Ezekieli 19 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 19:1-14

Maombolezo Kwa Ajili Ya Wakuu Wa Israeli

119:1 Yer 7:29; 2Nya 24:6; Eze 26:17; Yer 9:10, 20; Eze 27:32; 28:12“Wewe fanya maombolezo kuhusu wakuu wa Israeli 219:2 Hes 23:24; Mwa 49:9na useme:

“ ‘Tazama jinsi gani mama yako alivyokuwa simba jike

miongoni mwa simba!

Alilala katikati ya wana simba

na kulisha watoto wake.

319:3 Eze 19:6; 2Fal 23:31, 32Alimlea mmoja wa watoto wake,

naye akawa simba mwenye nguvu.

Akajifunza kurarua mawindo

naye akala watu.

419:4 2Nya 36:4; Mao 4:20; Ay 41:2; 2Fal 23:33-34Mataifa wakasikia habari zake,

naye akanaswa katika shimo lao.

Wakamwongoza kwa ndoana

mpaka nchi ya Misri.

519:5 2Fal 23:34; Mwa 49:9“ ‘Mama yake alipongoja na kuona tumaini lake halitimiziki,

nayo matarajio yake yametoweka,

akamchukua mwanawe mwingine

na kumfanya simba mwenye nguvu.

619:6 Yer 22:13; 2Nya 36:9; 2Fal 24:9Alizungukazunguka miongoni mwa simba,

kwa kuwa sasa alikuwa simba mwenye nguvu.

Akajifunza kurarua mawindo

naye akala watu.

719:7 Eze 29:10; 30:12Akabomoa ngome zao

na kuiharibu miji yao.

Nchi na wote waliokuwa ndani yake

wakatiwa hofu kwa kunguruma kwake.

819:8 2Fal 24:2, 11; Mao 4:20; Eze 12:13; 2Fal 24:11Kisha mataifa wakaja dhidi yake

kutoka sehemu zilizomzunguka.

Wakatanda nyavu zao kwa ajili yake,

naye akanaswa katika shimo lao.

919:9 2Fal 25:7; 24:15; 2Nya 36:6; 2Fal 19:28; Zek 11:3Kwa kutumia ndoana wakamvutia kwenye tundu

na kumleta mpaka kwa mfalme wa Babeli.

Wakamtia gerezani, hivyo kunguruma kwake

hakukusikika tena

katika milima ya Israeli.

1019:10 Za 80:8-11; Eze 15:2; Yer 17:8; Mwa 49:22“ ‘Mama yako alikuwa kama mzabibu

katika shamba lako la mizabibu

uliopandwa kando ya maji,

ukiwa unazaa sana na wenye matawi mengi

kwa sababu ya wingi wa maji.

1119:11 Eze 31:3; Dan 4:11Matawi yake yalikuwa na nguvu,

yaliyofaa kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.

Ulikuwa mrefu kupita miti mingine

katikati ya matawi manene;

ulionekana kwa urahisi

kwa ajili ya urefu wake

na wingi wa matawi yake.

1219:12 Kum 29:28; Eze 17:10; Hos 13:15; Isa 27:11; Eze 28:17; Mwa 41:6Lakini ulingʼolewa kwa hasira kali

na kutupwa chini.

Upepo wa mashariki uliufanya usinyae,

matunda yake yakapukutika,

matawi yake yenye nguvu yakanyauka

na moto ukayateketeza.

1319:13 Eze 20:35; Hos 2:14; 2:3Sasa umepandwa jangwani

katika nchi kame na ya kiu.

1419:14 Amu 9:15; Eze 20:47; 15:4Moto ulienea kuanzia katika mmojawapo ya matawi yake makubwa

na kuteketeza matunda yake.

Hakuna tawi lenye nguvu lililobaki juu yake

lifaalo kuwa fimbo ya enzi ya mtawala.’

Hili ndilo ombolezo, na litumike kama ombolezo.”

New International Reader’s Version

Ezekiel 19:1-14

A Song of Sadness About Israel’s Princes

1“Sing a song of sadness about Israel’s princes. 2Say to Israel,

“ ‘You were like a mother lion to your princes.

She lay down among the lions.

She brought up her cubs.

3One of them was Jehoahaz.

He became a strong lion.

He learned to tear apart what he caught.

And he became a man-eater.

4The nations heard about him.

They trapped him in their pit.

They put hooks in his face.

And they led him away to Egypt.

5“ ‘The mother lion looked and waited.

But all her hope was gone.

So she got another one of her cubs.

She made him into a strong lion.

6He prowled with the lions.

He became very strong.

He learned to tear apart what he caught.

And he became a man-eater.

7He broke down their forts.

He completely destroyed their towns.

The land and all those who were in it

were terrified when he roared.

8Then nations came against him.

They came from all around him.

They spread out their net to catch him.

He was trapped in their pit.

9They used hooks to pull him into a cage.

They brought him to the king of Babylon.

They put him in prison.

So his roar was not heard anymore

on the mountains of Israel.

10“ ‘Israel, you were like a vine in a vineyard.

It was planted near water.

It had a lot of fruit and many branches.

There was plenty of water.

11Its branches were strong.

Each was good enough to be made into a ruler’s scepter.

The vine grew high

above all the leaves.

It stood out because it was so tall

and had so many branches.

12But Nebuchadnezzar became angry.

He pulled it up by its roots.

He threw it to the ground.

The east wind dried it up.

Its fruit was stripped off.

Its strong branches dried up.

And fire destroyed them.

13Now it is planted in the Babylonian desert.

It is in a dry and thirsty land.

14One of its main branches was Zedekiah.

Fire spread from it and burned up its fruit.

None of its branches is good enough

to be made into a ruler’s scepter.’

This is a song of sadness. And that is how it should be used.”