Ezekieli 38 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 38:1-23

Unabii Dhidi Ya Gogu

1Neno la Bwana likanijia kusema: 238:2 Mwa 10:2; Eze 27:13; Ufu 20:8; Eze 39:11“Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake 338:3 Eze 39:1na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali. 438:4 2Fal 19:28; Isa 43:17; Dan 11:40; Eze 23:12; 29:4; 39:2Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao. 538:5 Eze 27:10-14; Mwa 10:6Uajemi, Kushi38:5 Kushi ni Ethiopia. na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma, 638:6 Mwa 10:2-3; Eze 32:30pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.

738:7 Isa 8:9; 8:10; Yer 46:3, 4, 14; 51:12“ ‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe. 838:8 Isa 11:11; 24:22; Kum 4:30; Yer 23:6; Yoe 3:1; Eze 28:26Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama. 938:9 Isa 25:4; 28:2; Yer 4:13; Yoe 2:2; Ufu 20:8Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.

1038:10 Yer 17:10; Za 36:4; Mik 2:1“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya. 1138:11 Yer 49:31; Zek 2:4; Amu 18:7-27; Mwa 34:25Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo. 12Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.” 1338:13 Mwa 10:7; Eze 27:22; Isa 33:23; Yer 15:13; Mwa 25:3; Isa 10:6Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?” ’

1438:14 Law 25:18; Yer 16:15; Zek 2:5“Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo? 1538:15 Eze 39:2; Ufu 20:8; Eze 32:30Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu. 1638:16 Eze 38:9; 38:8; Kut 14:4; Eze 36:23; 39:21Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.

17“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao. 18Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi. 1938:19 Za 18:7; Hag 2:6, 21; Isa 29:23; Yoe 3:11; Law 10:3Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli. 2038:20 Za 76:8; Yer 4:24; Kut 15:14; Isa 42:15; Ay 14:18; Hos 4:3Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini. 2138:21 Isa 66:16; Kut 9:18; Ufu 16:21; Yer 25:31; Amu 7:22; 1Sam 14:20; Hag 2:22Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake. 2238:22 Yer 25:31; Eze 36:5; 14:19; Kut 9:18; Za 18:12; Ufu 16:21Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye. 2338:23 Eze 20:42; 36:23; 37:6Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’

Korean Living Bible

에스겔 38:1-23

곡에 대한 예언

1여호와께서 나에게 말씀하셨다.

2“사람의 아들아, 너는 마곡 땅에 있는 메섹과 두발의 통치자인 곡을 향하여 그를 책망하고 예언하라.

3너는 나 주 여호와가 그에게 이렇게 말한다고 일러 주어라. ‘메섹과 두발 왕 곡아, 내가 너를 대적한다.

4내가 너를 빙 돌려 네 턱에 갈고리를 꿰고 너의 전 군대, 곧 너의 말들과 완전 무장한 너의 기병들과 크고 작은 방패를 가지고 칼을 휘두르는 너의 대군과 함께 너를 끌어내고

5또 방패와 투구를 갖추고 그들과 함께 있는 38:5 원문에는 ‘바사와 구스와 붓과’페르시아, 에티오피아, 리비아,

6그리고 고멜과 그 모든 군대와 먼 북방의 벧 – 도갈마와 그 모든 군대, 곧 많은 백성을 너와 함께 끌어낼 것이다.

7“ ‘너는 준비하라. 너와 네 주변에 모인 모든 군대가 만반의 준비를 갖추고 너는 그들을 지휘하라.

8먼 훗날, 곧 마지막 때에 너는 명령을 받고 전쟁의 참화에서 복구된 한 땅을 침략하게 될 것이다. 그 백성은 여러 나라에서 모여들어 오랫동안 황폐했던 이스라엘 산에 이르러 지금은 모두 편안하게 살고 있다.

9너와 너의 군대와 너와 함께한 모든 나라의 군대가 폭풍처럼 공격하여 그 땅을 구름처럼 덮어 버릴 것이다.’ ”

10주 여호와께서 다시 곡에게 말씀하셨다. “그 날에 네 마음에 여러 가지 생각이 일어나서 네가 악한 꾀를 내어

11이렇게 말할 것이다. ‘내가 무방비 상태의 마을들을 침략하겠다. 성벽도 없고 문이나 빗장도 없이 마음 놓고 태평스럽게 살고 있는 백성들을 내가 쳐서

12그들을 약탈하겠다.’ 그러고서 네가 한때 폐허가 되었으나 지금은 사람이 살고 있는 땅과 여러 나라에서 모여들어 가축과 재산을 소유하고 세상 중앙에 살고 있는 백성을 치려고 할 때

13스바와 드단과 다시스의 상인들과 그 마을들이 너에게 ‘네가 약탈하러 왔느냐? 네가 네 군대를 모아 은과 금과 가축과 재물을 빼앗아 그 모든 약탈물을 가져가려고 하느냐?’ 하고 말할 것이다.”

14여호와께서 다시 나에게 말씀하셨다. “사람의 아들아, 그러므로 너는 곡에게 예언하라. 너는 그에게 나 주 여호와가 이렇게 말한다고 일러 주어라. ‘내 백성 이스라엘이 평안하게 살고 있을 때 네가 그것을 모르겠느냐?

15네가 먼 북쪽 땅에서 수많은 기병과 막강한 병력을 이끌고

16땅을 덮는 구름처럼 몰려와서 내 백성 이스라엘을 칠 것이다. 곡아, 앞으로 내가 너를 불러내어 내 땅을 치게 하겠다. 내가 너를 통해서 이방 민족들이 보는 가운데 나의 거룩함을 나타내어 그들이 나를 알 수 있게 할 것이다.

17“ ‘나 주 여호와가 말한다. 너는 옛날 내가 내 종 예언자들을 통해서 말하던 자가 아니냐? 그때 그들은 내가 너를 끌어다가 이스라엘 백성을 칠 것이라고 여러 해 동안 예언하였다.

18나 주 여호와가 말한다. 네가 이스라엘 땅을 치는 날에 내 분노가 치밀어 오를 것이다.’

19“내가 맹렬한 분노로 말하지만 그 날에 큰 지진이 이스라엘 땅에 일어나서

20바다의 고기와 공중의 새와 들짐승과 땅에 기어다니는 모든 생물들과 지면에 있는 모든 사람들이 내 앞에서 떨 것이며 모든 산이 무너지고 절벽이 떨어지며 모든 성벽이 땅에 무너져내릴 것이다.

21나 주 여호와가 말한다. 38:21 또는 ‘내가 내 모든 산 중에서 그를 칠 칼을 부르리니’내가 온갖 재앙을 일으켜 곡을 치겠다. 그 군대가 자기들끼리 서로 칼을 들어 칠 것이다.

22내가 또 질병과 피로 그를 심판할 것이며 폭우와 우박과 불과 유황을 그와 그 군대와 그의 많은 동맹국들에게 쏟을 것이다.

23이와 같이 내가 나의 위대함과 거룩함을 나타내어 많은 나라가 보는 데서 나를 알릴 것이니 그제서야 그들이 나를 여호와인 줄 알 것이다.”