Ayubu 1 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 1:1-22

Sehemu Ya Kwanza: Habari Za Awali

(Ayubu 1–2)

Ayubu Na Jamaa Yake

11:1 Mwa 22:21; Yak 5:11; Eze 14:14, 20; Mit 8:13; Mwa 10:23; 6:9; 22:12; Ay 23:7, 10; 2:3; Za 11:7; 107:42; Mit 21:29; Mik 7:2; Kum 4:6; 1The 5:22Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu. 21:2 Za 127:3; Rut 4:15; Ay 1:13, 18; 42:13; Za 144:12Alikuwa na wana saba na binti watatu, 31:3 Ay 29:25; Mwa 13:2; 12:16; Ay 1:8; Mwa 25:6; Ay 42:10; Za 103:10naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.

41:4 Ay 1:13, 18Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao. 51:5 Mwa 8:20; Ay 42:8; 1Fal 21:10-13; Za 74:10; Neh 12:30; Ay 8:4; Za 10:3Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.

Jaribu La Kwanza La Ayubu

61:6 1Fal 22:19; Ay 38:7; 2:1; Dan 7:10; Mwa 6:2; 2Sam 24:1; 2Nya 18:21; Za 109:6; Lk 22:31Siku moja wana wa Mungu1:6 Wana wa Mungu hapa ina maana malaika au viumbe vya mbinguni. walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani1:6 Shetani hapa ina maana ya mshtaki wa watakatifu. naye akaja pamoja nao. 71:7 Mwa 3:1; 1Pet 5:8; Mt 12:43Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?”

Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”

81:8 Ay 42:7-8; Kut 20:20; Yos 1:7; Za 25:16; 26:12; 112:1; 128:4Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”

91:9 1Tim 6:5Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure? 101:10 Za 34:7; 128:1-2; Ay 8:7; 1Sam 25:16; Ay 2:4; 29:6; 42:12, 17Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima. 111:11 Ay 19:21; Law 24:11; Ufu 12:9-10; Lk 22:31; Isa 3:8; 65:3; Ay 2:5Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”

121:12 Ay 2:6; 1Kor 10:13Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.”

Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.

131:13 Ay 1:2, 4; Mhu 9:12; Lk 12:19, 20Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa, 141:14 Mwa 36:24akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao, 151:15 Mwa 10:7; Ay 6:19; 9:26Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”

161:16 1Fal 18:38; 2Fal 1:12; Ay 20:26; Mwa 18:17; Law 10:2; Hes 11:1-3Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”

171:17 Mwa 11:28-31; Ay 9:24Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”

181:18 Ay 1:2, 4Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa, 191:19 Isa 21:1; Mk 7:25; Za 11:6; Isa 5:28; Yer 4:11; 13:24; 18:17; Eze 17:10; Hos 13:15ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”

201:20 Mwa 37:29; Mk 14:63; Isa 3:24; 15:2; 22:12; Yer 7:29; 16:6; Eze 27:31; 29:18; Mik 1:16; 1Pet 5:6Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu 211:21 Mhu 5:15; Rut 1:21; Amu 10:15; Efe 5:20; Mwa 45:5; 1Tim 6:7; 1Sam 2:7; Mhu 7:14; Yak 5:11; Amo 3:6; Efe 5:20; Mwa 45:5na kusema:

“Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi,

nami nitaondoka uchi,1:21 Au: nitarudi huko uchi.

Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa,

jina la Bwana litukuzwe.”

221:22 Mit 10:19; Rum 9:20; Ay 2:10; Za 39:1; Isa 53:7Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

約伯記 1:1-22

約伯的敬虔

1烏斯有一個人名叫約伯,他純全正直,敬畏上帝,遠離罪惡。 2他有七子三女、 3七千隻羊、三千隻駱駝、五百對牛、五百頭母驢及許多僕婢。他在東方人中最富有。 4約伯的兒子們經常輪流在自己家裡設宴,派人邀請他們的三個姊妹來一起吃喝。 5宴會的日子結束後,約伯便派人召來他的兒女,為他們行潔淨禮。他清早起來,為他們每個人獻上燔祭,因為他想:「也許我的孩子們犯了罪,心中褻瀆了上帝。」約伯常常這樣做。

撒旦控告約伯

6有一天,眾天使1·6 眾天使」希伯來文是「上帝的眾子」,2·138·7同。來朝見耶和華,撒旦也在他們當中。 7耶和華問撒旦:「你從哪裡來?」撒旦答道:「我在地上到處遊走。」 8耶和華問撒旦:「你注意到我的僕人約伯了嗎?世上沒有人像他那樣純全正直,敬畏我,遠離罪惡。」 9撒旦說:「約伯敬畏你難道無緣無故嗎? 10你豈不是像籬笆一樣四面保護他及其全家和一切產業嗎?你使他事事蒙福,牛羊遍地。 11倘若你伸手毀壞他擁有的一切,他必當面褻瀆你。」 12耶和華對撒旦說:「好吧,他的一切都在你手中,但不可傷害他。」撒旦便從耶和華面前退去。

約伯失去所有

13有一天,約伯的兒女正在長兄家吃喝, 14有報信的人來對約伯說:「牛正在耕田、驢正在旁邊吃草的時候, 15示巴人忽然來襲,搶走了牲口,用刀殺了你的僕人,只有我一人逃脫來向你報信。」 16話音未落,又有人來報信說:「上帝的火從天而降,燒死了羊群和牧人,只有我一人逃脫來向你報信。」 17話音未落,又有人來報信說:「迦勒底人分三隊來襲,搶走了駱駝,用刀殺了你的僕人,只有我一人逃脫來向你報信。」 18話音未落,又有人來報信說:「你的兒女正在長兄家吃喝的時候, 19忽然從曠野颳來一陣狂風,摧毀了房子四角,房子倒塌,壓死了屋裡所有的人,只有我一人逃脫來向你報信。」

20約伯站起來,撕裂外袍,剃掉頭髮,俯伏在地上敬拜, 21說:「我從母腹赤身而來,也必赤身而去。賞賜的是耶和華,收回的也是耶和華。耶和華的名當受稱頌!」 22約伯遭此不幸,仍沒有犯罪,也沒有埋怨上帝。