Ezekieli 33 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 33:1-33

Wajibu Wa Ezekieli Kuwa Mlinzi Kwa Watu Wake

1Neno la Bwana likanijia kusema: 233:2 Law 26:25; Yer 12:12; Isa 14:16; 21:6-9; Yer 51:12“Mwanadamu, sema na watu wako uwaambie, ‘Nitakapoleta upanga dhidi ya nchi, nao watu wa nchi wakamchagua mmoja wa watu wao na kumfanya awe mlinzi wao, 333:3 Hes 10:7; Hos 5:8; Kut 20:18naye auonapo upanga unakuja dhidi ya nchi na kupiga tarumbeta kuonya watu, 433:4 2Nya 25:16; Mdo 18:6; Eze 18:13; Law 20:9; Yer 6:17kama mtu yeyote asikiapo sauti ya tarumbeta hakukubali kuonywa, basi upanga ujapo na kuutoa uhai wake, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe. 533:5 Law 20:9; Kut 9:21Kwa kuwa alisikia sauti ya tarumbeta lakini hakukubali maonyo, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe. Kama angekubali maonyo, angelijiokoa mwenyewe. 633:6 Isa 56:10-11; Eze 3:18Lakini kama mlinzi akiona upanga unakuja na asipige tarumbeta kuonya watu na upanga ukija na kutoa uhai wa mmoja wao, yule mtu ataondolewa kwa sababu ya dhambi yake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwa mlinzi huyo.’

733:7 Isa 52:8; Yer 26:5“Mwanadamu, nimekufanya wewe kuwa mlinzi kwa ajili ya nyumba ya Israeli, kwa hiyo sikia neno nisemalo na uwape maonyo kutoka kwangu. 833:8 Eze 33:14; Isa 3:11; Eze 18:14Nimwambiapo mtu mwovu, ‘Ewe mtu mwovu, hakika utakufa,’ nawe hukusema neno la kumwonya ili atoke katika njia zake, yule mtu mwovu atakufa kwa ajili ya dhambi yake, mimi nitaitaka damu yake mkononi mwako. 933:9 Eze 3:17-19; Mdo 13:46; Lk 12:4; Za 7:12Lakini kama utamwonya huyo mtu mwovu aache njia zake mbaya naye hafanyi hivyo, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, lakini utakuwa umejiokoa mwenyewe.

1033:10 Law 26:16; Eze 24:23; 4:17“Mwanadamu, sema na nyumba ya Israeli uwaambie, ‘Hili ndilo mnalosema: “Makosa yetu na dhambi zetu zimetulemea, nasi tunadhoofika kwa sababu ya hayo. Tutawezaje basi kuishi?” ’ 1133:11 2Sam 14:14; Mao 3:33; 2Pet 3:9; Yoe 2:12; 1Tim 2:4; 2Nya 30:9; Yer 3:12; Isa 19:22; Yer 44:7-8Waambie, ‘Hakika kama mimi niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, sifurahii kifo cha watu waovu, bali kwamba wageuke kutoka njia zao mbaya wapate kuishi. Geukeni! Geukeni kutoka njia zenu mbaya! Kwa nini mkafe, ee nyumba ya Israeli?’

1233:12 2Nya 7:14; Eze 18:21; 3:20“Kwa hiyo, mwanadamu, waambie watu wako, ‘Haki ya mtu mwenye haki haitamwokoa wakati anapoacha kutii, wala uovu wa mtu mwovu hautamsababisha yeye kuanguka anapotubu na kuacha uovu. Mtu mwenye haki, kama akitenda dhambi, hataishi kwa sababu ya uadilifu wake wa awali.’ 1333:13 Eze 18:23; Ebr 10:38; Lk 18:9; 2Pet 2:20-21Kama nikimwambia mtu mwenye haki kwamba hakika utaishi, lakini akategemea hiyo haki yake na kutenda uovu, hakuna tendo lolote la haki alilotenda litakalokumbukwa, atakufa kwa ajili ya uovu alioutenda. 1433:14 Yer 22:3; Eze 18:27Nami kama nikimwambia mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ kisha akageuka kutoka dhambi yake na kufanya lile lililo haki na sawa, 1533:15 Kut 22:1-4; Law 6:2-5; Lk 19:8; Isa 55:7; Yer 18:7-8kama akirudisha kile alichochukua rehani kwa ajili ya deni, akarudisha alichoiba na kufuata amri zile ziletazo uzima, wala hafanyi uovu, hakika ataishi, hatakufa. 1633:16 Isa 43:25; Eze 18:22-26; Yer 50:20Hakuna dhambi yoyote aliyoitenda itakayokumbukwa juu yake. Ametenda lile lililo haki na sawa, hakika ataishi.

1733:17 Eze 33:20; 18:25-29“Lakini watu wako wanasema, ‘Njia ya Bwana si sawa.’ Lakini ni njia zao ambazo si sawa. 1833:18 Eze 3:20; 18:26; Yer 18:10Kama mtu mwenye haki akigeuka kutoka uadilifu wake na kufanya uovu, atakufa kwa ajili ya huo uovu. 1933:19 Eze 33:14-15Naye mtu mwovu kama akigeuka kutoka uovu wake na kufanya lile lililo haki na sawa, kwa kufanya hivyo ataishi. 2033:20 Ay 34:11; Eze 33:17; 18:25-29Lakini, ee nyumba ya Israeli, unasema, ‘Njia ya Bwana si sawa.’ Lakini nitamhukumu kila mmoja wenu sawasawa na njia zake mwenyewe.”

Anguko La Yerusalemu Laelezewa

2133:21 Eze 24:26; 2Fal 25:4, 10; Yer 52:4-7; Eze 32:1Mwaka wa kumi na mbili wa uhamisho wetu, mwezi wa kumi, siku ya tano, mtu aliyekuwa ametoroka kutoka Yerusalemu akanijia na kusema, “Mji wa Yerusalemu umeanguka!” 2233:22 Eze 3:26-27; 24:27; Lk 1:64; Eze 29:21Basi jioni kabla mtu huyo hajaja, mkono wa Bwana, ulikuwa juu yangu, naye alifungua kinywa changu kabla ya mtu yule aliyenijia asubuhi hajafika. Basi kinywa changu kilifunguliwa na sikuweza tena kunyamaza.

23Ndipo neno la Bwana likanijia kusema: 2433:24 Eze 36:4; Isa 51:2; Lk 3:8; Mik 3:11; Mdo 7:5; Yer 40:7; Eze 11:15“Mwanadamu, watu wanaoishi katika magofu hayo katika nchi ya Israeli wanasema hivi, ‘Abrahamu alikuwa mtu mmoja tu, hata hivyo akaimiliki nchi. Lakini sisi ni wengi, hakika tumepewa nchi kuwa milki yetu.’ 2533:25 Mwa 9:4; Kum 12:16; Yer 7:9-10; Eze 22:6, 27; Yer 7:21Kwa hiyo waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa kuwa mnakula nyama pamoja na damu na kuinulia sanamu zenu macho na kumwaga damu, je, mtaimiliki nchi? 2633:26 Yer 41:7; Eze 22:11Mnategemea panga zenu, mnafanya mambo ya machukizo na kila mmoja wenu humtia unajisi mke wa jirani yake. Je, mtaimiliki nchi?’

2733:27 1Sam 13:6; Isa 2:19; Amu 6:2; Yer 42:22; Eze 7:15; 14:21“Waambie hivi: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Hakika kama niishivyo, wale waliobaki katika magofu wataanguka kwa upanga, wale walio nje mashambani nitawatoa wararuliwe na wanyama pori, nao wale walio katika ngome na kwenye mapango watakufa kwa tauni. 2833:28 Isa 41:15; Mwa 6:7; Yer 9:10Nitaifanya nchi kuwa ukiwa na utupu na kiburi cha nguvu zake zitafikia mwisho, nayo milima ya Israeli itakuwa ukiwa ili mtu yeyote asipite huko. 2933:29 Law 26:34; Yer 18:16; 44:22; Eze 36:4; Mik 7:13Kisha watajua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapokuwa nimeifanya nchi kuwa ukiwa na utupu kwa sababu ya mambo yote ya machukizo waliyotenda.’

3033:30 Isa 29:13“Kwa habari yako wewe, mwanadamu, watu wako wanaongea habari zako wakiwa karibu na kuta na kwenye milango ya nyumba, wakiambiana kila mmoja na mwenzake, ‘Njooni msikie ujumbe ule utokao kwa Bwana.’ 3133:31 Eze 8:1; Isa 33:15; Mt 13:22; Za 119:36; 78:36-37; Isa 29:13; Yer 3:10Watu wangu wanakujia, kama wafanyavyo, nao wanaketi mbele yako kama watu wangu na kusikiliza maneno yako, lakini hawayatendi. Kwa maana udanganyifu u katika midomo yao, lakini mioyo yao ina tamaa ya faida isiyo halali. 3233:32 Mk 6:20; Yak 1:22Naam, mbele yao umekuwa tu kama yeye aimbaye nyimbo za mapenzi kwa sauti nzuri za kuvutia na kupiga vyombo kwa ustadi, kwa kuwa wanasikia maneno yako lakini hawayatendi.

3333:33 1Sam 3:20; Yer 28:9; Eze 2:5“Wakati mambo haya yote yatakapotimia, kwa kuwa hakika yatatokea, ndipo watakapojua kwamba nabii amekuwepo miongoni mwao.”

New Russian Translation

Иезекииль 33:1-33

Иезекииль – страж Израиля

1Было ко мне слово Господа:

2– Сын человеческий, поговори с соплеменниками и скажи им: «Если Я наведу на страну меч, а жители той страны изберут у себя человека, поставят его своим стражем, 3и он увидит, что на страну идет меч, и затрубит в рог, чтобы предупредить народ, 4то тот, кто услышит рог, но не остережется, и меч, придя, лишит его жизни, сам будет повинен в своей гибели. 5Раз он услышал рог и не остерегся, он сам виноват в своей гибели. Если бы он остерегся, то остался бы жив. 6Но если страж увидит, что идет меч, и не затрубит в рог, чтобы предупредить народ, и меч придет и лишит жизни кого-то из них, то этот человек будет взят за свой грех, а стража за эту гибель Я призову к ответу».

7Сын человеческий, Я поставил тебя стражем для дома Израиля. Слушай же Мое слово и передавай им Мои предостережения. 8Если Я скажу злодею: «Злой человек, ты непременно умрешь», а ты не будешь говорить, чтобы отвести его от его пути, то злодей умрет за свой грех33:8 Или: «во грехе»; также в ст. 9., а за его гибель Я призову к ответу тебя. 9Но если ты предостерегал злодея, чтобы он оставил свой путь, а он этого не сделал, то он умрет за свой грех, а ты спасешь свою душу.

10Сын человеческий, скажи дому Израиля: «Вы говорите: „Наши преступления и грехи гнетут нас. Мы угасаем из-за них. Как нам выжить?“» 11Скажи им: «Верно, как и то, что Я живу, – возвещает Владыка Господь, – Я хочу не смерти грешников, но того, чтобы они оставили свои пути и жили. Обратитесь! Оставьте свои неправедные пути! Дом Израиля, зачем вам умирать?»

12Итак, сын человеческий, скажи соплеменникам: «Праведность не спасет праведника, если тот согрешит, и беззаконие злодея не погубит его, если он отвернется от него. Также если согрешит праведник, то он не сможет остаться в живых ради его былой праведности». 13Если Я скажу праведнику, что он непременно будет жить, а он понадеется на свою праведность и сделает зло, то ни одно из праведных дел, которые он совершил, не вспомнится; он умрет за то зло, которое сделал. 14А если Я скажу злодею: «Ты непременно умрешь», а он оставит грех и станет поступать справедливо и праведно: 15отдаст обратно то, что взял в залог за долги, вернет украденное, будет исполнять установления, которые дают жизнь, и не будет делать зла, то он непременно будет жить; он не умрет. 16Ни один из совершенных им грехов не будет ему припомнен. Он поступает справедливо и праведно: он непременно будет жить.

17А твои соплеменники говорят: «Путь Господа несправедлив». Нет, это их пути несправедливы. 18Если праведник оставит праведность и примется делать зло, то он за это и умрет. 19А если злодей оставит злодейство и станет делать то, что справедливо и праведно, то, поступая так, он будет жить. 20А вы говорите: «Путь Господа несправедлив». Я буду судить вас, дом Израиля, каждого по его поступкам.

Падение Иерусалима

21В двенадцатом году нашего плена, в пятый день десятого месяца33:21 8 января 585 г. до н. э. ко мне пришел человек, который спасся из Иерусалима, и сказал: «Город пал!» 22А вечером, накануне того дня, когда пришел беженец, рука Господа была на мне, и Он открыл мои уста, прежде чем беженец утром пришел ко мне. Он открыл мои уста, и я уже не молчал.

23И было ко мне слово Господа:

24– Сын человеческий, жители этих развалин, что в земле Израиля, говорят: «Авраам был совсем один и владел этой землей, а нас много. Конечно же, эта земля отдана нам во владение». 25Поэтому скажи им: «Так говорит Владыка Господь: Вы едите мясо с кровью, поклоняетесь идолам и проливаете чужую кровь – вам ли владеть этой землей? 26Вы полагаетесь на меч, делаете мерзости, и один оскверняет жену другого. Вам ли владеть этой землей?»

27Скажи им вот что: «Так говорит Владыка Господь: Верно как и то, что Я живу: оставшиеся в развалинах падут от меча; тех, кто находится в открытом поле, Я отдам на съедение диким зверям; а те, кто сидит в укреплениях и в пещерах, погибнут от мора. 28Я превращу эту землю в мертвую пустыню, ее гордая мощь исчезнет, и горы Израиля станут такими дикими, что никто не будет по ним проходить. 29Они узнают, что Я – Господь, когда Я превращу эту землю в мертвую пустыню за все те мерзости, которые они сделали».

30А о тебе, сын человеческий, твои соплеменники разговаривают у стен и дверей домов, говоря друг другу: «Идем, послушаем весть от Господа». 31Мой народ ходит к тебе, как обычно, и садится пред тобой слушать твои слова, но не исполняет их. На устах у них – лесть, а сердца тянутся к нечестной наживе. 32Истинно говорю, ты для них что певец, поющий о любви красивым голосом и хорошо играющий: они слышат твои слова, но не исполняют их.

33Когда все это сбудется, – а сбудется это непременно, – тогда они и узнают, что среди них был пророк.