Ezekieli 11 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 11:1-25

Hukumu Juu Ya Viongozi Wa Israeli

111:1 Eze 8:16; 43:4-5; 3:12-14; Yer 5:5Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu. 211:2 Isa 29:20; Nah 1:11Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu. 311:3 Yer 1:13; Eze 24:3; 12:22, 27; Mik 3:3Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’ 411:4 Eze 3:4, 17Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”

511:5 Ebr 4:11; Za 26:2; Yer 17:10Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu. 611:6 Eze 7:23; 22:6Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.

711:7 Mik 3:2-3; Eze 24:3-13; Yer 1:13“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko. 811:8 Mit 10:24; Isa 66:4; Law 26:25; Yer 42:16Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi. 911:9 Za 106:41; Eze 5:8; Kum 28:36Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu. 1011:10 Yer 39:6; 2Fal 14:25Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana. 1111:11 Eze 24:6Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. 1211:12 Law 18:4; Eze 18:9; 8:10; 6:7Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”

1311:13 Eze 9:8; Amo 7:2Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”

14Neno la Bwana likanijia kusema: 1511:15 Eze 33:24“Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’

Ahadi Ya Kurudi Kwa Israeli

1611:16 Za 31:20; Isa 8:14; Za 91:9; Isa 4:6“Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’

1711:17 Neh 1:9; Yer 24:5-6; 3:18; 31:16; Eze 20:41; 28:25; 34:13“Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’

1811:18 Eze 5:11; 37:2311:18 Eze 5:11; 37:23“Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo. 1911:19 Za 86:11; Yer 32:36; Zek 7:12; Yer 24:7; Rum 2:5; 2Kor 3:3; Eze 36:26; 18:31; 2Nya 30:12Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama. 2011:20 Za 105:45; Kut 6:7; Ebr 8:10; Yer 11:4; 32:38; Eze 36:26-28Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao. 2111:21 Yer 16:11; Eze 16:43; Ebr 3:12; Eze 9:10Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”

2211:22 Eze 9:3; 10:19; Kut 24:16Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao. 2311:23 Eze 1:28; 8:4; Zek 14:4; Eze 10:4Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji. 2411:24 2Kor 12:2; Eze 8:3Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu.

Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka, 2511:25 Eze 3:4, 11; Mdo 20:20nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.

New Russian Translation

Иезекииль 11:1-25

Суд над вождями Израиля

1Дух поднял меня и перенес к тем воротам Господнего дома, что смотрят на восток. Там, у входа в ворота, было двадцать пять человек, и среди них я увидел Иазанию, сына Азура, и Пелатию, сына Беная, вождей народа.

2Господь сказал мне:

– Сын человеческий, вот люди, которые замышляют зло и дают в этом городе злые советы. 3Они говорят: «Разве не скоро придет время строить дома? Этот город – котел, а мы – мясо». 4Поэтому пророчествуй против них; пророчествуй, сын человеческий.

5Дух Господень сошел на меня и сказал мне:

– Скажи: «Так говорит Господь: Вот о чем вы думаете, дом Израиля. Я знаю то, что приходит вам на ум. 6Вы многих убили в этом городе и завалили его улицы трупами. 7Поэтому так говорит Владыка Господь: Ваши убитые, которых вы положили в нем – это мясо, а этот город – котел, но вас Я изгоню из него. 8Вы страшитесь меча, и Я пошлю на вас меч, – возвещает Владыка Господь. – 9Я изгоню вас из города, отдам во власть чужеземцев и исполню над вами приговор. 10Вы падете от меча; Я буду судить вас на границе Израиля. Тогда вы узнаете, что Я – Господь. 11Этот город не будет для вас котлом, а вы не будете в нем мясом; Я буду судить вас на границе Израиля. 12Тогда вы узнаете, что Я – Господь, потому что вы не соблюдали Моих установлений и не исполняли законов, но поступали по обычаям народов, которые вокруг вас».

13Пока я пророчествовал, Пелатия, сын Бенаи, умер. Тогда я пал ниц и громко закричал:

– О Владыка Господи! Неужели Ты до конца погубишь всех оставшихся в живых в Израиле?

Утешение пленникам

14Было ко мне слово Господа:

15– Сын человеческий, твои сородичи, твоя родня, те, кто разделил с тобой плен11:15 Букв.: «те, кто с тобой в родстве»., и весь дом Израиля – это те, о ком жители Иерусалима говорят: «Они далеко от Господа; эта земля отдана во владение нам».

16– Поэтому скажи: «Так говорит Владыка Господь: Хотя Я и изгнал их к другим народам и рассеял по странам, Я Сам на время11:16 Или: «в некой мере». стал для них святилищем в тех странах, куда они ушли».

17Поэтому скажи: «Так говорит Владыка Господь: Я соберу вас из народов и верну из стран, по которым вы были рассеяны, и опять отдам вам землю Израиля».

18Когда они вернутся туда, они уберут из нее все мерзости и все ее гнусности. 19Я дам им единое сердце и вложу в них новый дух; Я возьму у них сердце из камня и дам им сердце из плоти. 20Тогда они будут соблюдать Мои установления, хранить Мои законы и исполнять их. Они будут Моим народом, а Я буду их Богом. 21Но на головы тех, чьи сердца обращены к их гнусным истуканам и омерзительным идолам11:21 Букв.: «Но к сердцу их гнусностей и мерзостей их сердце идет»., Я обрушу то, что они заслужили, – возвещает Владыка Господь.

Слава Господня покидает Иерусалим

22И херувимы, с колесами возле них, расправили крылья, и слава Бога Израилева была над ними. 23Слава Господня поднялась из города и остановилась над горой к востоку от него. 24Дух поднял меня и перенес к пленникам в Халдею11:24 То есть в Вавилон; евр.: «касдим»; также в остальных местах книги. в видении, которое было дано Духом Божьим.

Потом видение, которое я видел, покинуло меня, 25и я рассказал пленникам обо всем, что показал мне Господь.