Esta 5 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Esta 5:1-14

Ombi La Esta Kwa Mfalme

15:1 Eze 16:13; Mit 21:1Siku ya tatu, Esta alivaa mavazi yake ya kimalkia, naye akasimama katika ua wa ndani wa jumba la mfalme, mbele ya ukumbi wa mfalme. Naye mfalme alikuwa akiketi katika kiti chake cha kifalme katika ukumbi, akielekea langoni. 2Alipomwona Malkia Esta amesimama uani alipendezwa naye, akamnyooshea fimbo ya utawala ya dhahabu ile iliyokuwa mkononi mwake. Kwa hiyo Esta alikaribia na kuigusa ncha ya fimbo ya mfalme.

35:3 Es 7:2; Mk 6:23Kisha mfalme aliuliza, “Malkia Esta, ni nini? Ombi lako ni nini? Hata kama ni nusu ya ufalme, utapewa.”

4Esta akajibu, “Kama itampendeza mfalme, mfalme pamoja na Hamani waje leo katika karamu ambayo nimeiandaa kwa ajili yake.”

5Mfalme akasema, “Mleteni Hamani mara moja, ili tupate kufanya lile Esta analoomba.”

Kwa hiyo mfalme na Hamani walihudhuria karamu aliyoiandaa Esta. 65:6 Dan 5:16Walipokuwa wakinywa mvinyo mfalme akamuuliza Esta tena, “Sasa haja yako ni nini? Utapewa. Ombi lako ni nini? Hata nusu ya ufalme, utapewa.”

7Esta akajibu, “Haja yangu na ombi langu ni hili: 85:8 Es 2:15; 1Fal 3:15Kama mfalme ameona vyema, nami nimepata kibali kwake na kama ikimpendeza mfalme kunipa ombi langu na kunitimizia haja yangu, mfalme na Hamani waje kwangu kesho katika karamu nitakayowaandalia. Kisha nitajibu swali la mfalme.”

Ghadhabu Ya Hamani Dhidi Ya Mordekai

95:9 Mit 14:17Hamani alitoka siku hiyo kwa furaha na moyo mchangamfu. Lakini alipomwona Mordekai langoni mwa mfalme na kuona kwamba hakusimama wala hakuonyesha hofu mbele yake, alijawa na ghadhabu dhidi ya Mordekai. 105:10 Es 6:13Hata hivyo, Hamani alijizuia akaenda zake nyumbani.

Akawaita pamoja rafiki zake na Zereshi, mkewe. 115:11 Mit 13:16; Es 9:10, 13Hamani akajisifia kwao juu ya utajiri wake mwingi, wanawe wengi na kwa njia zote ambazo mfalme amemheshimu kwazo na jinsi alivyomweka juu ya wakuu na maafisa wengine. 12Hamani akaongeza, “Si hayo tu. Mimi ndiye mtu pekee ambaye Malkia Esta amemwalika kumsindikiza mfalme kwenye karamu aliyomwandalia. Naye amenialika pamoja na mfalme kesho. 13Lakini haya yote hayanipi kuridhika iwapo ninaendelea kumwona yule Myahudi Mordekai akiketi kwenye lango la mfalme.”

145:14 Es 7:9; Ezr 6:11Zereshi mkewe na rafiki zake wote wakamwambia, “Tengeneza mahali pa kuangika watu kimo chake dhiraa hamsini,5:14 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. kisha kesho asubuhi mwombe mfalme Mordekai aangikwe juu yake. Ndipo uende na mfalme kwenye karamu kwa furaha.” Shauri hili lilimpendeza Hamani, naye akajenga mahali pa kuangika watu.

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Есфирь 5:1-14

Пир у Есфири

1И вот на третий день Есфирь надела свои царские одежды и встала во внутреннем дворе дворца, напротив царского тронного зала. Царь сидел на своём троне в зале, лицом к входу. Когда он увидел стоявшую во дворе царицу Есфирь, он смилостивился над ней 2и протянул к ней золотой скипетр, который был у него в руке. Есфирь подошла и коснулась конца скипетра.

3Царь спросил её:

– Что тебе, царица Есфирь? О чём ты просишь? Всё тебе будет, даже полцарства.

4– Если царю угодно, – ответила Есфирь, – то пусть царь вместе с Аманом придут сегодня на пир, который я для него устроила.

5– Немедленно сходите за Аманом, – сказал царь, – чтобы нам исполнить просьбу Есфири.

Так царь с Аманом пошли на пир, который устроила Есфирь. 6Когда они пили вино, царь спросил у Есфири:

– Чего же ты хочешь? Всё тебе будет. Какова твоя просьба? Даже полцарства – всё получишь!

7Есфирь ответила:

– Моё желание и моя просьба таковы: 8если я нашла у царя расположение, и если царю угодно даровать мне то, чего я хочу, и исполнить мою просьбу, то пусть царь с Аманом придут и завтра на пир, который я для них устрою. Тогда я и отвечу на царский вопрос.

План Амана погубить Мардохея

9Аман вышел в тот день весёлый и в прекрасном настроении. Но, увидев у царских ворот Мардохея и заметив, что он не встал и не выказал перед ним страха, он разозлился на него. 10Однако Аман сдержался и пошёл домой. Собрав вместе своих друзей и свою жену Зерешь, 11Аман хвастался им своим огромным богатством, множеством сыновей и всеми почестями, которыми удостоил его царь, и тем, как он возвысил его над всеми сановниками и чиновниками.

12– Но это ещё не всё, – добавил Аман. – Я единственный, кого царица Есфирь пригласила вместе с царём на пир, который она устроила. Она пригласила меня вместе с царём и на завтра. 13Но меня это не радует, пока я вижу иудея Мардохея, сидящего у царских ворот.

14Его жена Зерешь и все друзья сказали ему:

– Вели построить виселицу высотой в двадцать два метра5:14 Букв.: «пятидесяти локтей»., и утром попроси царя, чтобы Мардохея повесили на ней. А потом спокойно иди с царём на пир.

Этот совет понравился Аману, и он велел построить виселицу.