Ayubu 41 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 41:1-34

141:1 Za 104:26; Isa 27:1“Je, waweza kumvua Lewiathani41:1 Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa. kwa ndoano ya samaki,

au kufunga ulimi wake kwa kamba?

241:2 Isa 37:29; Eze 19:4; Isa 30:28Waweza kupitisha kamba puani mwake,

au kutoboa taya lake kwa kulabu?

341:3 1Fal 20:31Je, ataendelea kukuomba umhurumie?

Atasema nawe maneno ya upole?

441:4 Kut 21:6Je, atafanya agano nawe ili umtwae

awe mtumishi wako maisha yake yote?

5Je, utamfuga na kumfanya rafiki kama ndege,

au kumfunga kamba kwa ajili ya wasichana wako?

6Je, wafanyabiashara watabadilishana bidhaa kwa ajili yake?

Watamgawanya miongoni mwa wafanyao biashara?

741:7 Ay 40:24Je, waweza kuijaza ngozi yake kwa vyuma vyenye ncha kali,

au kichwa chake kwa mkuki wa kuvulia samaki?

841:8 Ay 3:8Kama ukiweka mkono wako juu yake,

utavikumbuka hivyo vita na kamwe hutarudia tena!

941:9 Ay 40:16Tumaini lolote la kumtiisha ni kujidanganya;

kule kumwona tu kunamwangusha mtu chini.

1041:10 Ay 3:8; 2Nya 20:6; Ufu 6:17; 1Kor 10:22Hakuna yeyote aliye mkali athubutuye kumchokoza.

Ni nani basi awezaye kusimama dhidi yangu?

1141:11 Ay 34:33; Yos 3:11; Rum 11:35; Mdo 4:24; Mwa 14:19; Kum 10:14Ni nani mwenye madai dhidi yangu ili nipate kumlipa?

Kila kitu kilicho chini ya mbingu ni mali yangu.

1241:12 Ay 40:18; 39:11“Sitashindwa kunena juu ya maungo yake,

nguvu zake na umbo lake zuri.

1341:13 Ay 30:11; 39:10Ni nani awezaye kumvua gamba lake la nje?

Ni nani awezaye kumsogelea na lijamu?

1441:14 Za 22:13Nani athubutuye kuufungua mlango wa kinywa chake,

kilichozungukwa na meno yake ya kutisha pande zote?

1541:15 Ay 40:17Mgongo wake una safu za ngao

zilizoshikamanishwa imara pamoja;

16kila moja iko karibu sana na mwenzake,

wala hakuna hewa iwezayo kupita kati yake.

17Zimeunganishwa imara kila moja na nyingine;

zimengʼangʼaniana pamoja wala haziwezi kutenganishwa.

1841:18 Ay 40:17Akipiga chafya mwanga humetameta;

macho yake ni kama mionzi ya mapambazuko.

1941:19 Dan 10:6Mienge iwakayo humiminika kutoka kinywani mwake;

cheche za moto huruka nje.

2041:20 Za 18:8Moshi hufuka kutoka puani mwake,

kama kutoka kwenye chungu kinachotokota kwa moto wa matete.

2141:21 Ay 4:9; Isa 11:4; 10:17; Yer 4:4Pumzi yake huwasha makaa ya mawe,

nayo miali ya moto huruka kutoka kinywani mwake.

2241:22 Ay 39:11Nguvu hukaa katika shingo yake;

utisho hutangulia mbele yake.

23Mikunjo ya nyama yake imeshikamana imara pamoja;

iko imara na haiwezi kuondolewa.

2441:24 Mt 18:6Kifua chake ni kigumu kama mwamba,

kigumu kama jiwe la chini la kusagia.

2541:25 Ay 39:20; 3:8Ainukapo, mashujaa wanaogopa;

hurudi nyuma mbele yake anapokwenda kwa kishindo.

2641:26 Ay 8:18; 40:24Upanga unaomfikia haumdhuru,

wala mkuki au mshale wala fumo.

2741:27 Ay 41:29Chuma hukiona kama unyasi,

na shaba kama mti uliooza.

2841:28 Za 91:5Mishale haimfanyi yeye akimbie;

mawe ya kombeo kwake ni kama makapi.

2941:29 Ay 41:27; 5:22Rungu kwake huwa kama kipande cha jani kavu;

hucheka sauti za kugongana kwa mkuki.

3041:30 Isa 28:27; Amo 1:3; Isa 41:15Sehemu zake za chini kwenye tumbo

zina menomeno na mapengo kama vigae vya chungu,

zikiacha mburuzo kwenye matope

kama chombo chenye meno cha kupuria.

3141:31 1Sam 2:14; Eze 32:2Huvisukasuka vilindi kama sufuria kubwa ichemkayo,

na kukoroga bahari kama chungu cha marhamu.

32Anapopita nyuma yake huacha mkondo unaometameta;

mtu angedhani vilindi vilikuwa na mvi.

3341:33 Ay 40:19Hakuna chochote duniani kinacholingana naye:

yeye ni kiumbe kisicho na woga.

3441:34 Ay 28:8Yeye huwatazama chini wale wote wenye kujivuna;

yeye ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約伯記 41:1-34

1「你豈能用魚鉤釣鱷魚,

用繩索綁住牠的舌頭?

2你豈能用繩子穿牠的鼻子,

用鉤子穿牠的腮骨?

3牠豈會向你連連求饒,

對你說柔和的話?

4牠豈肯與你立約,

一生做你的奴隸?

5你豈能拿牠當小鳥玩耍,

或拴起來給幼女取樂?

6漁夫們豈能把牠當貨物出售,

賣給商人?

7你豈能在牠皮上戳滿長矛,

頭上插滿魚叉?

8你動手碰碰牠,

就知道有何惡戰,絕不會再碰。

9企圖捕捉牠的都會失望,

人看到牠就會心驚膽戰。

10再兇猛的人也不敢惹牠。

這樣,誰能在我面前站立得住?

11誰給過我什麼,要我償還?

天下萬物都是我的。

12「論到牠的四肢、大力和姣美的身體,

我不能緘默不言。

13誰能剝去牠的外皮?

誰能給牠戴上轡頭?

14誰能打開牠的口?

牠的牙齒令人恐懼。

15牠的脊背覆著行行鱗甲,

牢牢地密封在一起,

16緊密無間,

連氣也透不進去。

17鱗甲彼此相連相扣,

無法分開。

18牠打噴嚏時,水光四射;

牠的眼睛發出晨光;

19口中噴出火炬,

迸出火星;

20鼻孔冒煙,

如沸騰的鍋和燃燒的蘆葦;

21呼氣可點燃煤炭,

口中噴出火焰;

22頸項強而有力,

恐懼在牠前面開路;

23身上的皺褶緊密相連,

牢牢地密封在一起;

24心堅如石,

硬如磨石。

25牠一站起來,勇士都害怕,

見牠衝來,他們慌忙退縮。

26刀劍擋不住牠,

長矛、標槍、尖戟也無能為力。

27牠視鐵如乾草,

視銅如朽木。

28利箭嚇不跑牠,

彈石在牠看來只是碎稭;

29棍棒無異於稭稈,

牠嗤笑投來的標槍。

30牠腹部有鋒利的瓦片,

在淤泥上留下道道耙痕。

31牠使深淵如鍋翻騰,

大海如油鍋滾動。

32牠游過後留下一道波光,

使深淵彷彿披上銀髮。

33地上沒有動物能與牠相比,

像牠那樣無所畏懼。

34牠藐視群雄,

在高傲的百獸中稱王。」