Ezekieli 44 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 44:1-31

Mkuu, Walawi, Makuhani

144:1 Eze 43:1Ndipo yule mtu akanirudisha mpaka kwenye lango la nje la mahali Patakatifu, lile linaloelekea upande wa mashariki, nalo lilikuwa limefungwa. 244:2 Eze 43:4-5Bwana akaniambia, “Lango hili litabaki limefungwa. Haliruhusiwi kufunguliwa, wala hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kuingilia kwenye lango hili. Litabaki limefungwa kwa sababu Bwana, Mungu wa Israeli, ameingia kwa kupitia lango hili. 344:3 Zek 6:12; Kut 24:9-11; Eze 46:2-8Yeye aliye mkuu peke yake ndiye anayeweza kukaa penye njia ya hilo lango na kula chakula mbele za Bwana. Itampasa aingie kwa njia hiyo ya lango la ukumbini na kutokea njia iyo hiyo.”

444:4 Isa 6:4; Ufu 15:8; Eze 1:28; Dan 8:17; Eze 40:35; 10:4Kisha yule mtu akanileta kwa njia ya lango la kaskazini mpaka mbele ya Hekalu. Nikatazama nami nikauona utukufu wa Bwana ukilijaza Hekalu la Bwana, nami nikaanguka kifudifudi.

544:5 Eze 40:4; 43:10-11; 42:9Bwana akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa uangalifu, usikilize kwa bidii na uzingatie kila kitu ninachokuambia kuhusu masharti yote yanayohusu Hekalu la Bwana. Uwe mwangalifu kuhusu wale wanaoruhusiwa hekaluni na wale wasioruhusiwa kuingia mahali patakatifu. 644:6 Eze 3:19Iambie nyumba ya kuasi ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Matendo yenu ya machukizo yatosha, ee nyumba ya Israeli! 744:7 Law 26:4; Mwa 17:14; Kut 12:48; Mdo 21:28; Law 22:25Zaidi ya matendo yenu yote ya machukizo, mmewaleta wageni wasiotahiriwa mioyo na miili katika patakatifu pangu, mkilinajisi Hekalu langu, huku mkinitolea chakula, mafuta ya wanyama na damu, nanyi mmevunja Agano langu. 844:8 Law 22:2; Hes 18:7; 2Tim 4:1Badala ya kutimiza wajibu wenu kuhusiana na vitu vyangu vitakatifu, mmeweka watu wengine kuwa viongozi katika patakatifu pangu. 944:9 Yoe 3:17; Zek 14:21Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakuna mgeni asiyetahiriwa moyo na mwilini anayeruhusiwa kuingia patakatifu pangu, wala hata wageni wanaoishi miongoni mwa Waisraeli.

1044:10 Neh 9:34; 2Fal 23:8; Za 95:10; Hes 18:23“ ‘Walawi walioniacha wakati Waisraeli walipopotoka wakatoka kwangu na kutangatanga kwa kufuata sanamu zao, watachukua adhabu ya dhambi zao. 1144:11 2Nya 29:34; Hes 16:9; 1Nya 26:12-19; Hes 3:5-37Wanaweza wakatumika katika mahali patakatifu pangu, wakiwa na uangalizi wa malango ya Hekalu, nao watachinja sadaka za kuteketezwa na dhabihu kwa ajili ya watu na kusimama mbele ya watu ili kuwahudumia. 1244:12 2Fal 16:10-16; Yer 14:10; Za 106:26; Yer 18:15Lakini kwa sababu waliwatumikia watu mbele ya sanamu zao na kuifanya nyumba ya Israeli ianguke kwenye dhambi, kwa hiyo nimeapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba ni lazima wachukue matokeo ya dhambi yao, asema Bwana Mwenyezi. 1344:13 Eze 16:6; Hes 18:3; Hos 5:1Hawaruhusiwi kukaribia ili kunitumikia kama makuhani wala kukaribia chochote changu kilicho kitakatifu au sadaka iliyo takatifu kupita zote, bali watachukua aibu ya matendo yao ya kuchukiza. 1444:14 1Sam 2:36; 2Fal 23:9; 1Nya 23:28-32Lakini nitawaweka katika uangalizi wa Hekalu na kazi zote zile zinazotakiwa kufanyika ndani yake.

1544:15 Yer 33:18; Zek 3:7; Kum 10:8; 2Sam 8:17; Eze 7:2; Kum 29:13; Eze 40:46“ ‘Lakini makuhani, ambao ni Walawi na wazao wa Sadoki, ambao walitimiza wajibu wao kwa uaminifu katika patakatifu pangu wakati Waisraeli walipopotoka, watakaribia ili kutumika mbele zangu. Itawapasa wasimame mbele zangu ili kutoa dhabihu za mafuta ya wanyama na damu, asema Bwana Mwenyezi. 1644:16 Eze 41:22; 1Sam 2:35; Mal 2:7; Law 3:16-17; Hes 8:15; Law 17:5-6Wao peke yao ndio wenye ruhusa ya kuingia mahali patakatifu pangu. Wao peke yao ndio watakaokaribia meza yangu ili kuhudumu mbele zangu na kufanya utumishi wangu.

1744:17 Kut 39:27-28; Ufu 19:8“ ‘Watakapoingia kwenye malango ya ukumbi wa ndani, watavaa nguo za kitani safi, hawaruhusiwi kamwe kuvaa mavazi ya sufu wakati wanapokuwa wakihudumu kwenye malango ya ukumbi wa ndani wala ndani ya Hekalu. 1844:18 Kut 28:39; Isa 3:20; Law 16:4; Kut 28:42Watavaa vilemba vya kitani safi vichwani mwao na nguo za ndani za kitani safi viunoni mwao. Hawatavaa chochote kitakachowafanya kutoa jasho. 1944:19 Law 6:27; Eze 46:20; Kut 39:27-29; Law 6:10-11Watakapotoka ili kuingia katika ukumbi wa nje mahali watu walipo, watavua nguo walizokuwa wakihudumu nazo na wataziacha katika vyumba vitakatifu nao watavaa nguo nyingine, ili kwamba wasije wakaambukiza watu utakatifu kwa njia ya mavazi yao.

2044:20 Law 21:5; Hes 6:5; Isa 28:7“ ‘Hawatanyoa nywele za vichwa vyao wala kuziacha ziwe ndefu, bali watazipunguza. 2144:21 Law 10:9Kuhani yeyote asinywe mvinyo aingiapo katika ukumbi wa ndani. 2244:22 Law 21:7Wasioe wanawake wajane wala walioachika, inawapasa kuoa wanawake bikira wenye heshima wa Israeli au wajane wa makuhani. 2344:23 Eze 22:26; Hag 2:11-13; Mal 2:7; Mwa 7:2; Law 13:50; Yer 15:19Watawafundisha watu wangu tofauti kati ya vitu vitakatifu na vitu vya kawaida na kuwaonyesha jinsi ya kupambanua kati ya vitu najisi na vitu safi.

2444:24 1Tim 4:5; 1Nya 23:4; 2Nya 19:8; Kum 17:8-9; 19:17“ ‘Katika magombano yoyote, makuhani watatumika kama mahakimu na kuamua hilo jambo kufuatana na sheria zangu. Watazishika sheria zangu na maagizo yangu katika sikukuu zangu zote zilizoamriwa, nao watatakasa Sabato zangu.

2544:25 Law 21:1-4“ ‘Kuhani asijitie unajisi kwa kukaribia maiti, lakini, kama mtu aliyekufa alikuwa baba yake au mama yake, mwana au binti yake, ndugu yake au dada ambaye hajaolewa, basi aweza kujitia unajisi kwa hao. 2644:26 Law 21:1-4; Hes 6:10Baada ya kujitakasa, atakaa hali hiyo kwa muda wa siku saba. 2744:27 Hes 3:28; 6:11; Law 4:28Siku atakapoingia katika ukumbi wa ndani wa mahali patakatifu ili kuhudumu, atatoa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe, asema Bwana Mwenyezi.

2844:28 Kum 10:9; Yos 13:33; Hes 18:20; Kum 18:1-2“ ‘Mimi nitakuwa ndio urithi pekee walio nao makuhani katika Israeli. Msiwape wao milki, mimi nitakuwa milki yao. 2944:29 Law 27:21; Hes 18:9, 14; Yos 13:14; Law 6:16Wao watakula sadaka za nafaka, sadaka za dhambi na sadaka za hatia na kila kitu kitakachotolewa kwa Bwana katika Israeli kitakuwa chao. 3044:30 Hes 18:12-13; 2Nya 31:5; Hes 15:18-21; Neh 10:35-37; 2Nya 30:10Yote yaliyo bora ya malimbuko ya vitu vyote na matoleo yenu maalum vitakuwa vya makuhani. Inawapasa kuwapa malimbuko ya kwanza ya unga wenu ili kwamba baraka ipate kuwa katika nyumba zenu. 3144:31 Kut 22:31; Law 22:8; 11:39-40Makuhani hawaruhusiwi kula chochote, ikiwa ni ndege au mnyama, aliyekutwa akiwa amekufa au aliyeraruliwa na wanyama pori.

King James Version

Ezekiel 44:1-31

1Then he brought me back the way of the gate of the outward sanctuary which looketh toward the east; and it was shut. 2Then said the LORD unto me; This gate shall be shut, it shall not be opened, and no man shall enter in by it; because the LORD, the God of Israel, hath entered in by it, therefore it shall be shut. 3It is for the prince; the prince, he shall sit in it to eat bread before the LORD; he shall enter by the way of the porch of that gate, and shall go out by the way of the same.

4¶ Then brought he me the way of the north gate before the house: and I looked, and, behold, the glory of the LORD filled the house of the LORD: and I fell upon my face. 5And the LORD said unto me, Son of man, mark well, and behold with thine eyes, and hear with thine ears all that I say unto thee concerning all the ordinances of the house of the LORD, and all the laws thereof; and mark well the entering in of the house, with every going forth of the sanctuary.44.5 mark well: Heb. set thine heart44.5 mark well: Heb. set thine heart 6And thou shalt say to the rebellious, even to the house of Israel, Thus saith the Lord GOD; O ye house of Israel, let it suffice you of all your abominations, 7In that ye have brought into my sanctuary strangers, uncircumcised in heart, and uncircumcised in flesh, to be in my sanctuary, to pollute it, even my house, when ye offer my bread, the fat and the blood, and they have broken my covenant because of all your abominations.44.7 strangers: Heb. children of a stranger 8And ye have not kept the charge of mine holy things: but ye have set keepers of my charge in my sanctuary for yourselves.44.8 my charge: or, my ward, or, ordinance

9¶ Thus saith the Lord GOD; No stranger, uncircumcised in heart, nor uncircumcised in flesh, shall enter into my sanctuary, of any stranger that is among the children of Israel.

10And the Levites that are gone away far from me, when Israel went astray, which went astray away from me after their idols; they shall even bear their iniquity. 11Yet they shall be ministers in my sanctuary, having charge at the gates of the house, and ministering to the house: they shall slay the burnt offering and the sacrifice for the people, and they shall stand before them to minister unto them. 12Because they ministered unto them before their idols, and caused the house of Israel to fall into iniquity; therefore have I lifted up mine hand against them, saith the Lord GOD, and they shall bear their iniquity.44.12 caused…: Heb. were for a stumblingblock of iniquity unto, etc 13And they shall not come near unto me, to do the office of a priest unto me, nor to come near to any of my holy things, in the most holy place: but they shall bear their shame, and their abominations which they have committed. 14But I will make them keepers of the charge of the house, for all the service thereof, and for all that shall be done therein.

15¶ But the priests the Levites, the sons of Zadok, that kept the charge of my sanctuary when the children of Israel went astray from me, they shall come near to me to minister unto me, and they shall stand before me to offer unto me the fat and the blood, saith the Lord GOD: 16They shall enter into my sanctuary, and they shall come near to my table, to minister unto me, and they shall keep my charge.

17¶ And it shall come to pass, that when they enter in at the gates of the inner court, they shall be clothed with linen garments; and no wool shall come upon them, whiles they minister in the gates of the inner court, and within. 18They shall have linen bonnets upon their heads, and shall have linen breeches upon their loins; they shall not gird themselves with any thing that causeth sweat.44.18 with…: or, in sweating places: Heb. in, or, with sweat 19And when they go forth into the utter court, even into the utter court to the people, they shall put off their garments wherein they ministered, and lay them in the holy chambers, and they shall put on other garments; and they shall not sanctify the people with their garments. 20Neither shall they shave their heads, nor suffer their locks to grow long; they shall only poll their heads. 21Neither shall any priest drink wine, when they enter into the inner court. 22Neither shall they take for their wives a widow, nor her that is put away: but they shall take maidens of the seed of the house of Israel, or a widow that had a priest before.44.22 put…: Heb. thrust forth44.22 that had…: Heb. from a priest 23And they shall teach my people the difference between the holy and profane, and cause them to discern between the unclean and the clean. 24And in controversy they shall stand in judgment; and they shall judge it according to my judgments: and they shall keep my laws and my statutes in all mine assemblies; and they shall hallow my sabbaths. 25And they shall come at no dead person to defile themselves: but for father, or for mother, or for son, or for daughter, for brother, or for sister that hath had no husband, they may defile themselves. 26And after he is cleansed, they shall reckon unto him seven days. 27And in the day that he goeth into the sanctuary, unto the inner court, to minister in the sanctuary, he shall offer his sin offering, saith the Lord GOD. 28And it shall be unto them for an inheritance: I am their inheritance: and ye shall give them no possession in Israel: I am their possession. 29They shall eat the meat offering, and the sin offering, and the trespass offering; and every dedicated thing in Israel shall be theirs.44.29 dedicated: or, devoted 30And the first of all the firstfruits of all things, and every oblation of all, of every sort of your oblations, shall be the priest’s: ye shall also give unto the priest the first of your dough, that he may cause the blessing to rest in thine house.44.30 And the first: or, And the chief 31The priests shall not eat of any thing that is dead of itself, or torn, whether it be fowl or beast.