Ayubu 40 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 40:1-24

140:1 Ay 5:8; 13:3; 13:3; 9:15; 9:3; 11:8; 33:13Bwana akamwambia Ayubu:

240:2 Rum 9:20“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha?

Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”

3Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:

440:4 Ay 42:6; Amu 18:19; Ay 29:9; Ezr 9:6; Zek 2:13“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe?

Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.

540:5 Ay 9:3; 9:15Nimesema mara moja, lakini sina jibu;

naam, nimesema mara mbili,

lakini sitasema tena.”

640:6 Kut 14:21; Ay 38:1Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:

740:7 Ay 38:3“Jikaze kama mwanaume;

nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.

840:8 Ay 15:25; Rum 3:3; Za 51:4“Je, utabatilisha hukumu yangu?

Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?

940:9 2Nya 32:8; Za 98:1; Kut 20:19; Za 29:3-4Je, una mkono kama wa Mungu,

nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?

1040:10 Za 29:1-2; 45:3; 93:1; 96:6; 104:1; 145:5Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari,

nawe uvae heshima na enzi.

1140:11 Nah 1:6; Sef 1:18; Za 18:27; Isa 32:19Fungulia ukali wa ghadhabu yako,

mtafute kila mwenye kiburi umshushe,

1240:12 Za 52:5; 1Pet 5:5; Dan 5:20; Mal 4:3; Lk 18:14mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze,

waponde waovu mahali wasimamapo.

1340:13 Hes 16:31-34; Ay 4:9Wazike wote mavumbini pamoja;

wafunge nyuso zao kaburini.

1440:14 Kut 15:6; Isa 63:5Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia

kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.

1540:15 Ay 9:9; Isa 11:7; 65:25“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi,40:15 Huyu alikuwa mnyama wa nyakati za zamani ambaye hajulikani hasa ni gani.

niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe,

anayekula majani kama ngʼombe.

1640:16 Ay 39:11; 41:9Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake,

uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!

1740:17 Ay 41:15Mkia wake hutikisika kama mwerezi;

mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.

1840:18 Ay 41:12; Isa 11:4; 49:2Mifupa yake ni bomba za shaba,

maungo yake ni kama fito za chuma.

1940:19 Za 40:5; Isa 27:1Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu,

lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.

2040:20 Za 104:14, 26Vilima humletea yeye mazao yake,

nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.

2140:21 Mwa 41:2; Za 68:30; Isa 35:7; Ay 8:11Hulala chini ya mimea ya yungiyungi,

katika maficho ya matete kwenye matope.

2240:22 Za 1:3; Isa 44:4Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake;

miti mirefu karibu na kijito humzunguka.

23Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu;

yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.

2440:24 2Fal 19:28; Isa 37:29Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho,

au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

Ketab El Hayat

أيوب 40:1-24

1وَاسْتَطْرَدَ الرَّبُّ قَائِلاً لأَيُّوبَ: 2«أَيُخَاصِمُ اللّائِمُ الْقَدِيرَ؟ لِيُجِبِ المُشْتَكِي عَلَى اللهِ».

3عِنْدَئِذٍ أَجَابَ أَيُّوبُ الرَّبَّ:

4«انْظُرْ، أَنَا حَقِيرٌ فَبِمَاذَا أُجِيبُكَ؟ هَا أَنَا أَضَعُ يَدِي عَلَى فَمِي 5لَقَدْ تَكَلَّمْتُ مَرَّةً وَلَنْ أُجِيبَ، وَمَرَّتَيْنِ وَلَنْ أُضِيفَ».

6حِينَئِذٍ أَجَابَ الرَّبُّ أَيُّوبَ مِنَ الْعَاصِفَةِ: 7«اشْدُدْ حَقَوَيْكَ وَكُنْ رَجُلاً، فَأَسْأَلَكَ وَتُجِيبَنِي. 8أَتَشُكُّ فِي قَضَائِي أَوْ تَسْتَذْنِبُنِي لِتُبَرِّرَ نَفْسَكَ؟ 9أَتَمْلِكُ ذِرَاعاً كَذِرَاعِ اللهِ؟ أَتُرْعِدُ بِمِثْلِ صَوْتِهِ؟ 10إِذاً تَسَرْبَلْ بِالْجَلالِ وَالْعَظَمَةِ، وَتَزَيَّنْ بِالْمَجْدِ وَالْبَهَاءِ. 11صُبَّ فَيْضَ غَضَبِكَ، وَانْظُرْ إِلَى كُلِّ مُتَكَبِّرٍ وَاخْفِضْهُ. 12انْظُرْ إِلَى كُلِّ مُتَعَظِّمٍ وَذَلّلْهُ، وَدُسِ الأَشْرَارَ فِي مَوَاضِعِهِمْ. 13اطْمِرْهُمْ كُلَّهُمْ فِي التُّرَابِ مَعاً، وَاحْبِسْ وُجُوهَهُمْ فِي الْهَاوِيَةِ. 14عِنْدَئِذٍ أَعْتَرِفُ لَكَ بِأَنَّ يَمِينَكَ قَادِرَةٌ عَلَى إِنْقَاذِكَ.

15انْظُرْ إِلَى بَهِيمُوثَ (الْحَيَوَانِ الضَّخْمِ) الَّذِي صَنَعْتُهُ مَعَكَ، فَإِنَّهُ يَأْكُلُ الْعُشْبَ كَالْبَقَرِ.

16إِنَّ قُوَّتَهُ فِي مَتْنَيْهِ، وَشِدَّتَهُ فِي عَضَلِ بَطْنِهِ. 17يَنْتَصِبُ ذَيْلُهُ كَشَجَرَةِ أَرْزٍ، وَعَضَلاتُ فَخْذَيْهِ مَضْفُورَةٌ. 18عِظَامُهُ أَنَابِيبُ نُحَاسٍ وَأَطْرَافُهُ قُضْبَانُ حَدِيدٍ، 19إِنَّهُ أَعْجَبُ كُلِّ الْخَلائِقِ، وَلا يَقْدِرُ أَنْ يَهْزِمَهُ إِلّا الَّذِي خَلَقَهُ. 20تَنْمُو الأَعْشَابُ الَّتِي يَتَغَذَّى بِها عَلَى الْجِبَالِ، حَيْثُ تَمْرَحُ وُحُوشُ الْبَرِّيَّةِ. 21يَرْبِضُ تَحْتَ شُجَيْرَاتِ السِّدْرِ، وَبَيْنَ الْحَلْفَاءِ فِي الْمُسْتَنْقَعَاتِ. 22يَسْتَظِلُّ بِشُجَيْرَاتِ السِّدْرِ، وَبِالصَّفْصَافِ عَلَى الْمِيَاهِ الْجَارِيَةِ 23لَا يُخَامِرُهُ الْخَوْفُ إِنْ هَاجَ النَّهْرُ، وَيَظَلُّ مُطْمَئِنّاً وَلَوِ انْدَفَقَ نَهْرُ الأُرْدُنِّ فِي فَمِهِ. 24مَنْ يَقْدِرُ أَنْ يَصْطَادَهُ مِنَ الأَمَامِ، أَوْ يَثْقُبَ أَنْفَهُ بِخِزَامَةٍ؟