Ezekieli 5 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 5:1-17

Upanga Dhidi Ya Yerusalemu

15:1 Law 21:5; Isa 7:20; Eze 44:20; Hes 6:5; 2Sam 10:14“Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo. 25:2 Law 26:33; Yer 39:1-2; Zek 13:8; Yer 21:10; Eze 15:7; Yer 13:24; 9:16Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa. 35:3 Yer 40:6; 39:10; 2Fal 25:12; Za 74:11Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako. 45:4 Eze 10:7; 15:7Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.

55:5 Kum 4:6; Mao 1:1; Eze 16:14“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote. 65:6 Neh 9:17; Zek 7:11; Rum 1:25; Eze 16:16; 2Fal 17:15; Yer 11:10Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.

75:7 2Fal 21:9; 2Nya 33:9; Yer 2:10-11“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.

85:8 Yer 21:5; Zek 14:2; Yer 24:9; Eze 11:9; 15:7“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa. 95:9 Dan 9:12; Amo 3:2; Mt 24:21Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena. 105:10 Law 26:29; Mao 2:20; Yer 13:14; Zek 2:6; Za 44:11; Eze 12:14Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia. 115:11 Eze 7:20; 8:6; 2Nya 36:14; Eze 11:18-21; Yer 16:18; Ay 27:22; Hes 14:21; Law 15:2; 15:31; Mao 2:17Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu. 125:12 Ufu 6:8; Za 107:39; Eze 12:14; Zek 13:8; Eze 6:11-12; Yer 21:9; 13:24Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.

135:13 2Nya 12:7; Ay 20:23; Isa 1:24; Mao 4:11; Eze 21:17; 24:13; Hos 10:10“Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.

145:14 Mik 3:12; Isa 64:11; Neh 2:17; Za 74:3-10; Eze 22:4; Dan 9:16“Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe. 155:15 Kum 28:20; 1Fal 9:7; Yer 23:40; Eze 25:17; Mao 2:15; Isa 43:28; Yer 22:8-9Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema. 165:16 Law 26:26; Kum 32:24; Eze 14:21Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako. 175:17 Eze 38:23; Law 26:25; Eze 28:22Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以西结书 5:1-17

1“人子啊,去拿一把快刀当作剃头刀,剃掉你的头发和胡须,然后用天平把须发平均分成三份。 2围城期满后,你要把三分之一的须发焚烧在城中,三分之一在城的四周用刀砍断,三分之一要扬在风中吹散,因为我要拔刀追杀他们。 3你要从须发中取出几缕用衣服包上, 4再从中取出几根丢在火里焚烧,必有火从这里燃起,蔓延到整个以色列。”

5主耶和华说:“这就是耶路撒冷!我把她安置在万邦的中央,使列国环绕着她。 6但她违背我的典章,作恶甚于列邦,触犯我的律例甚于她周围的列国。他们拒绝我的典章,不遵守我的律例。” 7所以主耶和华说:“你们比周围的国家更混乱不堪,你们没有遵行我的律例,不谨守我的典章,连周围的国家都不如。” 8因此主耶和华这样说:“看啊,我要对付你们,我必在列国面前审判你们。 9因为你们一切的恶行,我必向你们施行空前绝后的惩罚。 10在你们中间,父亲要吃自己的儿子,儿子要吃自己的父亲。我必惩罚你们,把你们余下的人分散到各地各方。” 11主耶和华说:“因为你们用一切可憎的偶像和恶行玷污我的圣所,我凭我的永恒起誓,我必毫不留情地铲除你们。 12你们三分之一的人要死于饥荒瘟疫,三分之一的人要死于刀下,我必把其余的三分之一分散到各地各方,并拔刀追杀他们。 13这样,我对你们的怒气才会发完,我才会息怒。我把烈怒倾倒在你们身上的时候,你们就会知道我耶和华的话是出于痛恨不贞。 14我必使你们的家园在周围的列国中,在路人眼前成为荒凉之地,使你们饱受羞辱。 15当我在气愤和烈怒中严厉地审判你们时,你们在各国必受羞辱和嘲讽,成为警戒,下场可怕。这是我耶和华说的。 16我要向你们射出饥荒的毒箭,破坏和毁灭你们,并且使饥荒越来越严重,断绝你们的粮源。 17我必让饥荒和猛兽来侵害你们,夺走你们的儿女,使你们饱受瘟疫、暴行和刀剑之灾,这是我耶和华说的。”