Ezekieli 35 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 35:1-15

Unabii Dhidi Ya Edomu

1Neno la Bwana likanijia kusema: 235:2 Mwa 14:6; Kum 2:5; Yer 49:7-8; Amo 1:11“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake 335:3 Yer 6:12; Eze 34:10; 25:12-14; Oba 1:10na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika. 435:4 Yer 49:10; 44:2Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

535:5 Za 137:7; Eze 21:29; Za 63:10; Oba 1:13“ ‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake, 635:6 Isa 63:2-6; 34:3kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia. 735:7 Yer 46:19; 49:17Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda. 835:8 Eze 31:12Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote. 935:9 Isa 34:5-6; Yer 49:13-17; Oba 1:10Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

1035:10 Za 83:12; Eze 36:2-5“ ‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko, 1135:11 Eze 25:14; Oba 1:15; Mt 7:2; Isa 26:9; Za 9:16kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu. 1235:12 Yer 50:7; Za 9:16Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.” 1335:13 Dan 11:36; Yer 49:16Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia. 1435:14 Yer 51:48Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa. 1535:15 Mit 17:5; Eze 36:5; Oba 1:12; Mao 4:4-21; Yer 50:11-13; Isa 34:5-6; Eze 32:29Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’ ”

Japanese Contemporary Bible

エゼキエル書 35:1-15

35

エドムについての預言

1再び、次のような主からのことばがありました。 2「人の子よ、セイル山の方を向き、そこに住む人々に預言せよ。」 3神である主がこう語ります。

「わたしはおまえの敵となる。こぶしでおまえを打ち砕き、完全に滅ぼそう。 4-5おまえがわたしの民イスラエルを憎んでいるので、町々を破壊し、荒れはてさせる。その時、おまえはわたしが神であることを知る。わたしがイスラエルの罪をきびしく罰し、彼らが窮地に立たされていた時、おまえは彼らを虐殺した。」

6主は語ります。「わたしは生きている。そんなに血を流したいのなら、わたしがおまえを血に染めてやろう。今度はおまえが殺される番だ。 7わたしはセイル山の住民を一掃する。逃げ出そうとする者も、引き返して来る者も一人残らず殺す。 8山々を死体でいっぱいにする。丘も谷も川もみな、剣で殺された者で埋め尽くされる。 9おまえが活気を取り戻すことは決してない。永久に見捨てられ、町々も再建されることがない。その時、おまえたちはわたしが主であることを知る。

10おまえは、『イスラエルもユダも、われわれのものだ。占領してしまおう。神がいようがかまうものか』と言った。」 11それゆえ、神である主はこう言います。「わたしは生きている。おまえが怒りにまかせてわたしの民にした数々の行為に仕返しする。ねたみと憎しみに駆られた、おまえの行為のすべてを必ず罰する。わたしがおまえにすることを見て、イスラエルはわたしをほめたたえるようになる。 12その時、『神の民と言っても、力も何もあったものではない。われわれの格好のえじきだ』と悪口を言ったのを、わたしが聞いていたことをおまえは知る。 13おまえは主に対して不遜なことばを吐いた。それをみな、わたしは聞いたのだ。 14わたしがおまえの地を荒廃させる時、すべての国々は喜ぶだろう。 15おまえはイスラエルの恐ろしい破滅を見て喜んだ。今わたしは、おまえの破滅を喜ぼう。ああ、セイル山の住民よ、エドムに住むすべての者よ。おまえたちは一掃されるのだ。その時、おまえたちはわたしが主であることを知る。