Esta 2 – NEN & TNCV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Esta 2:1-23

Esta Afanywa Malkia

1Baadaye, wakati hasira ya Mfalme Ahasuero ilikuwa imetulia, alimkumbuka Vashti na kile alichokuwa amekifanya na alilokuwa ameamuru juu yake. 2Kisha watumishi waliomhudumia mfalme walipendekeza, “Na ufanyike utafiti kwa ajili ya wanawali mabikira wazuri wa sura kwa ajili ya mfalme. 3Mfalme na ateue maafisa katika kila jimbo la himaya yake kuwaleta hao wanawali wote wazuri wa sura katika nyumba ya wanawake katika ngome ya mji wa Shushani. Kisha wawekwe chini ya utunzaji wa Hegai, towashi wa mfalme, msimamizi wa wanawake; na wapewe matunzo yote ya urembo. 4Kisha yule ambaye atampendeza mfalme na awe malkia badala ya Vashti.” Shauri hili likampendeza mfalme, naye akalifuata.

52:5 1Sam 9:1Basi katika mji wa ngome ya Shushani palikuwa na Myahudi wa kabila ya Benyamini, jina lake Mordekai mwana wa Yairi, mwana wa Shimei, mwana wa Kishi, 62:6 2Fal 24:15ambao walichukuliwa uhamishoni kutoka Yerusalemu na Mfalme Nebukadneza wa Babeli, wakiwa miongoni mwa waliochukuliwa mateka pamoja na Mfalme Yekonia wa Yuda. 72:7 Mwa 41:45; 39:6Mordekai alikuwa na binamu yake msichana aliyeitwa Hadasa, ambaye alimlea kwa kuwa hakuwa na baba wala mama. Msichana huyu, ambaye pia alijulikana kwa jina la Esta, alikuwa na umbo na sura ya kupendeza, naye Mordekai alimtunza kama binti yake mwenyewe baada ya baba yake na mama yake kufariki.

8Wakati agizo na amri ya mfalme lilitangazwa, wanawali wengi waliletwa kwenye ngome ya mji wa Shushani na kuwekwa chini ya uangalizi wa Hegai. Pia Esta alipelekwa katika jumba la mfalme na akakabidhiwa Hegai, aliyekuwa mkuu wa nyumba ya wanawake. 92:9 1Sam 9:22-24; Eze 16:9-13Msichana huyu alimpendeza na kupata kibali mbele zake. Mara moja akaanza kumpa matunzo ya uzuri na chakula maalum. Alimpa Esta vijakazi saba waliochaguliwa kutoka jumba la kifalme, na kumhamishia yeye pamoja na vijakazi wake katika sehemu bora zaidi katika nyumba ya wanawake.

102:10 Es 2:20Esta alikuwa hajadhihirisha uraia wala kabila lake, kwa sababu Mordekai alikuwa amemkataza. 11Kila siku Mordekai alikuwa akitembeatembea karibu na ua wa nyumba ya wanawake kujua Esta alivyoendelea na kuona yaliyokuwa yakitendeka kwake.

122:12 Mit 27:9; Isa 3:24Kabla zamu ya msichana haijafika ya kwenda kwa Mfalme Ahasuero, ilimbidi atimize miezi kumi na miwili ya matunzo ya urembo kama ilivyokuwa imepangwa. Kwa miezi sita walikuwa wajipake mafuta ya manemane, na miezi sita kujipaka manukato na vipodozi. 13Basi hivi ndivyo ambavyo msichana angeingia kwa mfalme: Kila kitu alichohitaji aliruhusiwa kuchukua kutoka nyumba ya wanawake na kwenda navyo katika jumba la mfalme. 142:14 1Fal 11:3; Dan 5:2Jioni angekwenda pale na asubuhi kurudi sehemu nyingine ya nyumba ya wanawake katika utunzaji wa Shaashgazi, towashi wa mfalme ambaye alikuwa mkuu wa masuria. Hangeweza kurudi kwa mfalme mpaka apendezwe naye na kuagiza aitwe kwa jina lake.

152:15 Za 45:14; Mwa 18:3Zamu ya Esta ilipofika kwenda kwa mfalme (msichana ambaye Mordekai alikuwa amemlea, binti wa Abihaili mjomba wake), Esta hakutaka vitu zaidi ya vile ambavyo Hegai, towashi wa mfalme aliyekuwa mkuu wa nyumba ya wanawake alivyokuwa amemshauri. Naye Esta alipata kibali kwa kila mtu aliyemwona. 16Esta alipelekwa kwa Mfalme Ahasuero katika makao ya mfalme mwezi wa kumi, yaani mwezi wa Tebethi, katika mwaka wake wa saba wa kutawala.

17Basi ikawa mfalme alivutiwa na Esta kuliko wanawake wengine wote, naye akapata upendeleo na kibali kuliko mabikira wengine. Kisha akamvika taji la kifalme kichwani mwake na kumfanya malkia badala ya Vashti. 182:18 1Fal 3:15; Es 1:7Mfalme akafanya karamu kubwa, karamu ya Esta, kwa wakuu wake wote na maafisa. Mfalme alitangaza mapumziko katika majimbo yake yote na kugawa zawadi kwa ukarimu wa kifalme.

Mordekai Afunua Hila

192:19 Es 4:2Wakati mabikira walikusanyika mara ya pili, Mordekai alikuwa ameketi katika lango la mfalme. 20Lakini Esta alikuwa ameficha siri ya kabila lake na uraia wake, kama Mordekai alivyokuwa amemwambia, kwa maana aliendelea kufuata maelekezo ya Mordekai kama alivyokuwa akifanya alipokuwa akimlea.

21Wakati Mordekai alikuwa ameketi kwenye lango la mfalme, Bigthana na Tereshi, maafisa wawili wa mfalme waliokuwa walinzi wa lango, walikasirika na kupanga njama ya kumuua Mfalme Ahasuero. 22Lakini Mordekai aligundua hila hii na kumwambia Malkia Esta, ambaye baadaye alimwarifu mfalme, huku akimsifu Mordekai. 232:23 Mwa 40:19; Mhu 10:8Taarifa hiyo ilipochunguzwa na kuonekana kuwa kweli, maafisa hao wawili waliangikwa juu ya miti ya kunyongea. Haya yote yaliandikwa katika kitabu cha kumbukumbu mbele ya mfalme.

Thai New Contemporary Bible

เอสเธอร์ 2:1-23

เอสเธอร์ได้รับเลือกเป็นราชินี

1ต่อมาเมื่อพระพิโรธของกษัตริย์เซอร์ซีสสงบลงแล้ว พระองค์ทรงคิดถึงพระนางวัชที ตลอดจนสิ่งที่พระนางได้ทำและพระราชโองการของพระองค์เองเกี่ยวกับพระนาง 2แล้วข้าราชบริพารส่วนพระองค์จึงทูลเสนอว่า “ควรเฟ้นหาหญิงสาวพรหมจารีผู้งดงามมาถวายกษัตริย์ 3ขอทรงตั้งเจ้าพนักงานในแต่ละมณฑลของอาณาจักรของพระองค์ให้เฟ้นหาตัวหญิงสาวโฉมงามทั้งหมด และนำตัวมายังฮาเร็มในป้อมเมืองสุสา ให้อยู่ในความดูแลของเฮกัยขันทีของกษัตริย์ซึ่งรับผิดชอบเกี่ยวกับเหล่าสตรี และให้พวกนางรับการประทินโฉม 4หลังจากนั้นให้สตรีซึ่งฝ่าพระบาทโปรดปรานเป็นราชินีแทนพระนางวัชที” กษัตริย์ก็พอพระทัยความคิดนี้และให้ลงมือปฏิบัติ

5ครั้งนั้นในป้อมเมืองสุสา มีชายชาวยิวจากเผ่าเบนยามินคนหนึ่งชื่อโมรเดคัย ผู้เป็นบุตรของยาอีร์ ผู้เป็นบุตรของชิเมอี ผู้เป็นบุตรของคีช 6เขาถูกจับมาเป็นเชลยเมื่อครั้งกษัตริย์เนบูคัดเนสซาร์แห่งบาบิโลนทรงกวาดต้อนเชลยมาจากเยรูซาเล็มพร้อมกษัตริย์เยโฮยาคีน2:6 ภาษาฮีบรูว่าเยโคนิยาห์เป็นอีกรูปหนึ่งของเยโฮยาคีนแห่งยูดาห์ 7โมรเดคัยมีลูกพี่ลูกน้องเป็นหญิงสาวรูปโฉมงามน่ารักชื่อ ฮาดัสสาห์หรือเอสเธอร์ เขาเลี้ยงดูนางเป็นบุตรสาวบุญธรรมหลังจากที่บิดามารดาของนางสิ้นชีวิต

8เนื่องด้วยพระราชโองการของกษัตริย์ หญิงสาวหลายคนจึงถูกนำมาอยู่ที่ป้อมเมืองสุสาในความดูแลของเฮกัย และเอสเธอร์ก็ถูกนำมาที่พระราชวังของกษัตริย์และอยู่ในความดูแลของเฮกัยผู้ดูแลฮาเร็มเช่นกัน 9เฮกัยเอ็นดูและพอใจเอสเธอร์มาก เขาจึงรีบจัดหาเครื่องประทินโฉมและอาหารพิเศษให้นางทันที ทั้งจัดเด็กหญิงเจ็ดคนซึ่งคัดเลือกจากพระราชวังมาคอยรับใช้นาง และให้นางกับสาวใช้ย้ายไปอยู่ที่ที่ดีที่สุดในฮาเร็ม

10เอสเธอร์ไม่ได้เปิดเผยเรื่องเชื้อชาติและภูมิหลังครอบครัวของนางเพราะโมรเดคัยสั่งห้ามไว้ 11ทุกวันโมรเดคัยจะเดินวนเวียนแถวๆ ลานฮาเร็ม เพื่อถามข่าวคราวและความเป็นไปของเอสเธอร์

12ก่อนถึงเวรที่หญิงสาวแต่ละคนเข้าเฝ้ากษัตริย์เซอร์ซีส พวกนางจะต้องรับการประทินโฉมครบสิบสองเดือนตามที่กำหนดไว้คือ หกเดือนแรกบำรุงด้วยน้ำมันมดยอบ จากนั้นบำรุงด้วยน้ำหอมและเครื่องประทินผิวอีกหกเดือน 13เมื่อถึงรอบที่แต่ละคนจะเข้าเฝ้ากษัตริย์ จะขอนำอะไรจากฮาเร็มไปพระราชวังด้วยก็ได้ 14ในเวลาเย็นนางจะเข้าวัง และเช้าวันรุ่งขึ้นจะกลับไปอยู่อีกตำหนักหนึ่งในฮาเร็มซึ่งอยู่ในความดูแลของชาอัชกาสขันทีของกษัตริย์ผู้คอยดูแลพวกสนม นางจะไม่ได้เฝ้ากษัตริย์อีกเว้นเสียแต่ว่าพระองค์ทรงโปรดและเอ่ยนามเรียกตัวนางมาเข้าเฝ้า

15เมื่อถึงรอบของเอสเธอร์ที่จะเข้าเฝ้ากษัตริย์ (หญิงสาวที่โมรเดคัยรับเป็นบุตรบุญธรรม นางเป็นบุตรสาวของอาบีฮายิล ผู้เป็นลุงของโมรเดคัย) นางไม่ได้ขอสิ่งใดนอกจากที่ขันทีเฮกัยผู้ดูแลฮาเร็มแนะนำ และทุกคนที่เห็นเอสเธอร์ก็ชื่นชอบนาง 16เอสเธอร์ถูกนำมาเข้าเฝ้ากษัตริย์เซอร์ซีสในพระราชวังเมื่อเดือนเทเบท ซึ่งเป็นเดือนที่สิบปีที่เจ็ดแห่งรัชกาล

17กษัตริย์พอพระทัยเอสเธอร์มากกว่าหญิงอื่นทั้งปวง พระองค์โปรดปรานและพอพระทัยนางมากกว่าหญิงพรหมจารีคนอื่นๆ จึงสวมมงกุฎให้และตั้งนางเป็นราชินีแทนพระนางวัชที 18และกษัตริย์ทรงจัดงานเลี้ยงใหญ่ประทานแก่ขุนนางและข้าราชบริพารทั้งปวงเพื่อเอสเธอร์ พระองค์ทรงประกาศวันหยุดทั่วทุกมณฑล และประทานของขวัญด้วยพระทัยกว้างขวาง

โมรเดคัยทูลเรื่องแผนการของคนร้าย

19เมื่อมีการเฟ้นตัวหญิงสาวพรหมจารีครั้งที่สอง โมรเดคัยนั่งประจำอยู่ที่ประตูพระราชวัง 20แต่เอสเธอร์ยังคงไม่เปิดเผยเชื้อชาติและภูมิหลังครอบครัวของพระนางตามที่โมรเดคัยสั่งไว้ พระนางยังคงปฏิบัติตามคำสั่งของโมรเดคัยเหมือนตอนที่เขายังเลี้ยงดูพระนาง

21ในช่วงที่โมรเดคัยนั่งประจำอยู่ที่ประตูพระราชวัง ข้าราชการสองคนซึ่งเป็นยามเฝ้าประตู คือบิกธานา2:21 ภาษาฮีบรูว่าบิกธานเป็นอีกรูปหนึ่งของบิกธานาและเทเรช มีเรื่องแค้นเคืองและคบคิดกันจะลอบปลงพระชนม์กษัตริย์เซอร์ซีส 22แต่โมรเดคัยล่วงรู้และนำความไปแจ้งพระนางเอสเธอร์ พระนางจึงขึ้นกราบทูลกษัตริย์และทูลว่าเป็นความดีความชอบของโมรเดคัย 23มีการสอบสวนเรื่องนี้และพบว่าเป็นความจริง ข้าราชบริพารทั้งสองจึงถูกแขวนคอที่ตะแลงแกง2:23 หรือถูกแขวน(หรือถูกเสียบ)ไว้บนเสาเหมือนที่อื่นๆ ในพระธรรมเอสเธอร์ เรื่องราวทั้งหมดบันทึกอยู่ในจดหมายเหตุรัชกาลกษัตริย์เซอร์ซีส