Ayubu 28 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 28:1-28

Mapumziko: Imani Inakopatikana

128:1 Za 12:6; 66:10; Yer 9:7; Mal 3:3; Dan 11:35“Kuna machimbo ya fedha,

na mahali dhahabu isafishwapo.

228:2 Kum 8:9Chuma hupatikana ardhini,

nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.

328:3 Mhu 7:25; 8:17; Mit 2:4Mwanadamu hukomesha giza;

huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali,

kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini

katika giza jeusi sana.

428:4 2Sam 5:8Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu,

mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu;

mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.

528:5 Mwa 1:29; Za 145:15Ardhi, ambako chakula hutoka,

chini hugeuzwa kwa moto;

628:6 Isa 54:11; Wim 5:14; Ay 22:24yakuti samawi hutoka katika miamba yake,

nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.

728:7 Ay 28:21Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika,

wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.

828:8 Ay 41:34; Isa 35:9Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga,

wala simba azungukaye huko.

928:9 Kum 8:15; Yn 2:6Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana,

na kuiacha wazi mizizi ya milima.

1028:10 Mit 2:4; Ay 28:4Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba;

macho yake huona hazina zake zote.

1128:11 Mwa 7:11; Isa 48:6; Yer 33:3Hutafuta vyanzo vya mito

na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.

1228:12 Mit 1:20; Mhu 7:24“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi?

Ufahamu unakaa wapi?

1328:13 Mit 3:15; Mt 13:44-46Mwanadamu hatambui thamani yake;

haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.

14Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’;

bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’

1528:15 Mit 16:16; Mdo 8:20Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote,

wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.

16Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri,

kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.

1728:17 Za 119:72; Mit 8:10; Ay 28:15Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo,

wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.

18Marijani na yaspi hazistahili kutajwa;

thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.

1928:19 Mit 3:14-15; 8:10-19Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo,

wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.

20“Ni wapi basi hekima itokako?

Ufahamu hukaa wapi?

2128:21 Ay 28:7Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai,

imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.

2228:22 Ay 26:6Uharibifu na Mauti husema,

‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’

2328:23 Mdo 15:18; Ay 22:22; Mit 8:22-31Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima

na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,

2428:24 Isa 11:12; Yos 3:11; Ebr 4:13; Za 66:7kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia

na huona kila kitu chini ya mbingu.

2528:25 Ay 38:8-11; Za 135:7Alipofanyiza nguvu za upepo

na kuyapima maji,

2628:26 Ay 38:25-27; Isa 35:7; Yer 14:22alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua

na njia kwa ajili ya umeme wa radi,

27ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake,

akaithibitisha na kuihakikisha.

2828:28 Kut 20:20; Kum 4:6Naye Mungu akamwambia mwanadamu,

‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima,

nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’ ”

King James Version

Job 28:1-28

1Surely there is a vein for the silver, and a place for gold where they fine it.28.1 vein: or, mine 2Iron is taken out of the earth, and brass is molten out of the stone.28.2 earth: or, dust 3He setteth an end to darkness, and searcheth out all perfection: the stones of darkness, and the shadow of death. 4The flood breaketh out from the inhabitant; even the waters forgotten of the foot: they are dried up, they are gone away from men. 5As for the earth, out of it cometh bread: and under it is turned up as it were fire. 6The stones of it are the place of sapphires: and it hath dust of gold.28.6 dust…: or, gold ore 7There is a path which no fowl knoweth, and which the vulture’s eye hath not seen: 8The lion’s whelps have not trodden it, nor the fierce lion passed by it. 9He putteth forth his hand upon the rock; he overturneth the mountains by the roots.28.9 rock: or, flint 10He cutteth out rivers among the rocks; and his eye seeth every precious thing. 11He bindeth the floods from overflowing; and the thing that is hid bringeth he forth to light.28.11 overflowing: Heb. weeping 12But where shall wisdom be found? and where is the place of understanding? 13Man knoweth not the price thereof; neither is it found in the land of the living.

14The depth saith, It is not in me: and the sea saith, It is not with me. 15It cannot be gotten for gold, neither shall silver be weighed for the price thereof.28.15 It…: Heb. Fine gold shall not be given for it 16It cannot be valued with the gold of Ophir, with the precious onyx, or the sapphire. 17The gold and the crystal cannot equal it: and the exchange of it shall not be for jewels of fine gold.28.17 jewels…: or, vessels of 18No mention shall be made of coral, or of pearls: for the price of wisdom is above rubies.28.18 coral: or, Ramoth 19The topaz of Ethiopia shall not equal it, neither shall it be valued with pure gold.

20Whence then cometh wisdom? and where is the place of understanding? 21Seeing it is hid from the eyes of all living, and kept close from the fowls of the air.28.21 air: or, heaven 22Destruction and death say, We have heard the fame thereof with our ears. 23God understandeth the way thereof, and he knoweth the place thereof. 24For he looketh to the ends of the earth, and seeth under the whole heaven; 25To make the weight for the winds; and he weigheth the waters by measure. 26When he made a decree for the rain, and a way for the lightning of the thunder: 27Then did he see it, and declare it; he prepared it, yea, and searched it out.28.27 declare…: or, number it 28And unto man he said, Behold, the fear of the Lord, that is wisdom; and to depart from evil is understanding.