Ezekieli 20 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 20:1-49

Israeli Waasi

120:1 Eze 8:1; 1:1-2; 21:1; Mwa 25:22Katika mwaka wa saba, mwezi wa tano siku ya kumi, baadhi ya wazee wa Israeli wakaja ili kutaka ushauri kwa Bwana, wakaketi mbele yangu.

2Ndipo neno la Bwana likanijia kusema: 320:3 Mwa 25:22; Eze 14:3; 1Sam 28:6; Amo 8:12; Mit 15:8; Mt 15:8; Isa 1:15“Mwanadamu, sema na wazee wa Israeli uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa nini mmekuja? Je, ni kutaka ushauri kwangu? Hakika kama niishivyo, sitawaruhusu mtake ushauri toka kwangu, asema Bwana Mwenyezi.’

420:4 Eze 22:2; 23:36; 16:2“Je, utawahukumu? Je, mwanadamu, utawahukumu? Basi uwakabili kwa ajili ya machukizo ya baba zao 520:5 Kum 7:6; Law 11:44; Kut 20:2; Kum 4:34; Mwa 14:22; Hes 14:30na uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Siku ile nilipochagua Israeli, niliwaapia wazao wa nyumba ya Yakobo kwa mkono ulioinuliwa nami nikajidhihirisha kwao huko Misri. Kwa mkono ulioinuliwa niliwaambia, “Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.” 620:6 Kut 3:8; Dan 8:9; Za 48:2; Dan 11:41; Kut 6:8; Kum 29:18Siku ile niliwaapia wao kwamba nitawatoa katika nchi ya Misri na kuwaleta katika nchi niliyowachagulia, nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi nzuri kupita zote. 720:7 Kut 20:2-4; Law 18:3; Eze 6:9; Kum 29:18Nami nikawaambia, “Kila mmoja wenu aondolee mbali sanamu za chukizo ambazo mmekazia macho, nanyi msijitie unajisi kwa sanamu za Misri. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”

820:8 Yer 11:10; Eze 16:26; Kut 32:7; Kum 9:7; Isa 63:10; Yer 7:26“ ‘Lakini waliniasi na hawakunisikiliza, hawakuondolea mbali sanamu za machukizo ambazo walikuwa wamezikazia macho, wala kuondolea mbali sanamu za Misri. Ndipo nikasema, nitawamwagia ghadhabu yangu na kutimiza hasira yangu dhidi yao huko Misri. 920:9 Eze 36:22; 39:7; Kut 32:12; Hes 14:13; Isa 48:11Lakini kwa ajili ya Jina langu nilifanya kile ambacho kingelifanya lisitiwe unajisi machoni mwa mataifa waliyoishi miongoni mwao na ambao machoni pao nilikuwa nimejifunua kwa Waisraeli kwa kuwatoa katika nchi ya Misri. 1020:10 Kut 13:18Kwa hiyo nikawaongoza watoke Misri na kuwaleta jangwani. 1120:11 Kut 20:1-23; Rum 10:5; Neh 9:13; Eze 18:9; Kum 4:7-8; Law 18:5Nikawapa amri zangu na kuwajulisha sheria zangu, kwa kuwa mtu anayezitii ataishi kwa hizo. 1220:12 Kut 31:13; Kum 5:12; Kut 20:10; Yer 17:22; Law 20:8Pia niliwapa Sabato zangu kama ishara kati yangu nao, ili wapate kujua kuwa Mimi Bwana niliwafanya kuwa watakatifu.

1320:13 Za 78:40; Kum 9:8; Law 26:15; Hes 14:29; Za 95:8-10; Isa 56:6; Kut 32:10“ ‘Lakini watu wa Israeli waliniasi Mimi jangwani. Hawakufuata amri zangu, bali walikataa sheria zangu, ingawa mtu yule anayezitii ataishi kwa hizo sheria, nao walizinajisi Sabato zangu kabisa. Hivyo nilisema ningemwaga ghadhabu yangu juu yao na kuwaangamiza huko jangwani. 1420:14 Eze 36:23; Isa 48:11Lakini kwa ajili ya Jina langu nikafanya kile ambacho kitalifanya Jina langu lisitiwe unajisi machoni mwa mataifa ambao mbele yao nilikuwa nimewatoa Waisraeli. 1520:15 Hes 14:22-23, 28; Ebr 3:11; Kum 1:34; Za 106:26; 95:11Tena kwa mkono ulioinuliwa nikawaapia huko jangwani kwamba nisingewaingiza katika nchi niliyokuwa nimewapa, yaani, nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi nzuri kuliko zote, 1620:16 Hes 16:39; Amo 5:26; Mdo 7:42-43; Yer 1:8; Amo 2:4; Hes 15:39kwa sababu walikataa sheria zangu na hawakufuata amri zangu na wakazinajisi Sabato zangu. Kwa kuwa mioyo yao iliandama sanamu zao. 1720:17 Za 78:38Lakini niliwahurumia wala sikuwaangamiza wala hakuwafuta kabisa jangwani. 1820:18 2Nya 30:7; Za 106; 39Niliwaambia watoto wao kule jangwani, “Msifuate amri za baba zenu wala kushika sheria zao au kujinajisi kwa sanamu zao. 1920:19 Kut 20:2; Kum 11:1; 5:32-33Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, fuateni amri zangu tena kuweni waangalifu kushika sheria zangu. 2020:20 Yer 17:22; Kut 20:10; 31:13Zitakaseni Sabato zangu ili ziwe ishara kati yangu nanyi. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”

2120:21 Yer 7:26; Hes 25:3; Eze 7:8“ ‘Lakini watoto hao wakaniasi: Hawakufuata amri zangu, wala hawakuwa waangalifu kushika sheria zangu, ingawa mtu anayezitii anaishi kwa hizo sheria, nao wakazinajisi Sabato zangu. Hivyo nikasema ningemwaga ghadhabu yangu juu yao na kutimiza hasira yangu dhidi yao huko jangwani. 2220:22 Za 78:38Lakini nikauzuia mkono wangu na kwa ajili ya Jina langu nikafanya kile ambacho kingelifanya Jina langu lisitiwe unajisi machoni mwa mataifa ambao mbele yao nilikuwa nimewatoa Waisraeli. 2320:23 Law 26:33; Kum 28:64; Za 106:27; Yer 15:4Tena kwa mkono ulioinuliwa nikawaapia huko jangwani kwamba ningewatawanya miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, 2420:24 Eze 2:3; 6:9; 18:6; Amo 2:4kwa sababu hawakutii sheria zangu lakini walikuwa wamekataa amri zangu na kuzinajisi Sabato zangu, nayo macho yao yakatamani sanamu za baba zao. 2520:25 Za 81:12; Rum 1:24-28; 2The 2:11; Isa 66:4Pia niliwaacha wafuate amri ambazo hazikuwa nzuri na sheria ambazo mtu hawezi kuishi kwa hizo sheria. 2620:26 Law 20:2-5; 2Fal 17:17; Eze 16:20-21; Law 18:21Nikawaacha wanajisiwe kwa matoleo yao, kuwatoa wazaliwa wao wa kwanza kafara kwa sanamu, yaani, kule kuwapitisha wazaliwa wao wa kwanza kwenye moto, nipate kuwajaza na hofu ili wajue kwamba Mimi ndimi Bwana.’

2720:27 Hes 15:30; Rum 1:23; 2:24; Eze 18:24; Za 78:57“Kwa hiyo, mwanadamu, sema na watu wa Israeli na uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika hili pia, baba zenu walinikufuru kwa kuniacha mimi: 2820:28 Neh 9:23; Za 78:55-58; Yer 19:13; Eze 6:13; Yer 2:7; 3:6Nilipowaleta katika nchi ile ambayo nilikuwa nimeapa kuwapa na kuona kilima chochote kirefu au mti wowote wenye majani mengi, huko walitoa dhabihu zao, wakatoa sadaka ambazo zilichochea hasira yangu, wakafukiza uvumba wenye harufu nzuri na kumimina sadaka zao za kinywaji. 29Ndipo nikawaambia: Ni nini maana yake hapa mahali pa juu pa kuabudia miungu mnapopaendea?’ ” (Basi jina la mahali pale panaitwa Bama20:29 Bama maana yake ni mahali pa juu pa kuabudia miungu. hata hivi leo.)

Hukumu Na Kurudishwa

3020:30 Amu 2:16-19; Yer 16:12“Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, mtajinajisi kama vile baba zenu walivyofanya na kutamani vinyago vyao vya machukizo? 3120:31 Mit 1:27-28; Eze 16:20; Amo 8:12; Zek 7:13; Za 106:37-39; Yer 7:31Mnapotoa matoleo yenu, yaani, wana wenu kafara katika moto, mnaendelea kujinajisi na sanamu zenu zote hadi siku hii ya leo. Je, niulizwe neno na ninyi, ee nyumba ya Israeli? Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, mimi sitaulizwa neno na ninyi.

3220:32 Eze 11:5“ ‘Lile lililoko mioyoni mwenu kamwe halitatokea, mnaposema, “Tunataka tuwe kama mataifa mengine, kama watu wengine wa dunia, wanaotumikia miti na mawe.” 3320:33 Yer 21:5; Eze 25:16; 16:27Hakika kama niishivyo asema Bwana Mwenyezi, nitatawala juu yenu kwa mkono wa nguvu na kwa mkono ulionyooshwa na kwa ghadhabu iliyomwagwa. 3420:34 2Kor 6:17; Yer 44:6; Mao 2:4; Kum 30:4; Isa 27:12-13; 31:3Nitawatoa toka katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mlikotawanywa, kwa mkono wa nguvu na kwa mkono ulionyooshwa na kwa ghadhabu iliyomwagwa. 3520:35 1Sam 12:7; Ay 22:4; Eze 19:13; Yer 2:35Nitawaleta katika jangwa la mataifa na huko nitatekeleza hukumu juu yenu uso kwa uso. 3620:36 Hes 14:28-30; 1Kor 10:5-10; Hes 11:1-35Kama nilivyowahukumu baba zenu katika jangwa la nchi ya Misri, ndivyo nitakavyowahukumu ninyi, asema Bwana Mwenyezi. 3720:37 Law 27:32; Yer 33:13; Eze 16:62Nitawafanya mpite chini ya fimbo yangu, nami nitawaleta katika mkataba wa Agano. 3820:38 Eze 34:17-22; Amo 9:9-10; Hos 2:14; Ebr 4:3; Za 95:11; Eze 13:9; Zek 13:8-9Nitawaondoa miongoni mwenu wale wanaohalifu na wale wanaoasi dhidi yangu. Ingawa nitawatoa katika nchi wanazoishi, hawataingia katika nchi ya Israeli. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

3920:39 Yer 44:25; Isa 1:13; Amo 4:4; Mit 21:27; Kut 20:7; Eze 13:19; 43:7“ ‘Kwa habari zenu ninyi, ee nyumba ya Israeli, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nendeni mkatumikie sanamu zenu, kila mmoja wenu! Lakini baadaye hakika mtanisikiliza mimi nanyi hamtalinajisi tena Jina langu takatifu, kwa matoleo yenu na sanamu zenu. 4020:40 Isa 60:7; 56:7; Mal 3:4; Zek 8:20; Rum 12:1; Eze 17:22; 34:14Kwa kuwa katika mlima wangu mtakatifu, mlima mrefu wa Israeli, asema Bwana Mwenyezi, hapo katika nchi nyumba yote ya Israeli itanitumikia mimi, nami huko nitawakubali. Huko nitataka sadaka zenu na matoleo ya malimbuko yenu, pamoja na dhabihu zenu takatifu zote. 4120:41 Eze 28:25; 36:23; Isa 5:16; 2Kor 6:17; 2:14; Kum 30:4Nitawakubali ninyi kama uvumba wenye harufu nzuri wakati nitakapowatoa katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mlipokuwa mmetawanyika, nami nitajionyesha kuwa mtakatifu miongoni mwenu na machoni mwa mataifa. 4220:42 Eze 38:23; Yer 23:8; Eze 36:24; Yer 30:3; Eze 34:13; 34:27Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapowaleta katika nchi ya Israeli, nchi niliyokuwa nimeapa kwa mkono ulioinuliwa kuwapa baba zenu. 4320:43 Eze 16:61; Law 26:39; Eze 6:9; Hos 5:15Hapo ndipo nitakapokumbuka mwenendo wenu na matendo yenu yote ambayo kwayo mlijitia unajisi, nanyi mtajichukia wenyewe kwa ajili ya maovu yote mliyokuwa mmetenda. 4420:44 Za 109:21; Isa 43:25; Eze 24:24; 36:32Nanyi mtajua kuwa mimi ndimi Bwana, nitakaposhughulika nanyi kwa ajili ya Jina langu na wala si sawasawa na njia zenu mbaya na matendo yenu maovu, ee nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.’ ”

Unabii Dhidi Ya Kusini

45Neno la Bwana likanijia kusema: 4620:46 Eze 21:2; Amo 7:16; Isa 30:6; Yer 13:17-19“Mwanadamu, uelekeze uso wako upande wa kusini, hubiri juu ya upande wa kusini na utoe unabii juu ya msitu wa Negebu. 4720:47 Yer 21:14; Isa 13:8; Eze 21:4; 2Fal 19:23; Isa 9:18-19; Eze 19:14Waambie watu wa Negebu: ‘Sikieni neno la Bwana. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kukutia moto, nao utateketeza miti yako yote, mibichi na iliyokauka. Miali ya moto haitaweza kuzimwa na kila uso kutoka kusini mpaka kaskazini utakaushwa kwa moto huo. 4820:48 Yer 7:20; Eze 21:5, 32; 23:25Kila mmoja ataona kuwa mimi Bwana ndiye niliyeuwasha huo moto, nao hautazimwa.’ ”

4920:49 Amu 14:12; Yn 16:24-25; Eze 4:14; Za 78:2; Eze 12:9; Mt 13:13Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi! Wao hunisema, ‘Huyu si huzungumza mafumbo tu?’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以西結書 20:1-49

以色列人的悖逆

1第七年五月十日,有幾個以色列的長老來到我這裡,坐在我面前。 2耶和華對我說: 3「人子啊,你要告訴他們,主耶和華這樣說,『你們是來求問我嗎?我憑我的永恆起誓,我決不讓你們求問。』 4人子啊,你要審判他們?你要審判他們?要使他們知道他們祖先所做的可憎之事。 5你要告訴他們,主耶和華這樣說,『我揀選以色列那日,曾向雅各家的後裔起誓,又在埃及向他們顯現,告訴他們我是他們的上帝耶和華。 6那日我向他們起誓,要帶領他們離開埃及,到我為他們預備的奶蜜之鄉,世上最佳美的地方。 7我告訴他們要除掉他們祭拜的可憎之物,不可讓埃及的偶像玷污自己,因為我是他們的上帝耶和華。

8「『然而,他們卻背叛我,不聽我的話,沒有除去他們祭拜的可憎之物和埃及的偶像。我本想在埃及向他們發烈怒,傾倒我的怒火, 9但我沒有這樣做,以免我的名在他們寄居的列邦面前被褻瀆。因為列邦親眼看見我向以色列人顯現,把他們帶出埃及10於是,我帶他們離開埃及,進入曠野, 11向他們頒佈我的律例和典章,若有人遵守,就必活著。 12我又讓他們遵守我的安息日,作為我與他們之間的記號,好叫他們知道是我耶和華使他們成為聖潔之民。

13「『可是,以色列人卻在曠野背叛我,不遵行我的律例和典章——遵行的人必活著,大肆褻瀆我的安息日。我本想在曠野向他們發烈怒,滅絕他們。 14但我沒有這樣做,以免我的名在周圍列邦面前被褻瀆,因為列邦親眼看見我向以色列人顯現,把他們帶出埃及15我在曠野曾向他們發誓,不帶他們進入我賜給他們的那奶蜜之鄉,那世上最佳美的地方, 16因為他們不遵守我的典章,不順從我的律例,褻瀆我的安息日,心戀偶像。 17但我憐憫他們,沒有毀滅他們,沒有在曠野把他們全部滅絕。

18「『我在曠野曾對他們的子孫說,不要效法你們祖先的律例,不要遵守他們的規條,不要拜他們的偶像,以致玷污自己。 19我是你們的上帝耶和華,你們要恪守我的律例,謹遵我的典章, 20尊我定的安息日為聖日,作為我與你們之間的記號,使你們知道我是你們的上帝耶和華。

21「『可是,他們的子孫卻背叛我,不恪守我的律例,不謹遵我的典章——遵守的人必活著。他們褻瀆我的安息日。我本想在曠野向他們發烈怒,傾倒我的怒氣, 22但我沒有這樣做,以免我的名在周圍列邦面前被褻瀆,因為列邦親眼看見我向以色列人顯現,把他們帶出埃及23我在曠野起誓要把他們驅散到列國,分散到列邦, 24因為他們不遵行我的典章,棄絕我的律例,褻瀆我的安息日,眼睛戀慕他們祖先的偶像。 25所以,我任由他們效法無用的律例,遵守無法使人活著的規條, 26任由他們把自己的長子燒作祭物獻給偶像,以致玷污自己——好使他們充滿恐懼,這樣他們便知道我是耶和華。』

27「人子啊,你要告訴以色列人,主耶和華這樣說,『你們的祖先背信棄義,褻瀆了我。 28當我引領他們進入我曾起誓要賜給他們的土地時,他們在所見的每一處高山或密林獻祭,焚燒馨香的祭牲,向偶像奠酒,惹我發怒。 29我問他們,你們所去的高處是什麼地方?』從此,那高處一直叫巴麻

30「所以,你要告訴以色列人,主耶和華這樣說,『你們仍像你們祖先一樣與可憎的偶像苟合,玷污自己嗎? 31你們至今仍把自己的兒子燒作祭物獻給偶像,玷污自己嗎?以色列人啊,我會讓你們求問嗎?主耶和華說,我憑我的永恆起誓,我決不讓你們求問。

32「『你們說要像外族人一樣去供奉木頭石頭,你們的想法絕不能實現!』

33「主耶和華說,『我憑我的永恆起誓,我要發烈怒,伸出大能的臂膀治理你們。 34我要發烈怒,伸出大能的臂膀把你們從列國中領出來,從你們散居的列邦聚集你們, 35領你們進入外族人的曠野,面對面地審判你們, 36就像我從前在埃及的曠野審判你們的祖先一樣。這是主耶和華說的。 37我要對你們嚴加管教20·37 對你們嚴加管教」希伯來文是「讓你們在杖下經過」。,使你們遵守我的約。 38我要剷除你們中間叛逆和犯罪的人。雖然我要領他們離開寄居之地,他們卻不能回以色列。這樣,你們就知道我是耶和華。』

39「主耶和華說,『你們以色列人若不聽我的話,就去供奉你們的偶像吧!但將來你們必不再向偶像獻祭物褻瀆我的聖名!』

40「主耶和華說,『在我的聖山,就是以色列的高山上,所有的以色列人都要事奉我,我要在那裡悅納你們,要求你們獻上供物、最好的禮物和一切聖物。 41當我把你們從列國領出來,從你們散居的列邦聚集起來時,你們必如馨香之祭一樣蒙我悅納,我必當著列國的面在你們中間彰顯我的聖潔。 42我要把你們帶回我起誓應許給你們祖先的以色列,這樣你們就知道我是耶和華。 43你們在那裡會想起以往玷污自己的行徑,並因自己的一切惡行而憎惡自己。』 44主耶和華說,『以色列人啊,我為了自己的名,沒有照你們的邪惡行徑懲罰你們,這樣你們便知道我是耶和華。』」

45耶和華對我說: 46「人子啊,你要面向南方,說預言斥責南地的樹林。 47你要對南地的樹林說,『你要聽耶和華的話。主耶和華說,我要在你那裡燃起火來,燒毀你所有的青樹和枯樹。這不熄的烈火要從南到北燒焦一切。 48這樣,世人便知道這烈火是我耶和華點燃的,它絕不會熄滅。』」 49於是我說:「唉,主耶和華啊,他們在議論我說,『這人豈不是在說比喻嗎?』」