Ayubu 37 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 37:1-24

137:1 Za 38:10; Isa 15:5; Yer 4:19; Hab 3:16“Kwa hili moyo wangu unatetemeka,

nao unaruka kutoka mahali pake.

237:2 Za 18:13; 29:3-9Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake,

sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.

337:3 2Sam 22:13; Za 18:14; Ay 36:32; Mt 24:27; Lk 17:24Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote

na kuupeleka hata miisho ya dunia.

437:4 1Sam 2:10; Kut 20:19Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake;

Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari.

Wakati sauti yake ingurumapo tena,

huuachilia umeme wake wa radi.

537:5 Ay 11:7-9Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu;

yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.

637:6 Kum 28:12; Ay 38:22; Mwa 7:4; Ay 36:27Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’

nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

737:7 Ay 12:14; Za 111:2; 109:27; 104:19-23Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake,

yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.

837:8 Ay 28:26; 38:40; Za 104:22Wanyama hujificha;

hubakia kwenye mapango yao.

937:9 Za 50:3; 147:17Dhoruba hutoka katika chumba chake,

baridi hutoka katika upepo uendao kasi.

1037:10 Ay 38:29-30; Za 147:17Pumzi ya Mungu hutoa barafu,

eneo kubwa la maji huganda.

1137:11 Ay 26:8; 36:30; 28:26Huyasheheneza mawingu kwa maji,

naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.

1237:12 Za 147:16; 148:8; Ay 37:3Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake,

juu ya uso wa dunia yote,

kufanya lolote ayaamuruyo.

1337:13 Kut 9:22-23; 1Sam 12:17; Kut 9:18; 1Fal 18:45Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu,

au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.

1437:14 Ay 32:10; 5:9“Ayubu, sikiliza hili;

nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.

1537:15 Ay 36:30, 32Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu,

na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?

1637:16 Ay 36:29; 5:9; 36:4Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia,

hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?

1737:17 Mdo 27:13Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako

wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,

1837:18 Mwa 1:1, 8; Ay 22:14; Kum 28:23; Za 104:2je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga,

zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?

1937:19 Rum 8:26; Ay 13:18; 9:3“Tuambieni yatupasayo kumwambia;

hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.

20Je, aambiwe kwamba nataka kuongea?

Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?

2137:21 Amu 5:31; Mdo 22:1; 26:13Basi hakuna awezaye kulitazama jua,

jinsi linavyongʼaa angani,

upepo ukishafagia mawingu.

2237:22 Za 19:5; Kut 24:17Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu;

Mungu huja katika utukufu wa kutisha.

2337:23 Ay 5:9; Rum 11:33; Ay 8:3; Yer 25:5; Mao 3:33Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza;

katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.

2437:24 Mik 6:8; Mt 10:28; 11:25; Efe 5:15Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni,

kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

New International Reader’s Version

Job 37:1-24

1“When I hear the thunder, my heart pounds.

It beats faster inside me.

2Listen! Listen to the roar of his voice!

Listen to the thunder that comes from him!

3He sends his lightning across the sky.

It reaches from one end of the earth to the other.

4Next comes the sound of his roaring thunder.

He thunders with his majestic voice.

When his voice fills the air,

he doesn’t hold anything back.

5God’s voice thunders in wonderful ways.

We’ll never understand the great things he does.

6He says to the snow, ‘Fall on the earth.’

He tells the rain, ‘Pour down your mighty waters.’

7He stops everyone from working.

He wants them to see his work.

8The animals go inside.

They remain in their dens.

9The storm comes out of its storeroom in the heavens.

The cold comes from the driving winds.

10The breath of God produces ice.

The shallow water freezes over.

11He loads the clouds with moisture.

He scatters his lightning through them.

12He directs the clouds to circle

above the surface of the whole earth.

They do everything he commands them to do.

13He tells the clouds to punish people.

Or he brings them to water his earth and show his love.

14“Job, listen to me.

Stop and think about the wonderful things God does.

15Do you know how he controls the clouds?

Do you understand how he makes his lightning flash?

16Do you know how the clouds stay up in the sky?

Do you understand the wonders of the God who has perfect knowledge?

17Even your clothes are too hot for you

when the land lies quiet under the south wind.

18Can you help God spread out the skies?

They are as hard as a mirror

that’s made out of bronze.

19“Job, tell us what we should say to God.

We can’t prepare our case

because our minds are dark.

20Should he be told that I want to speak?

Would anyone ask to be destroyed by him?

21No one can look at the sun.

It’s too bright after the wind has swept the skies clean.

22Out of the north, God comes in his shining glory.

He comes in all his wonderful majesty.

23We can’t reach up to the Mighty One.

He is lifted high because of his power.

Everything he does is fair and right.

So he doesn’t crush people.

24That’s why they have respect for him.

He cares about all those who are wise.”