Ayubu 18 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 18:1-21

Bildadi Anasema: Mungu Huwaadhibu Waovu

118:1 Ay 8:1Bildadi Mshuhi akajibu:

218:2 Ay 8:2; 16:3“Je, ni lini utafika mwisho wa maneno haya?

Uwe mwenye busara, nasi ndipo tutakapoweza kuongea.

318:3 Za 73:22; Ay 12:7Kwa nini sisi tunafikiriwa kama wanyama,

na kuonekana wajinga machoni pako?

418:4 Ay 13:14; 16:9; 14:18Wewe unayejirarua mwenyewe vipande vipande

katika hasira yako,

je, dunia iachwe kwa ajili yako wewe?

Au ni lazima miamba iondolewe mahali pake?

518:5 Yer 25:10; Yn 8:12; Mit 13:9“Taa ya mwovu imezimwa,

nao mwali wa moto wake umezimika.

618:6 Ay 8:22; 5:14; 11:17; 12:25Mwanga hemani mwake umekuwa giza;

taa iliyo karibu naye imezimika.

718:7 Za 18:36; Mit 4:12; Ay 5:13; 15:6Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa;

shauri lake baya litamwangusha.

818:8 Mik 7:2; Hab 1:15Miguu yake imemsukumia kwenye wavu,

naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.

918:9 Ay 22:10; 30:12; Isa 24:18; Yer 48:44; Amo 5:14; Mit 7:22Tanzi litamkamata kwenye kisigino;

mtego utamshikilia kwa nguvu.

1018:10 Mit 7:22; Isa 51:20; 1Sam 28:9; Za 140:5Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake;

mtego uko kwenye njia yake.

1118:11 Ay 15:21; 20:8; Za 31:13; Isa 22:18; Yer 6:25Vitisho vimemtia hofu kila upande,

na adui zake humwandama kila hatua.

1218:12 Isa 9:20; 65:13; 8:21; Ay 21:17; 31:3; 15:25Janga linamwonea shauku;

maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.

1318:13 Zek 14:12; Hes 12:12Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake;

mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.

1418:14 Ay 8:22; 15:24; 18:11Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake,

na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.

1518:15 Mwa 19:24; Za 11:6; Ay 18:18; 20:26Moto utakaa katika hema lake;

moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.

1618:16 Hos 5:12; Amo 2:9; Mwa 27:28Mizizi yake chini itakauka

na matawi yake juu yatanyauka.

1718:17 Mit 2:22; 10:7; Isa 49:15; Kum 32:26; 9:14; Za 9:5; 69:28Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia,

wala hatakuwa na jina katika nchi.

1818:18 Ay 5:14; 18:11; 11:20; 30:8Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani,

naye amefukuzwa mbali atoke duniani.

1918:19 Za 37:28; 21:10; Isa 14:22; Ay 27:14-15Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake,

wala aliyenusurika mahali alipoishi.

2018:20 Yer 46:21; Eze 7:7Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata;

watu wa mashariki watapatwa na hofu.

2118:21 Ay 21:28; Yer 9:3; 1The 4:5Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu;

ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”

Swedish Contemporary Bible

Job 18:1-21

Bildad talar igen

1Bildad från Shuach svarade:

2Ska inte detta ordflöde upphöra någon gång?

Bli nu förnuftig, så vi kan prata!18:2 Grundtextens innebörd är osäker.

3Varför betraktas vi som boskap,

som är dumma i dina ögon?

4Du sliter ju sönder dig själv i din vrede.

Skulle jorden ödeläggas för din skull

eller klippan förflytta sig från sin plats?

5Den ogudaktiges ljus slocknar,

lågan av hans eld slutar brinna.

6Det är mörkt i hans tält,

hans lampa slocknar.

7Hans starka steg försvagas,

hans egna planer fäller honom.

8Hans fötter fastnar i nätet,

han vandrar mot snaran.

9Snaran griper honom om hälen,

fällan håller honom fast.

10En snara ligger gömd i marken,

en fälla är lagd på stigen.

11Skräcken ansätter honom från alla håll

och jagar varje steg han tar.

12Olyckan vill sluka honom,

hemsökelsen är beredd för hans fall.

13Hans hud fräts sönder av sjukdomar,

dödens förstfödde förtär hans lemmar.

14Han rycks bort från sin trygga boning,

han förs bort till fasornas kung.

15Hans boning intas av ingenting,

och svavel sprids ut över den.18:15 Grundtextens innebörd är osäker.

16Hans rötter förtorkas nertill,

hans krona vissnar bort upptill.

17Han utplånas från jorden,

hans namn nämns ingenstans på jorden.

18Han drivs ut ur ljuset in i mörkret

och förföljs ut ur världen.

19Han ska varken ha barn eller ättlingar bland sitt folk,

och där han bott överlever ingen.

20I väst förskräcks folk över hans öde,

i öst grips man av förfäran.

21Detta är vad som händer med syndarens boning,

så går det med den plats där man förkastar Gud.