Ezekieli 24 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 24:1-27

Chungu Cha Kupikia

124:1 Eze 8:1; 26:1; 29:17Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la Bwana likanijia kusema: 224:2 2Fal 25:1; Yer 52:4; Isa 30:8; Hab 2:2; Yer 39:1“Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo. 324:3 Za 78:2; Eze 17:2; 11:3-6; 11:3Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Teleka sufuria jikoni; iteleke

na umimine maji ndani yake,

424:4 Eze 11:7Weka vipande vya nyama ndani yake,

vipande vyote vizuri,

vya paja na vya bega.

Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri;

524:5 Isa 34:12; Yer 52:10, 24-27; Mik 3:2-3chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo.

Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa;

chochea mpaka ichemke

na uitokose hiyo mifupa ndani yake.

624:6 Eze 22:2; Ay 6:27; Nah 3:10; Oba 1:11; Eze 16:23; Yoe 3:3; Eze 11:11“ ‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ole wa mji umwagao damu,

ole wa sufuria ambayo sasa

ina ukoko ndani yake,

ambayo ukoko wake hautoki.

Kipakue kipande baada ya kipande,

bila kuvipigia kura.

724:7 Law 17:13; Kum 12:16“ ‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake:

huyo mwanamke aliimwaga

juu ya mwamba ulio wazi;

hakuimwaga kwenye ardhi,

ambako vumbi lingeifunika.

824:8 Mt 7:2Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi,

nimemwaga damu yake

juu ya mwamba ulio wazi,

ili isifunikwe.

924:9 Eze 24:6; Nah 3:1; Hab 2:12“ ‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ole wa mji umwagao damu!

Mimi nami nitalundikia kuni nyingi.

10Kwa hiyo lundika kuni

na uwashe moto.

Pika hiyo nyama vizuri,

changanya viungo ndani yake,

na uiache mifupa iungue kwenye moto.

1124:11 Yer 21:10; Eze 22:15Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaa

mpaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae,

ili uchafu wake upate kuyeyuka

na ukoko wake upate kuungua na kuondoka.

12Imezuia juhudi zote,

ukoko wake mwingi haujaondoka,

hata ikiwa ni kwa moto.

1324:13 Mao 1:9; Zek 6:8; Eze 5:13; 8:18; Isa 22:14; Yer 6:28-30; Eze 16:18“ ‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua.

1424:14 Zek 8:14; Hes 23:19; Isa 3:11; Eze 18:30; Isa 22:14; Hes 11:23; Ay 27:22“ ‘Mimi Bwana nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema Bwana Mwenyezi.’ ”

Kifo Cha Mke Wa Ezekieli

15Neno la Bwana likanijia kusema: 1624:16 Yer 13:17; 16:5; Za 39:10; 84:1; Mao 2:4; Yer 22:10“Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote. 1724:17 Yer 16:7; Hes 20:29; Isa 3:20; 20:2; 20:2; Law 13:45Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.”

1824:18 Eze 12:7Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa.

1924:19 Eze 12:9; 37:18Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?”

20Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la Bwana lilinijia kusema: 2124:21 Za 27:4; Yer 7:14; Eze 23:25; Hos 9:12-16; Mal 2:12; Law 26:19, 31‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga. 2224:22 Yer 16:7; Law 13:45Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji. 2324:23 Kut 33:4; Ay 27:15; Za 78:64; Kut 28:39; Isa 3:20Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake. 2424:24 Isa 20:3; Eze 4:3; Yn 13:19; Eze 12:11Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’

2524:25 Kum 28:32; Yer 11:22; Za 20:4; Mao 2:4“Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile, 2624:26 1Sam 4:12; Ay 1:15-19siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari. 2724:27 Eze 3:26; 33:22; Dan 10:15Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以西结书 24:1-27

锈锅的比喻

1第九年十月十日,耶和华对我说: 2“人子啊,今天是巴比伦王围攻耶路撒冷的日子,你要记下这日子。 3你要向叛逆的以色列人说比喻,告诉他们,主耶和华这样说,

“‘把锅放在火上,

里面倒进水,

4把羊腿、羊肩等上好的肉块放进锅里,

让锅里盛满精选的骨头。

5要从羊群中选一头上好的羊,

把柴堆在锅下,

烧开锅煮里面的骨头。’”

6主耶和华说:“这像锈锅一样充满血腥的城有祸了!要把肉从这锈迹斑斑的锅中一块块地取出来。 7这城沾满血腥,任凭受害者的血流在光秃秃的磐石上,而不是流在地上用土掩盖。 8我任凭这城把受害者的血洒在磐石上,不加掩盖,好激起我的烈怒,使她受报应。 9所以主耶和华说,‘血腥的城啊,你有祸了!我要预备大堆木柴, 10添在火上,燃起旺火,把肉煮烂,加入香料,烧焦骨头。 11然后,把倒空的锅放在炭火上烧热,把铜烧红,好熔化它的杂质,除净锈垢, 12却徒劳无功,因为锈垢太厚,就是用火也不能清除。 13耶路撒冷啊,淫荡使你污秽不堪,我要洁净你,你却不愿被洁净。所以,除非我向你倾尽一切愤怒,否则你的污秽将不能清除。 14我耶和华言出必行,决不宽容,也不留情,我必照你的所作所为来审判你。’这是主耶和华说的。”

15耶和华对我说: 16“人子啊,我要突然夺去你心爱的人,你不可悲伤,也不可流泪哭泣。 17你要默然哀叹,不可为死人办丧事,仍要缠着头巾,穿着鞋,不可蒙着脸,也不可吃丧家吃的饭。” 18早晨我把这事告诉百姓,晚上我的妻子便死了。次日早晨,我便遵照耶和华的吩咐行。

19百姓问我:“你可以告诉我们,你这样做跟我们有什么关系吗?” 20我告诉他们:“耶和华对我说, 21‘你告诉以色列人,我要使我的圣所,就是你们引以为傲、眼中所爱、心里所慕的受到亵渎。你们留下的儿女必死于刀下。 22那时,你们将像我的仆人一样不蒙脸,不吃丧家吃的饭。 23你们仍将裹着头巾,穿着鞋,不哭泣,也不悲伤。你们必因自己的罪恶而默然叹息,逐渐灭亡。 24以西结做的事都是你们的预兆,你们也将做他做的。当这事发生时,你们就知道我是主耶和华了。’

25“人子啊,有一天我要夺去他们所喜悦、所夸耀、眼中所爱、心里所慕的堡垒,也要夺去他们的儿女。 26那日,幸存的人必来告诉你这个消息。 27那时,你必开口向那人说话,不再沉默。你必成为他们的预兆,他们就知道我是耶和华。”