Amosi 9 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Amosi 9:1-15

Israeli Kuangamizwa

19:1 Za 68:21; Yer 11:11Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema:

“Piga vichwa vya nguzo

ili vizingiti vitikisike.

Viangushe juu ya vichwa vya watu wote;

na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga.

Hakuna awaye yote atakayekimbia,

hakuna atakayetoroka.

29:2 Za 139:8-10; Ay 20:6; 7:9; Yer 51:33; Oba 1:4; Eze 26:20Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu,

kutoka huko mkono wangu utawatoa.

Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu,

kutoka huko nitawashusha.

39:3 Yer 23:24; 6:16-17; Za 139:8-10; 68:22; Mwa 49:17; Ay 11:20Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli,

huko nitawawinda na kuwakamata.

Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu

katika vilindi vya bahari,

huko nako nitaamuru joka kuwauma.

49:4 Law 26:33; 17:10; Eze 5:12; 15:7; Kum 28:65; Yer 39:16; 21:10; 44:11Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao,

huko nako nitaamuru upanga uwaue.

Nitawakazia macho yangu kwa mabaya

wala si kwa mazuri.”

59:5 Za 46:2; Amo 8:8; Mik 1:4Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka,

na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza:

nayo nchi yote huinuka kama Naili,

kisha hushuka kama mto wa Misri;

69:6 Za 104:1-3, 5-13; Amo 5:8; Yer 43:9yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu

na kuisimika misingi yake juu ya dunia,

yeye aitaye maji ya bahari

na kuyamwaga juu ya uso wa nchi:

Bwana ndilo jina lake.

79:7 2Nya 12:3; Kum 2:23; Isa 43:3; 22:6; 2Fal 16:9; Yer 47:4; Amo 1:5; Mwa 10:14“Je, Waisraeli,

ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?”

asema Bwana.

“Je, sikuleta Israeli kutoka Misri,

Wafilisti kutoka Kaftori,9:7 Yaani Krete.

na Washamu kutoka Kiri?

89:8 Yer 30:11; 44:27; Za 11:4“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi

yako juu ya ufalme wenye dhambi.

Nami nitauangamiza

kutoka kwenye uso wa dunia:

hata hivyo sitaiangamiza kabisa

nyumba ya Yakobo,”

asema Bwana.

99:9 Lk 22:31; Isa 30:28; Yer 31:36; Dan 9:7“Kwa kuwa nitatoa amri,

na nitaipepeta nyumba ya Israeli

miongoni mwa mataifa yote,

kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo,

na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.

109:10 Yer 5:12; 23:17; 49:37; Eze 20:38; Amo 6:3Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu

watauawa kwa upanga,

wale wote wasemao,

‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’

Kurejezwa Kwa Israeli

119:11 Mdo 15:16; Mik 7:8-11; Zek 12:7; Isa 7:2; 49:8; Mwa 26:22; Eze 17:24“Katika siku ile nitaisimamisha

hema ya Daudi iliyoanguka.

Nitakarabati mahali palipobomoka

na kujenga upya magofu yake,

na kuijenga kama ilivyokuwa awali,

129:12 Hes 24:18; Isa 43:7; Oba 1:19; Yer 25:29; Mdo 15:16-17ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu,

na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,”

asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.

139:13 Law 26:5; Amu 9:27; Yoe 3:18; 2:24; Yer 31:38; 33:14; Rut 2:3“Siku zinakuja,” asema Bwana,

“wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima,

naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu.

Divai mpya itadondoka kutoka milimani,

na kutiririka kutoka vilima vyote.

149:14 Isa 32:18; 49:8; 62:9; 61:4; Eze 34:13-14; Yer 29:14; 33:7; 30:18Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa;

wataijenga tena miji iliyoachwa magofu,

nao wataishi ndani mwake.

Watapanda mizabibu na kunywa divai yake;

watalima bustani na kula matunda yake.

159:15 Kut 15:17; Isa 60:21; 65:9; Yer 18:9; 23:8; 3:18; 24:6; 32:15; Eze 28:26; 34:28; Yoe 3:20Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe,

hawatangʼolewa tena

kutoka nchi ambayo nimewapa,”

asema Bwana Mungu wenu.

New International Version

Amos 9:1-15

Israel to Be Destroyed

1I saw the Lord standing by the altar, and he said:

“Strike the tops of the pillars

so that the thresholds shake.

Bring them down on the heads of all the people;

those who are left I will kill with the sword.

Not one will get away,

none will escape.

2Though they dig down to the depths below,

from there my hand will take them.

Though they climb up to the heavens above,

from there I will bring them down.

3Though they hide themselves on the top of Carmel,

there I will hunt them down and seize them.

Though they hide from my eyes at the bottom of the sea,

there I will command the serpent to bite them.

4Though they are driven into exile by their enemies,

there I will command the sword to slay them.

“I will keep my eye on them

for harm and not for good.”

5The Lord, the Lord Almighty—

he touches the earth and it melts,

and all who live in it mourn;

the whole land rises like the Nile,

then sinks like the river of Egypt;

6he builds his lofty palace9:6 The meaning of the Hebrew for this phrase is uncertain. in the heavens

and sets its foundation9:6 The meaning of the Hebrew for this word is uncertain. on the earth;

he calls for the waters of the sea

and pours them out over the face of the land—

the Lord is his name.

7“Are not you Israelites

the same to me as the Cushites9:7 That is, people from the upper Nile region?”

declares the Lord.

“Did I not bring Israel up from Egypt,

the Philistines from Caphtor9:7 That is, Crete

and the Arameans from Kir?

8“Surely the eyes of the Sovereign Lord

are on the sinful kingdom.

I will destroy it

from the face of the earth.

Yet I will not totally destroy

the descendants of Jacob,”

declares the Lord.

9“For I will give the command,

and I will shake the people of Israel

among all the nations

as grain is shaken in a sieve,

and not a pebble will reach the ground.

10All the sinners among my people

will die by the sword,

all those who say,

‘Disaster will not overtake or meet us.’

Israel’s Restoration

11“In that day

“I will restore David’s fallen shelter—

I will repair its broken walls

and restore its ruins—

and will rebuild it as it used to be,

12so that they may possess the remnant of Edom

and all the nations that bear my name,9:12 Hebrew; Septuagint so that the remnant of people / and all the nations that bear my name may seek me

declares the Lord, who will do these things.

13“The days are coming,” declares the Lord,

“when the reaper will be overtaken by the plowman

and the planter by the one treading grapes.

New wine will drip from the mountains

and flow from all the hills,

14and I will bring my people Israel back from exile.9:14 Or will restore the fortunes of my people Israel

“They will rebuild the ruined cities and live in them.

They will plant vineyards and drink their wine;

they will make gardens and eat their fruit.

15I will plant Israel in their own land,

never again to be uprooted

from the land I have given them,”

says the Lord your God.