Ayubu 21 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 21:1-34

Hotuba Ya Saba Ya Ayubu

Ayubu Anajibu: Waovu Mara Nyingi Huenda Bila Kuadhibiwa

1Ndipo Ayubu akajibu:

221:2 Ay 13:17; 21:34“Yasikilizeni maneno yangu kwa makini;

hii na iwe faraja mnayonipa mimi.

321:3 Ay 6:14; 11:3; 16:10Nivumilieni ninapozungumza,

nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki.

421:4 Za 22:1-3; Ay 6:3, 11; 1Sam 1:16“Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu?

Kwa nini nisikose subira?

521:5 Amu 18:19; Ay 40:4Niangalieni mkastaajabu;

mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu.

621:6 Mwa 45:3; Ay 4:14Ninapowaza juu ya hili, ninaogopa,

nao mwili wangu unatetemeka.

721:7 Mhu 7:15; Mal 3:15; Yer 12:1-3Kwa nini waovu wanaendelea kuishi,

wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?

821:8 Za 17:14; Mal 3:15Huwaona watoto wao wakithibitika

wakiwa wamewazunguka,

wazao wao mbele za macho yao.

921:9 Ay 5:24; Za 73:5Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu;

fimbo ya Mungu haiko juu yao.

1021:10 Kut 23:26Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe;

ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.

1121:11 Za 78:52; 107:41Huwatoa watoto wao nje kama kundi;

wadogo wao huchezacheza.

1221:12 1Nya 15:16; Mt 15:17Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi,

nao huifurahia sauti ya filimbi.

1321:13 Ay 24:19; Za 49:14; Isa 14:15; Ay 3:13Huitumia miaka yao katika mafanikio

nao hushuka kaburini kwa amani.

1421:14 Ay 4:17; Kum 32:15; Isa 30:11; 1Sam 11:15Lakini humwambia Mungu, ‘Tuache sisi!’

Hatuna haja ya kufahamu njia zako.

1521:15 Yer 9:6; Mal 3:14Mwenyezi ni nani hata tumtumikie?

Tutapata faida gani kumwomba?

1621:16 Ay 22:18; Za 1:1; 26:5; 36:1Lakini kufanikiwa kwao hakupo mikononi mwao wenyewe,

hivyo najitenga mbali na shauri la waovu.

1721:17 Ay 18:5; 18:12; 20:22, 28“Lakini ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa?

Ni mara ngapi maafa huwajia,

yale yawapatayo ambayo Mungu

huwapangia katika hasira yake?

1821:18 Ay 13:15; Mwa 19:15; Ay 7:10; Mit 10:25; Mwa 7:23Ni mara ngapi huwa kama majani makavu mbele ya upepo,

kama makapi yachukuliwayo na dhoruba?

1921:19 Kut 20:5; Yn 9:2Imesemekana, ‘Mungu huiweka akiba adhabu ya mtu

kwa ajili ya wanawe.’

Mungu na amlipe mtu mwenyewe,

ili apate kulijua!

2021:20 Ay 6:4; Isa 51:17; Yer 25:15; Ufu 14:10Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake;

yeye na ainywe ghadhabu ya Mwenyezi.

2121:21 Ay 14:22; 14:5; 14:21; Mhu 9:5-6Kwani anajali nini kuhusu jamaa anayoiacha nyuma,

miezi yake aliyopangiwa ifikapo mwisho?

2221:22 Za 94:12; 86:8; Rum 11:34“Je, yuko mtu yeyote awezaye kumfundisha Mungu maarifa,

iwapo yeye ndiye ahukumuye hata walio juu ya wote?

2321:23 Mwa 15:15; Ay 13:26; 3:13Mtu mmoja hufa akiwa na nguvu zake kamili,

akiwa salama na mwenye raha kamili,

2421:24 Mit 3:8mwili wake ukiwa umenawiri,

nayo mifupa yake ikiwa imejaa mafuta ndani yake.

2521:25 Ay 10:1Mtu mwingine hufa katika uchungu wa nafsi,

akiwa hajafurahia kamwe jambo lolote zuri.

2621:26 Mhu 9:2-3; Isa 14:11Hao wote hulala mavumbini,

nao mabuu huwafunika wote.

27“Ninayajua kikamilifu yale mnayoyafikiri,

mipango ambayo kwayo mngenitendea mabaya.

2821:28 Ay 1:3; 12:21; 29:25; 31:37; 8:22Mwasema, ‘Iko wapi sasa nyumba ya huyo mtu mkuu,

mahema ambayo watu waovu walikaa?’

29Je, hamkuwahi kuwauliza hao wanaosafiri?

Je, hamkutafakari taarifa zao:

3021:30 Ay 31:3; Mit 16:4; Isa 5:30; Rum 5:2kwamba mtu mwovu huepushwa kutoka siku ya maafa,

kwamba huokolewa kutoka siku ya ghadhabu?

3121:31 Ay 34:11; Za 62:12; Mit 24:11-12; Isa 59:18Ni nani hulaumu matendo yake mbele ya uso wake?

Ni nani ampatilizaye kwa yale aliyoyatenda?

3221:32 Isa 14:18Hupelekwa kaburini,

nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake.

3321:33 Ay 3:17-19; 17:16; 24:24Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake;

watu wote watamfuata,

nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia.

34“Hivyo ninyi mnawezaje kunifariji kwa upuzi wenu?

Hakuna kilichosalia cha majibu yenu isipokuwa uongo!”

Japanese Contemporary Bible

ヨブ 記 21:1-34

21

ヨブのことば

1ヨブの返答。

2-3「私の言い分をよく聞け。

とにかく、話させてほしい。

そのあとで、好きなだけあざければよい。

4人に対してではない。

神に言いたいことがあるのだ。

こんな状態なら、悩むのが当然だろう。

5まともに私を見てみるがよい。

あまりの恐怖に、あなたがたは手を口に当てるだろう。

6私さえ、自分の姿を見ると恐ろしくなって身震いする。

7罪深い悪者が天寿を全うし、名を上げ、

羽振りをきかせているのが現実だ。

8彼らは子どもが成長するまで長生きし、

孫の顔まで見ることができる。

9家庭の心配事など一つもなく、平和そのものだ。

しかも、神は彼らを罰しない。

10家畜もどんどん増えるし、

11快活な子どもたちにも恵まれる。

12-13彼らは毎日、歌と踊りで明け暮れる。

資産家となり、倹約などする必要もなく、

死ぬまで栄える。

14神を追い出し、神になどかかわりたくないと

思っているのに、このようになるのだ。

15彼らは大きな口をたたく。

『全能の神だって? いったい、だれのことだ。

なぜ神などに従わなきゃならないのだ。

大したご利益もないのに。』

16悪者がさわった物は、何もかも金になる。

だが私は、そんな人々とはかかわりたくない。

17悪者はいつでも罰を免れる。

災いに会わず、

神が悲しんだり、怒ったりするときも、

彼らだけが見逃される。

18風が彼らをわらのように吹き飛ばし、

嵐が運び去るというのか。とんでもない。

19『だが神は、少なくとも彼らの子どもを罰する』

と言っても、私は納得できない。

罪を犯した当人が罰されるべきで、

子どもは罰されるべきではない。

当人が身をもって、

刑罰の痛みを思い知るべきではないか。

20自分が悪くて滅びを招いたのだから、

全能者の怒りを自分でのみ尽くすべきだ。

21そして死んで、

二度と家族と楽しむこともできなくなるのだ。

22とはいえ、だれが、さばき主である神に異議を申し立てることができようか。

23-24神は健康な者、富んでいる者、

肥えている者、栄えている者を滅ぼす。

25一方では、生まれて一度も幸せだったことのない

貧しい人をも滅ぼす。

26どちらも、同じちりの中に埋められ、

同じようにうじ虫の餌食になる。

27あなたたちの言おうとすることはわかっている。

28きっと、罪のために災いを招いた、

金持ちの悪者を引き合いに出すことだろう。

29だが、手近な人に尋ねてみるがよい。

30-32悪者はたいてい災いの日に命拾いし、逃げのびる、

と答えるに決まっているから。

だれも面と向かって彼を責めず、報復もしない。

そればかりか、兵士が彼の墓を見張ってくれる。

33盛大な葬儀の行列が続き、

やわらかい土が彼を覆う。

34あなたがたは前提から間違っている。

なぜ私を慰められると思っているのか。」