Ezekieli 32 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 32:1-32

Maombolezo Kwa Ajili Ya Farao

132:1 Eze 31:1; 33:21Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema: 232:2 2Sam 1:17; 2Nya 35:25; 2Fal 24:1; Nah 2:11-13; Ay 41:31; Eze 29:3; Ay 3:8; Eze 34:18; 2Sam 3:33“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie:

“ ‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa,

wewe ni kama joka kubwa baharini,

unayevuruga maji kwa miguu yako

na kuchafua vijito.

332:3 Eze 12:13; Hab 1:15“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu

nitautupa wavu wangu juu yako,

nao watakukokota katika wavu wangu.

432:4 Isa 18:6; 1Sam 17:44-46; Eze 39:4-5; 31:12-13Nitakutupa nchi kavu

na kukuvurumisha uwanjani.

Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako

na wanyama wote wa nchi

watajishibisha nyama yako.

532:5 Eze 31:12Nitatawanya nyama yako juu ya milima

na kujaza mabonde kwa mabaki yako.

632:6 Isa 34:3; Eze 29:5Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka

njia yote hadi milimani,

nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.

732:7 Yoe 3:15; Mt 24:29; Ufu 6:12; Isa 34:4; Eze 30:3; Yoe 2:2Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu

na kuzitia nyota zake giza;

nitalifunika jua kwa wingu,

nao mwezi hautatoa nuru yake.

832:8 Za 102:26; Ay 9:7; Yer 4:23; Yoe 2:10Mianga yote itoayo nuru angani

nitaitia giza juu yako;

nitaleta giza juu ya nchi yako,

asema Bwana Mwenyezi.

9Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi

nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa,

nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi

ambazo haujapata kuzijua.

1032:10 Yer 46:10; Eze 26:16; Ufu 18:9-10; Isa 30:32; Eze 27:35; 30:9Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie,

wafalme wao watatetemeka

kwa hofu kwa ajili yako

nitakapotikisa upanga wangu mbele yao.

Siku ya anguko lako

kila mmoja wao atatetemeka

kila dakika kwa ajili ya maisha yake.

1132:11 Isa 19:4; Yer 46:26; Eze 21:19; 46:13; 29:19“ ‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Upanga wa mfalme wa Babeli

utakuja dhidi yako.

1232:12 Eze 28:7; 31:11-12Nitafanya makundi yako ya wajeuri kuanguka

kwa panga za watu mashujaa,

taifa katili kuliko mataifa yote.

Watakivunjavunja kiburi cha Misri,

nayo makundi yake yote

ya wajeuri yatashindwa.

1332:13 Eze 29:8-11Nitaangamiza mifugo yake yote

wanaojilisha kando ya maji mengi,

hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu

wala kwato za mnyama

hazitayachafua tena.

14Kisha nitafanya maji yake yatulie

na kufanya vijito vyake

vitiririke kama mafuta,

asema Bwana Mwenyezi.

1532:15 Kut 7:5; Za 107:33-34; Kut 14:4; 18Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa

na kuiondolea nchi kila kitu

kilichomo ndani yake,

nitakapowapiga wote waishio humo,

ndipo watakapojua kuwa

Mimi ndimi Bwana.’

1632:16 Mwa 50:10; 2Sam 1:17; Eze 26:17; 19:1“Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote ya wajeuri wataliimba, asema Bwana Mwenyezi.”

17Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema: 1832:18 Yer 1:10; Mik 1:8; Eze 26:20; 31:14-16; 32:1“Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya wajeuri wa Misri na uwatupe kuzimu yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao washukao shimoni. 1932:19 Eze 28:10; 31:18Je, ninyi mnamzidi nani kwa uzuri? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa! 2032:20 Za 28:3; Eze 31:17-18Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa, mwache aburutwe mbali pamoja na hao wajeuri wake wote. 2132:21 Isa 14:9; Eze 28:10Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’

2232:22 Eze 32:24, 26, 29, 30“Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga. 2332:23 Isa 14:15; Nah 1:14Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.

2432:24 Mwa 10:22; Yer 49:37; Ay 28:13; Eze 26:20“Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni. 2532:25 Eze 28:10; 28:10Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.

2632:26 Mwa 10:2; Eze 27:13“Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao ya wajeuri wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai. 27Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai.

28“Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.

2932:29 Za 137:7; Eze 25:12-14; 35:15; Yer 49:7; Isa 34:5-15“Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale washukao shimoni.

3032:30 Isa 14:31; Yer 25:26; Mwa 10:15; Eze 38:6; Yer 25:22; Eze 28:10; 28:8“Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale washukao chini shimoni.

3132:31 Eze 14:22; 31:16“Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote ya wajeuri, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi. 3232:32 Yer 44:30; Ay 3:14Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.”

Nueva Versión Internacional

Ezequiel 32:1-32

Lamento por el faraón

1El día primero del mes duodécimo del año duodécimo, el Señor me dirigió la palabra: 2«Hijo de hombre, entona este lamento dedicado al faraón, rey de Egipto:

»“Pareces un león entre las naciones;

eres semejante a un monstruo marino

chapoteando en el río;

con tus patas enturbias el agua

y revuelves sus corrientes.

3»”Así dice el Señor y Dios:

»” Aunque estés entre numerosos pueblos,

tenderé sobre ti mi red

y te atraparé con ella.

4Te arrastraré por tierra

y en pleno campo te dejaré tendido.

Dejaré que sobre ti se posen

todas las aves del cielo.

Dejaré que con tu carne

se sacien todas las bestias de la tierra.

5Desparramaré tu carne por los montes

y con tu carroña llenaré los valles.

6Con tu sangre empaparé la tierra

hasta la cima de las montañas;

con tu sangre llenaré los canales de los ríos.

7Cuando te hayas consumido,

haré que el cielo se oscurezca

y se apaguen las estrellas;

cubriré el sol con una nube,

y no brillará más la luna.

8Todos los astros brillantes de los cielos,

los oscureceré sobre ti;

traeré oscuridad sobre la tierra,

afirma el Señor y Dios.

9Yo turbaré el corazón de muchos pueblos

cuando provoque tu destrucción,

aún entre las naciones que no conocías.

10Haré que por ti muchos pueblos queden consternados.

Cuando yo esgrima mi espada delante de ellos,

sus reyes se estremecerán.

En el día de tu caída,

en todo momento temblarán de miedo

por temor a perder la vida.

11»”Así dice el Señor y Dios:

»”La espada del rey de Babilonia

vendrá contra ti.

12Haré que tus multitudes caigan a filo de espada,

empuñada por los guerreros

más crueles entre las naciones.

Ellos arrasarán la soberbia de Egipto

y toda su multitud será derrotada.

13Voy a destruir todo el ganado

que pasta junto a las aguas abundantes;

nunca más serán enturbiadas

por hombres ni animales.

14Entonces dejaré que las aguas se asienten

y que corran tranquilas, como el aceite,

afirma el Señor y Dios.

15Cuando deje en ruinas a Egipto,

la despoje de todo lo que hay en su tierra

y hiera a todos los que la habitan,

entonces sabrán que yo soy el Señor ”.

16»Este es el lamento que las ciudades de las naciones entonarán sobre Egipto y toda su multitud, afirma el Señor y Dios».

17En el día quince del mes duodécimo del año duodécimo, el Señor me dirigió la palabra: 18«Hijo de hombre, entona un lamento sobre las multitudes de Egipto y, junto con las ciudades de las naciones más poderosas, hazlas descender con los que bajan a la fosa, a las regiones más profundas. 19Pregúntales: “¿Se creen acaso más privilegiados que otros? ¡Pues bajen y tiéndanse entre los paganos!”.32:19 paganos. Lit. incircuncisos. 20Y caerán entre los que murieron a filo de espada. Ya tienen la espada en la mano: ¡que se arrastre a Egipto y a sus multitudes! 21Allí en los dominios de la muerte,32:21 los dominios de la muerte. Lit. el Seol. los guerreros más fuertes y valientes hablarán de Egipto y de sus aliados. Y dirán: “¡Ya han descendido! ¡Yacen tendidos entre los paganos que murieron a filo de espada!”.

22»Allí está Asiria, con toda su multitud en torno a su sepulcro. Todos ellos murieron a filo de espada. 23Todos los que sembraban el terror en la tierra de los vivientes yacen muertos, víctimas de la espada. Ahora están sepultados en lo más profundo de la fosa, tendidos alrededor de su tumba.

24»Allí está Elam, con toda su multitud en torno a su sepulcro. Todos ellos murieron a filo de espada. Todos los que sembraban el terror en la tierra de los vivientes bajaron como paganos a lo más profundo de la fosa. Yacen tendidos sin honor entre los que descendieron a la fosa. 25A Elam le han preparado una cama en medio de los muertos, entre los paganos que murieron a filo de espada y que ahora rodean su tumba. Ellos sembraron el terror en la tierra de los vivientes, pero ahora yacen tendidos sin honor entre los que descendieron a la fosa. Allí quedaron, entre gente que murió asesinada.

26»Allí están Mésec y Tubal, con toda su multitud en torno a su sepulcro. Todos ellos son paganos, muertos a filo de espada porque sembraron el terror en la tierra de los vivientes. 27No yacen con los héroes caídos de entre los paganos, que bajaron a los dominios de la muerte con sus armas de guerra y que tienen sus espadas bajo la cabeza. El castigo de sus pecados cayó sobre sus huesos, porque estos héroes sembraron el terror en la tierra de los vivientes.

28»Ahí estarás tú, faraón, en medio de los paganos, abatido y sepultado junto con los que murieron a filo de espada.

29»Allí está Edom, con sus reyes y príncipes. A pesar de todo su poder, también ellos yacen tendidos junto a los que murieron a filo de espada. Yacen entre los paganos, con los que descendieron a la fosa.

30»Allí están todos los príncipes del norte, y todos los de Sidón. A pesar del terror que sembraron con su poderío, también ellos bajaron, envueltos en deshonra, con los que murieron a filo de espada. Son paganos, y ahora yacen tendidos entre los que murieron a filo de espada, en medio de los que descendieron a la fosa.

31»El faraón los verá y se consolará de la muerte de toda su gente, pues él y todo su ejército morirán a filo de espada, afirma el Señor y Dios. 32Aunque yo hice que el faraón sembrara el terror en la tierra de los vivientes, él y todo su ejército serán sepultados entre los paganos, con los que murieron a filo de espada, afirma el Señor y Dios».