Danieli 12 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 12:1-13

Nyakati Za Mwisho

112:1 Dan 10:13; Yud 9; Dan 9:12; Lk 10:20; Yer 17:13; Mt 24:21; Mk 13:19; Yer 30:7; Za 56:8; Kut 32:32“Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa. 212:2 Isa 26:19; Yn 5:28-29; Mt 25:46; Yn 11:24Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele. 312:3 Dan 11:33; Yn 5:35; Flp 2:15; Mit 4:18; 1Kor 15:42; Mt 13:43Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele. 412:4 Isa 8:16; Ufu 22:10; Yer 5:1Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”

512:5 Dan 10:4Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto. 612:6 Eze 9:2; Dan 8:13; Za 74:9Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”

712:7 Dan 6:26; Ufu 10:5-7; Lk 21:24; Dan 8:24; 8:24; Ufu 11:2; Mwa 14:22Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati.12:7 Wakati, nyakati mbili na nusu wakati maana yake mwaka mmoja, miaka miwili, na nusu mwaka, yaani miaka mitatu na nusu. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”

8Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”

912:9 Isa 29:11Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho. 1012:10 Isa 1:25; Zek 13:9; Hos 14:9; Isa 32:7; Ufu 22:11; Dan 11:35Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.

1112:11 Mk 13:14; Dan 8:11; 9:27; Mt 24:15; Kut 29:38; Ufu 11:2“Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290. 1212:12 Isa 30:18; Eze 4:5-6; Dan 8:14Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.

1312:13 Isa 57:2“Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”

Swedish Contemporary Bible

Daniel 12:1-13

Profetia över tidens slut

1Då träder Mikael fram, den store fursten som beskyddar ditt folk. Det blir en tid av nöd som aldrig funnits sedan folken blev till, ända till den tiden. Men då ska ditt folk räddas, alla som är uppskrivna i boken. 2De många som sover i jordens mull ska vakna, en del till evigt liv och andra till skam och evig fasa. 3De insiktsfulla ska lysa som himlens ljus, och de som leder många till rättfärdighet ska stråla som stjärnorna i evigheters evigheter. 4Men du, Daniel, bevara dessa ord som en hemlighet och försegla boken fram till ändens tid. Många kommer att gå hit och dit, men kunskapen ska öka.”

5Då såg jag, Daniel, två andra stå där, en på vardera sidan om floden. 6En av dem frågade mannen i linnekläderna, han som nu fanns ovanför flodens vatten: ”Hur länge ska slutet dröja, innan dessa besynnerliga ting fullbordas?”

7Jag lyssnade till mannen i linnekläderna, han som fanns ovanför flodens12:7 Tigris vatten, och med båda händerna lyfta mot himlen avlade han en ed vid honom som lever för evigt: ”Det dröjer ännu en tid, två tider och en halv tid.12:7 Se not till 7:25. När det heliga folkets makt är krossad12:7 En tänkbar alternativ översättning är: När den makt är krossad som krossat det heliga folket…, då fullbordas allt detta.”

8Jag hörde detta men förstod det inte, så jag frågade: ”Min herre, hur kommer alltsammans att sluta?”

9Han svarade: ”Gå nu, Daniel, för orden ska hållas hemliga och förseglade fram till ändens tid. 10Många kommer att renas, luttras och förädlas, medan de gudlösa ska fortsätta med sin gudlöshet, utan att förstå något. Bara de insiktsfulla ska förstå det.

11Från den tid det dagliga offret avskaffas och den vanhelgande vidrigheten blir uppsatt kommer det att gå 1 290 dagar. 12Lycklig är den som väntar och når fram till 1 335 dagar.

13Men gå nu vidare mot slutet. Du ska få vila och sedan stå upp till din del vid tidens slut.”