Ayubu 26 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 26:1-14

Hotuba Ya Tisa Ya Ayubu

Ayubu Anajibu: Utukufu Wa Mungu Hauchunguziki

1Kisha Ayubu akajibu:

226:2 Ay 6:12; 4:3; Za 71:9; Mit 25:11“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo!

Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!

326:3 Ay 34:35Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima?

Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!

426:4 1Fal 22:24Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo?

Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?

526:5 Za 88:10; Isa 14:9“Wafu wako katika maumivu makuu,

wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.

626:6 Za 139:8; Mit 15:11; Ebr 4:13; Amo 9:2Mauti26:6 Yaani Kuzimu; Kiebrania ni Sheol. iko wazi mbele za Mungu;

Uharibifu26:6 Kwa Kiebrania ni Abadon. haukufunikwa.

726:7 Ay 9:826:7 Ay 8:22; 31:35Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu;

naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.

826:8 Mit 30:4; Za 147:8Huyafungia maji kwenye mawingu yake,

hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.

926:9 2Sam 22:10; Za 97:2Huufunika uso wa mwezi mpevu,

akitandaza mawingu juu yake.

1026:10 Mit 8:27; Isa 40:22; Ay 28:3Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji,

ameweka mpaka wa nuru na giza.

1126:11 2Sam 22:8Nguzo za mbingu nazo zatetemeka,

zinatishika anapozikemea.

1226:12 Isa 51:15; Kut 14:21; Yer 31:35; Ay 12:13; Kut 14:21; Ay 12:13; 9:13Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari;

kwa hekima yake alimkata Rahabu26:12 Rahabu hapa ni fumbo la kumaanisha Lewiathani, mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa. vipande vipande.

1326:13 Za 33:6; Isa 27:1Aliisafisha anga kwa pumzi yake;

kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.

1426:14 Ay 9:6; 36:29Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake;

tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu!

Ni nani basi awezaye kuelewa

ngurumo za nguvu zake?”

King James Version

Job 26:1-14

1But Job answered and said, 2How hast thou helped him that is without power? how savest thou the arm that hath no strength? 3How hast thou counselled him that hath no wisdom? and how hast thou plentifully declared the thing as it is? 4To whom hast thou uttered words? and whose spirit came from thee?

5Dead things are formed from under the waters, and the inhabitants thereof.26.5 and the…: or, with the inhabitants 6Hell is naked before him, and destruction hath no covering. 7He stretcheth out the north over the empty place, and hangeth the earth upon nothing. 8He bindeth up the waters in his thick clouds; and the cloud is not rent under them. 9He holdeth back the face of his throne, and spreadeth his cloud upon it. 10He hath compassed the waters with bounds, until the day and night come to an end.26.10 until…: Heb. until the end of light with darkness 11The pillars of heaven tremble and are astonished at his reproof. 12He divideth the sea with his power, and by his understanding he smiteth through the proud.26.12 the proud: Heb. pride 13By his spirit he hath garnished the heavens; his hand hath formed the crooked serpent. 14Lo, these are parts of his ways: but how little a portion is heard of him? but the thunder of his power who can understand?