Amosi 7 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Amosi 7:1-17

Maono Ya Kwanza: Nzige

17:1 Amo 8:1; Za 78:46; Yer 51:14; Yoe 1:4Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua. 27:2 Kut 10:15; Eze 11:13; Isa 37:4; Amo 4:9Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”

37:3 Kut 32:14; Yon 3:10; Kum 32:36; Za 106:45; 1Nya 21:15; Hos 11:8; Yoe 2:14; Yak 5:16; Yer 18:8; 26:19Kwa hiyo Bwana akaghairi.

Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”

Maono Ya Pili: Moto

47:4 Isa 66:16; Yoe 1:19; Kum 32:22Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi. 57:5 Yoe 2:17Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”

67:6 Kut 32:14; Yer 18:8; 42:10; Za 102:17; Yon 3:10; Eze 9:8Kwa hiyo Bwana akaghairi.

Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”

Maono Ya Tatu: Timazi

7Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake. 87:8 Isa 28:17; Mao 2:8; 2Fal 21:13; Eze 7:2-9; Yer 1:11-13; 15:6; Mik 7:18Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?”

Nikamjibu, “Uzi wa timazi.”

Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.

97:9 Law 26:31; Mwa 26:23; 2Fal 14:23; 1Fal 13:34; 2Fal 15:9-10; Isa 63:18; Hos 10:8“Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa,

na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa;

kwa upanga wangu nitainuka

dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”

Amosi Na Amazia

107:10 1Fal 12:32; Yos 7:2; 2Fal 14:23-24; Yer 38:4; 26:8-11Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote. 117:11 Amo 5:27; Yer 36:16Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema:

“ ‘Yeroboamu atakufa kwa upanga,

na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni,

mbali na nchi yao.’ ”

127:12 Mt 8:34; 1Sam 9:9Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako. 137:13 Yer 20:2; 36:5; Amo 2:12; Mdo 4:18; Yos 7:2; 1Fal 12:29Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”

147:14 1Sam 10:5; Zek 13:5; 2Fal 2:5; 4:38; Isa 9:10; 1Fal 10:27Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu. 157:15 Mwa 37:5; 2Sam 7:8; Yer 7:1-2; 26:12; Eze 2:3-4; Isa 6:9Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’ 167:16 Isa 30:10; Eze 20:46; Mik 2:6; Yer 22:2Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema,

“ ‘Usitabiri dhidi ya Israeli,

na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’

177:17 Hos 4:13; 9:3; Eze 4:13; Yer 28:12; 29:21; Mao 5:11; Amo 5:27; 2:12-13; 2Fal 17:6“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Mke wako atakuwa kahaba mjini,

nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga.

Shamba lako litapimwa na kugawanywa,

na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani.

Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni,

mbali na nchi yao.’ ”

New International Version – UK

Amos 7:1-17

Locusts, fire and a plumb-line

1This is what the Sovereign Lord showed me: he was preparing swarms of locusts after the king’s share had been harvested and just as the late crops were coming up. 2When they had stripped the land clean, I cried out, ‘Sovereign Lord, forgive! How can Jacob survive? He is so small!’

3So the Lord relented.

‘This will not happen,’ the Lord said.

4This is what the Sovereign Lord showed me: the Sovereign Lord was calling for judgment by fire; it dried up the great deep and devoured the land. 5Then I cried out, ‘Sovereign Lord, I beg you, stop! How can Jacob survive? He is so small!’

6So the Lord relented.

‘This will not happen either,’ the Sovereign Lord said.

7This is what he showed me: the Lord was standing by a wall that had been built true to plumb,7:7 The meaning of the Hebrew for this phrase is uncertain. with a plumb-line7:7 The meaning of the Hebrew for this phrase is uncertain; also in verse 8. in his hand. 8And the Lord asked me, ‘What do you see, Amos?’

‘A plumb-line,’ I replied.

Then the Lord said, ‘Look, I am setting a plumb-line among my people Israel; I will spare them no longer.

9‘The high places of Isaac will be destroyed

and the sanctuaries of Israel will be ruined;

with my sword I will rise against the house of Jeroboam.’

Amos and Amaziah

10Then Amaziah the priest of Bethel sent a message to Jeroboam king of Israel: ‘Amos is raising a conspiracy against you in the very heart of Israel. The land cannot bear all his words. 11For this is what Amos is saying:

‘ “Jeroboam will die by the sword,

and Israel will surely go into exile,

away from their native land.” ’

12Then Amaziah said to Amos, ‘Get out, you seer! Go back to the land of Judah. Earn your bread there and do your prophesying there. 13Don’t prophesy anymore at Bethel, because this is the king’s sanctuary and the temple of the kingdom.’

14Amos answered Amaziah, ‘I was neither a prophet nor the son of a prophet, but I was a shepherd, and I also took care of sycamore-fig trees. 15But the Lord took me from tending the flock and said to me, “Go, prophesy to my people Israel.” 16Now then, hear the word of the Lord. You say,

‘ “Do not prophesy against Israel,

and stop preaching against the descendants of Isaac.”

17‘Therefore this is what the Lord says:

‘ “Your wife will become a prostitute in the city,

and your sons and daughters will fall by the sword.

Your land will be measured and divided up,

and you yourself will die in a pagan7:17 Hebrew an unclean country.

And Israel will surely go into exile,

away from their native land.” ’