Ezekieli 18 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 18:1-32

Roho Itendayo Dhambi Itakufa

1Neno la Bwana likanijia kusema: 218:2 Isa 3:15; Mao 5:7; Ay 21:19; Yer 31:29“Je, ninyi watu mna maana gani kutumia mithali hii inayohusu nchi ya Israeli:

“ ‘Baba wamekula zabibu zenye chachu,

nayo meno ya watoto yametiwa ganzi’?

318:3 Za 49:4“Hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hamtatumia tena mithali hii katika Israeli. 418:4 Mwa 18:32; Rum 6:23; Ebr 12:9; 2Fal 14:6; Mit 13:21; Kut 17:14; Ay 21:20; Isa 42:5; Eze 33:8Kwa kuwa kila roho ni mali yangu, kama vile ilivyo roho ya baba, vivyo hivyo roho ya mtoto ni mali yangu. Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa.

5“Mtu aweza kuwa ni mwenye haki

atendaye yaliyo haki na sawa.

618:6 Eze 6:2; 22:9; Kum 4:19; Amo 5:26; Ebr 13:4; Eze 6:13; Law 15:24Hakula katika mahali pa ibada za miungu

kwenye milima

wala hakuziinulia macho sanamu

za nyumba ya Israeli.

Hakumtia unajisi mke wa jirani yake,

wala hakukutana kimwili na mwanamke

wakati wa siku zake za hedhi.

718:7 Yak 5:4; Kut 22:26; Kum 24:12; 24:12; 15:11; Lk 3:11; Kut 20:15; Ay 22:7Hamwonei mtu yeyote,

bali hurudisha kilichowekwa rehani kwake.

Hanyangʼanyi, bali huwapa wenye njaa chakula chake

na huwapa nguo walio uchi.

818:8 Zek 8:16; Kut 18:21; Kum 23:19-20; Yer 22:3; Kut 22:25; Law 25:35-37Hakopeshi kwa riba

wala hajipatii faida ya ziada.

Huuzuia mkono wake usifanye mabaya,

naye huhukumu kwa haki kati ya mtu na mtu.

918:9 Hab 2:4; Law 18:5; Amo 5:4; Law 19:37; Eze 11:12; 20:11Huzifuata amri zangu

na kuzishika sheria zangu kwa uaminifu.

Huyo mtu ni mwenye haki;

hakika ataishi,

asema Bwana Mwenyezi.

1018:10 Kut 21:12; Eze 22:6“Aweza kuwa ana mwana jeuri, amwagaye damu au atendaye mojawapo ya mambo haya 1118:11 Kut 22:22; Ay 24:9; Isa 54:9; 59:6-7; Hab 2:6; Kut 22:17; Eze 16:49(ingawa baba yake hakufanya mojawapo ya haya):

“Hula katika mahali pa ibada za miungu kwenye milima.

Humtia unajisi mke wa jirani yake.

1218:12 Kut 22:22; 22:27; Ay 24:9; Amo 4:1; 2Fal 21:11Huwaonea maskini na wahitaji.

Hunyangʼanyana.

Harudishi kile kilichowekwa rehani kwake.

Huziinulia sanamu macho.

Hufanya mambo ya machukizo.

1318:13 Kut 22:25; Law 20:9; Hos 12:14; Eze 33:4-5Hukopesha kwa riba na kutafuta faida ya ziada.

Je, mtu wa namna hii ataishi? Hapana, hataishi! Kwa sababu amefanya mambo haya yote ya machukizo, hakika atauawa na damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.

1418:14 2Nya 34:21; Mit 23:24“Lakini yawezekana mwana huyo ana mwana aonaye dhambi hizi zote anazofanya baba yake, naye ingawa anaziona, yeye hafanyi mabaya kama haya:

1518:15 Eze 22:9; Za 24:4“Hakula katika mahali pa ibada za miungu

kwenye milima,

wala hainulii macho sanamu

za nyumba ya Israeli.

Hakumtia unajisi

mke wa jirani yake.

1618:16 Kut 22:27; Ay 22:7; Mit 22:9; Za 41:1; Eze 16:49; Isa 7:10Hakumwonea mtu yeyote

wala hakutaka rehani kwa ajili ya mkopo.

Hanyangʼanyi,

bali huwapa wenye njaa chakula chake

na huwapa nguo walio uchi.

1718:17 Za 1:2Huuzuia mkono wake usitende dhambi,

hakopeshi kwa riba

wala hajipatii faida ya ziada.

Huzishika amri zangu

na kuzifuata sheria zangu.

Hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake; hakika ataishi. 1818:18 Eze 3:18Lakini baba yake atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe, kwa sababu alitoza bei isiyo halali kwa nguvu, akamnyangʼanya ndugu yake na kufanya yaliyo mabaya miongoni mwa watu wake.

1918:19 Kut 20:5; Kum 5:9; Yer 15:4; Zek 1:3-6“Lakini mnauliza, ‘Kwa nini mwana asiadhibiwe kwa uovu wa baba yake?’ Kwa vile mwana ametenda yaliyo haki na sawa na amekuwa mwangalifu kuzishika amri zangu zote, hakika ataishi. 2018:20 Kum 24:16; Rum 2:9; Isa 3:10; Hes 15:31; 1Fal 8:32; 2Fal 14:6; Eze 7:27; Mt 16:27Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa. Mwana hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya baba yake, wala baba hataadhibiwa kwa ajili ya makosa ya mwanawe. Haki ya mtu mwenye haki itahesabiwa juu yake na uovu wa mtu mwovu utalipizwa juu yake.

2118:21 Eze 13:22; 33:12-19; Yer 18:8; Mwa 26:5“Lakini mtu mwovu akiacha dhambi zake zote alizozitenda na kushika amri zangu zote na kufanya lililo haki na sawa, hakika ataishi, hatakufa. 2218:22 Dan 4:27; Mik 7:19; Mit 18:20-24; Isa 43:25Hakuna kosa lolote alilotenda litakalokumbukwa juu yake. Kwa ajili ya mambo ya haki aliyoyatenda, ataishi. 2318:23 Mao 3:33; 2Pet 3:9; 1Tim 2:4; Za 147:11; Ay 37:23; Eze 16:6; Mik 7:18Je, mimi ninafurahia kifo cha mtu mwovu? Asema Bwana Mwenyezi. Je, si mimi ninafurahi wanapogeuka kutoka njia zao mbaya na kuishi?

2418:24 Ay 35:8; 2Pet 2:20-22; Ebr 10:38; Yer 34:6; Eze 15:8; 1Sam 15:11; 2Nya 24:17-20“Lakini kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi na kufanya mambo ya machukizo ambayo mtu mwovu hufanya, Je, ataishi? Hakuna hata mojawapo ya matendo ya haki aliyotenda litakalokumbukwa. Kwa sababu ya kukosa uaminifu kwake anayo hatia na kwa sababu ya dhambi alizozitenda, atakufa.

2518:25 Sef 3:5; Mal 3:1-17; Mwa 18:25; Yer 2:29; Eze 33:17; Mal 2:17“Lakini mnasema, ‘Njia ya Bwana si ya haki.’ Sikia, ee nyumba ya Israeli: Njia yangu siyo iliyo ya haki? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki? 2618:26 Eze 18:24Kama mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda dhambi, atakufa kwa ajili ya dhambi yake, kwa sababu ya dhambi alizotenda, atakufa. 2718:27 Isa 1:18; Eze 13:22Lakini mtu mwovu akigeuka kutoka maovu aliyoyatenda na kufanya yaliyo haki na sawa, ataokoa maisha yake. 2818:28 Eze 18:14; Isa 55:7Kwa kuwa anayafikiria na kugeuka kutoka makosa yake yote aliyoyatenda na kuyaacha, hakika ataishi, hatakufa. 29Lakini nyumba ya Israeli inasema, ‘Njia za Bwana si haki.’ Je, njia zangu si za haki, ee nyumba ya Israeli? Je, si njia zenu ndizo ambazo si za haki?”

3018:30 Yer 35:15; Eze 7:13; Mt 3:2; Hos 12:6; 1Pet 1:17; Isa 27“Kwa hiyo, ee nyumba ya Israeli, nitawahukumu, kila mmoja sawasawa na njia zake, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni! Geukeni kutoka makosa yenu yote, ndipo dhambi haitakuwa anguko lenu. 3118:31 Za 51:10; Isa 1:16-17; Eze 36:26; Efe 4:22; Amu 6:8; Yer 27:13; Eze 11:19Tupilieni mbali makosa yenu yote mliyoyatenda, nanyi mpate moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, ee nyumba ya Israeli? 3218:32 2Nya 7:14; Ay 37:23; Eze 33:11; Ay 22:23; Isa 55:7; Mal 3:7; Eze 16:6Kwa maana sifurahii kifo cha mtu awaye yote afaye katika uovu, asema Bwana Mwenyezi. Tubuni basi, mkaishi!

Священное Писание

Езекиил 18:1-32

Личная ответственность за грех

1Было ко мне слово Вечного:

2– Что вы имеете в виду, повторяя о земле исраильской поговорку:

«Отцы ели кислый виноград,

а у детей на зубах оскомина»?

3Верно, как и то, что Я живу, – возвещает Владыка Вечный, – вы больше не будете произносить эту поговорку в земле исраильской. 4Знайте, всякая жизнь принадлежит Мне: и отец, и сын – оба Мои. Кто согрешит, тот и умрёт.

5Если кто-то праведен и поступает справедливо и праведно:

6не ест в горных капищах,

не поклоняется идолам исраильтян,

не соблазняет жены другого

и не спит с женщиной во время её месячных,

7никого не притесняет

и возвращает должнику взятое у того в залог,

не грабит,

даёт свой хлеб голодным

и одевает нагих,

8не даёт в рост денег

и не взимает процентов,

удерживает руку от преступления

и справедливо судит между спорящими,

9следует Моим установлениям

и усердно исполняет Мои законы –

тот праведен; он, несомненно, будет жить, – возвещает Владыка Вечный.

10Если у него есть сын, который разбойничает, проливает чужую кровь и делает что-либо из нижеследующего 11(хотя его отец и не делал ничего подобного):

ест в горных капищах,

соблазняет жену другого,

12притесняет нищих и бедняков,

грабит,

не возвращает должнику взятое у того в залог,

поклоняется идолам,

творит мерзости,

13даёт деньги в рост

и взимает проценты, –

будет ли он жить? Нет! За то, что он совершил эти мерзости, он, несомненно, умрёт и сам будет повинен в своей смерти.

14Но если у такого человека есть сын, который видит грехи, совершённые отцом, и, видя, не поступает по его примеру:

15не ест в горных капищах,

не поклоняется идолам исраильтян,

не соблазняет жены другого,

16никого не притесняет,

не требует залога,

не грабит,

даёт свой хлеб голодным

и одевает нагих,

17удерживает руку от преступления,

не даёт денег в рост и не взимает процентов,

исполняет Мои законы и следует Моим установлениям, –

то он не умрёт за грех отца; он, несомненно, будет жить. 18А его отец умрёт за свой грех, потому что он вымогал, грабил брата и творил зло среди своего народа.

19А вы спрашиваете: «Почему же сын не причастен к вине отца?» Раз сын поступал справедливо и праведно и прилежно исполнял Мои установления, он, несомненно, будет жить. 20Кто согрешил, тот и умрёт. Сын не будет причастен к вине отца, и отец не будет причастен к вине сына. Праведность будет засчитана праведнику, и нечестие будет засчитано нечестивому.

21Но если нечестивый оставит грехи, которые творит, станет исполнять Мои установления и делать то, что справедливо и праведно, он, несомненно, будет жить; он не умрёт. 22Ни одно из преступлений, которые он совершил, не припомнится ему. Ради сделанных им праведных дел он будет жить. 23Неужели Мне больше угодна смерть нечестивого, – возвещает Владыка Вечный, – а не то, чтобы он оставил свои поступки и жил?

24Но если праведник оставит праведность, совершит преступление и начнёт совершать те же мерзости, что и нечестивый, то разве он будет жить? Ни одно из сделанных им праведных дел не вспомнится. За вероломство, в котором он повинен, и за совершённые им грехи он умрёт.

25А вы говорите: «Путь Владыки несправедлив». Слушайте, исраильтяне: это Мой-то путь несправедлив? Не ваши ли пути несправедливы? 26Если праведник оставит праведность и совершит преступление, то за это он и умрёт; за сделанное им преступление он умрёт. 27А если нечестивый оставит нечестие, которое творит, и примется делать то, что справедливо и праведно, он спасёт себе жизнь. 28За то, что, признав все преступления, которые он творил, он больше не будет делать зло, он, несомненно, будет жить; он не умрёт. 29А исраильтяне говорят: «Путь Владыки несправедлив». Мои ли пути несправедливы, народ Исраила? Не ваши ли?

30Поэтому, исраильтяне, Я буду судить вас, каждого по его делам, – возвещает Владыка Вечный. – Покайтесь! Оставьте свои преступления, чтобы грех не погубил вас. 31Отвергните преступления, которые вы совершили, и обретите новое сердце и новый дух. Зачем вам умирать, народ Исраила? 32Ничья смерть Мне не угодна, – возвещает Владыка Вечный. – Покайтесь и живите!