2 Wakorintho 11 – NEN & HHH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wakorintho 11:1-33

Paulo Na Mitume Wa Uongo

111:1 Mt 17:17; 2Kor 5:13Laiti mngenivumilia kidogo katika upumbavu wangu! Naam, nivumilieni kidogo. 211:2 Hos 2:19; Efe 5:26-27Ninawaonea wivu, wivu wa Kimungu, kwa kuwa mimi niliwaposea mume mmoja, ili niwalete kwa Kristo kama mabikira safi. 311:3 Mwa 3:1-6; 1Tim 2:14; Ufu 12:5Lakini nina hofu kuwa, kama vile Eva alivyodanganywa kwa ujanja wa yule nyoka, mawazo yenu yasije yakapotoshwa, mkauacha unyofu na usafi wa upendo wenu kwa Kristo. 411:4 1Kor 3:11; Rum 8:15; Gal 1:6-9Kwa sababu kama mtu akija na kuwahubiria Yesu mwingine ambaye si yule tuliyemhubiri, au kama mkipokea roho mwingine ambaye si yule mliyempokea, au Injili tofauti na ile mliyoikubali, ninyi mnaitii kwa urahisi. 511:5 2Kor 12:11; Gal 2:6Lakini sidhani ya kuwa mimi ni dhalili sana kuliko hao “mitume wakuu.” 611:6 1Kor 1:17; 2Kor 9:7; Efe 3:4Inawezekana mimi nikawa si mnenaji hodari, lakini ni hodari katika elimu. Jambo hili tumelifanya liwe dhahiri kwenu kwa njia zote.

711:7 2Kor 12:13; Rum 1:1; 1Kor 9:18Je, nilitenda dhambi kwa kujishusha ili kuwainua ninyi kwa kuwahubiria Injili ya Mungu pasipo malipo? 811:8 Flp 4:15-18Niliyanyangʼanya makanisa mengine kwa kupokea misaada kutoka kwao ili niweze kuwahudumia ninyi. 911:9 Flp 4:15; 2Kor 12:13-16Nami nilipokuwa pamoja nanyi, nikipungukiwa na chochote, sikuwa mzigo kwa mtu yeyote, kwa maana ndugu waliotoka Makedonia walinipatia mahitaji yangu. Kwa hiyo nilijizuia kuwa mzigo kwenu kwa njia yoyote, nami nitaendelea kujizuia. 1011:10 Rum 9:1; Mdo 18:12; 1Kor 9:15Kwa hakika kama vile kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, hakuna mtu yeyote katika Akaya nzima atakayenizuia kujivunia jambo hili. 1111:11 Rum 1:9; 2Kor 12:15Kwa nini? Je, ni kwa sababu siwapendi? Mungu anajua ya kuwa nawapenda! 1211:12 2Kor 9:12Nami nitaendelea kufanya lile ninalofanya sasa ili nisiwape nafasi wale ambao wanatafuta nafasi ya kuhesabiwa kuwa sawa na sisi katika mambo wanayojisifia.

1311:13 Mt 7:15; Tit 1:10; Ufu 2:2Watu kama hao ni mitume wa uongo, ni wafanyakazi wadanganyifu, wanaojigeuza waonekane kama mitume wa Kristo. 1411:14 Mt 4:10Wala hii si ajabu, kwa kuwa hata Shetani mwenyewe hujigeuza aonekane kama malaika wa nuru. 1511:15 Mt 16:27; Flp 3:19Kwa hiyo basi si ajabu, kama watumishi wa Shetani nao hujigeuza ili waonekane kama watumishi wa haki. Mwisho wao utakuwa sawa na matendo yao yanavyostahili.

Paulo Anajivunia Mateso Yake

1611:16 2Kor 11:1; 12:6, 11Nasema tena, mtu yeyote asidhani kwamba mimi ni mjinga. Lakini hata kama mkinidhania hivyo, basi nipokeeni kama mjinga ili nipate kujisifu kidogo. 1711:17 1Kor 7:12, 25; 2Kor 11:21; 1Kor 7:6Ninayosema kuhusiana na huku kujisifu kwa kujiamini, sisemi kama vile ambavyo Bwana angesema, bali kama mjinga. 1811:18 2Kor 5:16; 10:4; Flp 3:3-4Kwa kuwa wengi wanajisifu kama vile ulimwengu ufanyavyo, mimi nami nitajisifu. 1911:19 1Kor 4:10; 2Kor 11:1Ninyi mwachukuliana na wajinga kwa sababu mna hekima sana! 2011:20 2Kor 11:1Kweli ni kwamba mnachukuliana na mtu akiwatia utumwani au akiwatumia kwa ajili ya kupata faida au akiwanyangʼanya au akijitukuza mwenyewe au akiwadanganya. 2111:21 2Kor 10:1; Flp 3:4Kwa aibu inanipasa niseme kwamba sisi tulikuwa dhaifu sana kwa jambo hilo!

Lakini chochote ambacho mtu mwingine yeyote angethubutu kujisifia, nanena kama mjinga, nami nathubutu kujisifu juu ya hilo. 2211:22 Flp 3:5; Rum 9:4; 11:1; Lk 3:8Je, wao ni Waebrania? Mimi pia ni Mwebrania. Je, wao ni Waisraeli? Mimi pia ni Mwisraeli. Je, wao ni wazao wa Abrahamu? Mimi pia ni mzao wa Abrahamu. 2311:23 1Kor 3:5; 15:10; Mdo 16:23; 2Kor 6:4-5; Rum 8:36Je, wao ni watumishi wa Kristo? (Nanena kiwazimu.) Mimi ni zaidi yao. Nimefanya kazi kwa bidii kuwaliko wao, nimefungwa gerezani mara kwa mara, nimechapwa mijeledi sana, na nimekabiliwa na mauti mara nyingi. 2411:24 Kum 25:3Mara tano nimechapwa na Wayahudi viboko arobaini kasoro kimoja. 2511:25 Mdo 16:22; 14:19; 27:1-44Mara tatu nilichapwa kwa fimbo, mara moja nilipigwa kwa mawe, mara tatu nimevunjikiwa na meli, nimekaa kilindini usiku kucha na mchana kutwa, 2611:26 Mdo 20:3; 21:31; Gal 2:4katika safari za mara kwa mara. Nimekabiliwa na hatari za kwenye mito, hatari za wanyangʼanyi, hatari kutoka kwa watu wangu mwenyewe, hatari kutoka kwa watu wa Mataifa; hatari mijini, hatari nyikani, hatari baharini; na hatari kutoka kwa ndugu wa uongo. 2711:27 Mdo 18:3; Kol 1:29; 1Kor 4:11-12; 2Kor 6:5Nimekuwa katika kazi ngumu na taabu, katika kukesha mara nyingi; ninajua kukaa njaa na kuona kiu; nimefunga kula chakula mara nyingi; nimehisi baridi na kuwa uchi. 2811:28 1Kor 7:17Zaidi ya hayo yote, nakabiliwa na mzigo wa wajibu wangu kwa makanisa yote. 2911:29 Rum 14:1; 1Kor 2:3; Mt 5:29Je, ni nani aliye mdhaifu, nami nisijisikie mdhaifu? Je, nani aliyekwazwa, nami nisiudhike?

3011:30 Gal 6:14; 2Kor 12:5-9; 1Kor 2:3Kama ni lazima nijisifu, basi nitajisifia yale mambo yanayoonyesha udhaifu wangu. 3111:31 Rum 1:25; 9:5Mungu na Baba wa Bwana Yesu, yeye ambaye anahimidiwa milele, anajua ya kuwa mimi sisemi uongo. 3211:32 Mdo 9:24; 9:25Huko Dameski, mtawala aliyekuwa chini ya Mfalme Areta aliulinda mji wa Dameski ili kunikamata. 33Lakini nilishushwa kwa kapu kubwa kupitia katika dirisha ukutani, nikatoroka kutoka mikononi mwake.

Habrit Hakhadasha/Haderekh

אגרת פולוס השנייה אל-הקורנתים 11:1-33

1אני מקווה שתתייחסו אלי בסבלנות גם אם אני מדבר בטיפשות.

אנא, סלחו לי והניחו לי לומר את אשר על לבי. 2אני דואג לכם דאגה עמוקה כאלוהים עצמו; אתם כבתולה טהורה שהארשתי לאיש אחד, למשיח. 3אך אני חושש שמא תסטו יום אחד ממסירותכם הטהורה למשיח, כשם שחווה רומתה על־ידי הנחש בגן העדן. 4אתם מתנהגים כפתאים ומאמינים לכל מה שאומרים לכם, גם אם מישהו מכריז לכם על ישוע השונה מזה שהכרזנו, או על רוח ששונה מרוח הקודש שקיבלתם, או על דרך שונה לישועה. אכן, אתם מוכנים להאמין לכל דבר!

5סבורני שאיני נופל במאומה מ”שליחים“ מיוחדים אלה! 6אולי אינני נואם מעולה, אך אני יודע לפחות על מה אני מדבר, כפי שהוכחנו לכם פעמים רבות.

7האם חטאתי כשהשפלתי את עצמי (כדי לרומם אתכם!) ובישרתי לכם את בשורת האלוהים ללא תשלום? 8קהילות אחרות תמכו בי בעת שעבדתי למענכם. כן, לקחתי את כספם כדי לעזור לכם. 9בכל עת שהותי עמכם לא ביקשתי מכם פרוטה; האחים שבאו ממקדוניה סיפקו את כל צרכי. מעולם לא ביקשתי מכם דבר, וגם להבא לא אבקש. 10בשם אמת המשיח בי, אני מבטיח שאתגאה על כך בכל יוון! 11מדוע? האם משום שאיני אוהב אתכם? אלוהים יודע שאני אוהב אתכם! 12אעשה זאת כדי לסכור את פיהם של אלה שמתפארים וטוענים: ”אנחנו עושים את עבודת אלוהים בדיוק כמו פולוס וטימותיוס!“

13אנשים אלה הינם שליחי־שקר, רמאים שמתחפשים לשליחי המשיח. 14אך איני מתפלא על כך! אם השטן עצמו יכול להתחפש למלאך אור, 15אין פלא שמשרתיו יכולים להתחפש למשרתי צדק. אך לבסוף הם יקבלו את העונש שמגיע להם על מעלליהם.

16אני חוזר ואומר, אל תחשבוני לשוטה, אך גם אם אתם חושבים אותי לשוטה, הקשיבו לי בכל זאת והניחו לי להתגאות כמוהם. 17גאווה זאת לא ניתנה לי מאת המשיח, שכן אני נוהג כשוטה. 18אך מאחר שרבים מתגאים על הישגיהם האנושיים, גם אני אתגאה כמוהם. 19אתם חושבים את עצמכם לחכמים גדולים, אך אתם מקשיבים ברצון לשוטים האלה. 20לא אכפת לכם אם הם משעבדים אתכם, מנצלים אתכם, מכשילים אתכם, סוטרים על פניכם או מתנשאים עליכם. 21אני מתבייש להודות שאיני חזק או נועז כמוהם. אך בכל מה שהם יכולים להתגאות, אני שוב מדבר כשוטה, גם אני יכול להתגאות! 22האם הם עברים? גם אני. האם הם ישראלים? גם אני. זרע אברהם? גם אני. 23האם הם משרתי המשיח? אולי אני מדבר כשוטה, אך אני משרת טוב מהם! עמלתי קשה מהם, הושלכתי לכלא פעמים רבות מהם, הוכיתי יותר, ועמדתי לפני המוות פעמים רבות יותר. 24חמש פעמים הלקוני היהודים שלושים־ותשע מלקות. 25שלוש פעמים הולקיתי בשוטים, פעם אחת נסקלתי באבנים, שלוש פעמים נטרפה ספינתי, ופעם נסחפתי עשרים־וארבע שעות בים הפתוח. 26במסעותיי הרבים והמעייפים ניצלתי מסכנת שיטפונות, מידי שודדים, מידי היהודים ומידי הגויים. הותקפתי על־ידי המון בערים שונות, ניצלתי ממוות במדבר, מטביעה בים ומאנשים שהתחזו כמאמינים משיחיים. 27עמלתי וטרחתי ולילות רבים לא עצמתי עין. פעמים רבות רעבתי וצמאתי; כן, הייתי ללא אוכל, לבוש או קורת־גג.

28מלבד כל אלה אני נושא עמי דאגה מתמדת לשלום הקהילות. 29כאשר מישהו שוגה, אני חש בצערו. כאשר מישהו חוטא, לבי כואב.

30אם עלי להתגאות, אני בוחר להתגאות בדברים שמראים את חולשתי. 31האלוהים ואבי המשיח אדוננו, יבורך שמו לעולמים, יודע שאני דובר אמת. 32בהיותי בדמשק, המושל מטעם המלך ארטס הפקיד שומרים על שערי העיר כדי לתפסני, 33אך הורדתי בסל דרך פתח בחומה ונמלטתי מידיו.