Esta 5 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Esta 5:1-14

Ombi La Esta Kwa Mfalme

15:1 Eze 16:13; Mit 21:1Siku ya tatu, Esta alivaa mavazi yake ya kimalkia, naye akasimama katika ua wa ndani wa jumba la mfalme, mbele ya ukumbi wa mfalme. Naye mfalme alikuwa akiketi katika kiti chake cha kifalme katika ukumbi, akielekea langoni. 2Alipomwona Malkia Esta amesimama uani alipendezwa naye, akamnyooshea fimbo ya utawala ya dhahabu ile iliyokuwa mkononi mwake. Kwa hiyo Esta alikaribia na kuigusa ncha ya fimbo ya mfalme.

35:3 Es 7:2; Mk 6:23Kisha mfalme aliuliza, “Malkia Esta, ni nini? Ombi lako ni nini? Hata kama ni nusu ya ufalme, utapewa.”

4Esta akajibu, “Kama itampendeza mfalme, mfalme pamoja na Hamani waje leo katika karamu ambayo nimeiandaa kwa ajili yake.”

5Mfalme akasema, “Mleteni Hamani mara moja, ili tupate kufanya lile Esta analoomba.”

Kwa hiyo mfalme na Hamani walihudhuria karamu aliyoiandaa Esta. 65:6 Dan 5:16Walipokuwa wakinywa mvinyo mfalme akamuuliza Esta tena, “Sasa haja yako ni nini? Utapewa. Ombi lako ni nini? Hata nusu ya ufalme, utapewa.”

7Esta akajibu, “Haja yangu na ombi langu ni hili: 85:8 Es 2:15; 1Fal 3:15Kama mfalme ameona vyema, nami nimepata kibali kwake na kama ikimpendeza mfalme kunipa ombi langu na kunitimizia haja yangu, mfalme na Hamani waje kwangu kesho katika karamu nitakayowaandalia. Kisha nitajibu swali la mfalme.”

Ghadhabu Ya Hamani Dhidi Ya Mordekai

95:9 Mit 14:17Hamani alitoka siku hiyo kwa furaha na moyo mchangamfu. Lakini alipomwona Mordekai langoni mwa mfalme na kuona kwamba hakusimama wala hakuonyesha hofu mbele yake, alijawa na ghadhabu dhidi ya Mordekai. 105:10 Es 6:13Hata hivyo, Hamani alijizuia akaenda zake nyumbani.

Akawaita pamoja rafiki zake na Zereshi, mkewe. 115:11 Mit 13:16; Es 9:10, 13Hamani akajisifia kwao juu ya utajiri wake mwingi, wanawe wengi na kwa njia zote ambazo mfalme amemheshimu kwazo na jinsi alivyomweka juu ya wakuu na maafisa wengine. 12Hamani akaongeza, “Si hayo tu. Mimi ndiye mtu pekee ambaye Malkia Esta amemwalika kumsindikiza mfalme kwenye karamu aliyomwandalia. Naye amenialika pamoja na mfalme kesho. 13Lakini haya yote hayanipi kuridhika iwapo ninaendelea kumwona yule Myahudi Mordekai akiketi kwenye lango la mfalme.”

145:14 Es 7:9; Ezr 6:11Zereshi mkewe na rafiki zake wote wakamwambia, “Tengeneza mahali pa kuangika watu kimo chake dhiraa hamsini,5:14 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. kisha kesho asubuhi mwombe mfalme Mordekai aangikwe juu yake. Ndipo uende na mfalme kwenye karamu kwa furaha.” Shauri hili lilimpendeza Hamani, naye akajenga mahali pa kuangika watu.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以斯帖记 5:1-14

以斯帖为王和哈曼设宴

1第三天,以斯帖身穿朝服进入王宫内院,面对大殿站立,王在殿里正面朝宫门坐在宝座上。 2王见以斯帖王后站在院内,就施恩给她,向她伸出手中的金杖,以斯帖便上前摸杖头。 3王问道:“以斯帖王后啊,你有什么事?你有何要求?就是半壁江山,也必赐给你!” 4以斯帖回答说:“王若愿意,就请王今天带哈曼来赴我预备的宴席。” 5王说:“快召哈曼来,我们好照以斯帖的话做。”于是王带着哈曼以斯帖预备的宴席。 6席间,王对以斯帖说:“你要什么?我必赐给你。你有何要求?就是半壁江山,也必为你成就。” 7以斯帖回答说:“王啊,我所要、我所求的就是, 8我若得到王的恩宠,王若愿意赐我所要所求的,就请王明天带哈曼再来赴我预备的宴席,到时我一定向王禀明。”

哈曼图谋杀末底改

9那天哈曼出来,心中欢喜快乐。但他看见末底改在宫门前既不起身,也不对他表示畏惧,心中十分恼火。 10哈曼忍怒回到家中,把朋友和妻子细利斯叫来, 11向他们夸耀自己的荣华富贵和儿孙满堂,以及王怎样擢升他,使他位极人臣。 12哈曼又说:“还有,以斯帖王后只请了我随王赴她预备的宴席。她还请我明天随王赴宴。 13但只要我看见犹太末底改坐在宫门口,这一切对我都毫无意义。” 14他妻子细利斯和他所有的朋友对他说:“你可以叫人做一个二十三米高的木架,明天早上求王将末底改吊在上面,然后你可以快乐地随王去赴宴。”哈曼喜欢这个提议,就叫人做了木架。