蹋。 22我必转脸不看他们,任由外族人亵渎我的殿,强盗必进入殿里大肆亵渎。

23“你要预备锁链,因为这地方充满了血腥的罪恶,城里充斥着暴行。 24我必让最凶恶的外族人侵占他们的房屋。我必挫掉强悍之人的傲气,使他们的圣所遭受亵渎。 25恐怖的日子来临了,他们想寻求平安,却得不到平安。 26灾祸接踵而至,噩耗不断传来。那时,他们必求问先知,但祭司的教导必消逝,长老们必无计可施。 27君王必悲哀,首领必惊恐,百姓的手都必颤抖。我必按他们的恶行对付他们,使他们受到应得的审判。这样,他们就知道我是耶和华。”