2 Wafalme 3 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 3:1-27

Moabu Wanaasi

13:1 2Fal 1:17Yehoramu3:1 Yehoramu wakati mwingine limetajwa kama Yoramu. mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye akatawala kwa miaka kumi na miwili. 23:2 1Fal 16:30; Kut 23:24Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini sio kama baba yake na mama yake walivyokuwa wamefanya. Akaondoa nguzo ya ibada ya Baali ambayo baba yake alikuwa ameitengeneza. 33:3 1Fal 12:30Hata hivyo akashikamana na dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, wala hakuziacha.

43:4 Mwa 19:37; Isa 16:1Basi Mesha mfalme wa Moabu akafuga kondoo, naye akawa ampatie mfalme wa Israeli wana-kondoo 100,000 pamoja na sufu ya kondoo dume 100,000. 53:5 2Fal 1:1Lakini baada ya Ahabu kufa, mfalme wa Moabu aliasi dhidi ya mfalme wa Israeli. 6Kwa hiyo wakati ule Mfalme Yehoramu akaondoka kutoka Samaria na kukusanya Israeli yote tayari kwenda vitani. 73:7 1Fal 22:4Akapeleka pia ujumbe ufuatao kwa Yehoshafati mfalme wa Yuda: “Mfalme wa Moabu ameasi dhidi yangu. Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Moabu?”

Akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe. Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”

8Akauliza, “Je, tutashambulia kupitia njia gani?”

Akajibu, “Kupitia Jangwa la Edomu.”

93:9 1Fal 22:47Hivyo mfalme wa Israeli akaondoka akiwa pamoja na mfalme wa Yuda na mfalme wa Edomu. Baada ya kuzunguka kwa siku saba, jeshi likawa limeishiwa maji kwa matumizi yao na kwa ajili ya wanyama waliokuwa nao.

10Mfalme wa Israeli akamaka, “Nini! Je, Bwana ametuita sisi wafalme watatu ili tu kututia mikononi mwa Moabu?”

113:11 Mwa 25:22; 1Fal 19:16Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa, ili tuweze kumuuliza Bwana kupitia kwake?”

Afisa mmoja wa mfalme wa Israeli akajibu, “Elisha mwana wa Shafati yuko hapa. Ndiye alikuwa akimimina maji juu ya mikono ya Eliya.”

123:12 Hes 11:17Yehoshafati akasema, “Neno la Bwana liko pamoja naye.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli na Yehoshafati pamoja na mfalme wa Edomu wakamwendea.

13Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Nina nini mimi nawe? Nenda kwa manabii wa baba yako na manabii wa mama yako.”

Mfalme wa Israeli akajibu, “La hasha, kwa sababu ni Bwana ambaye ametuita pamoja sisi wafalme watatu ili atutie mikononi mwa Moabu.”

14Elisha akasema, “Hakika, kama Bwana Mwenye Nguvu Zote aishivyo ambaye ninamtumikia, kama si kuheshimu Yehoshafati mfalme wa Yuda, nisingekutazama wala hata kukutupia jicho. 153:15 1Sam 10:5; Eze 1:3Lakini sasa, nileteeni mpiga kinubi.”

Mpiga kinubi alipokuwa akipiga, mkono wa Bwana ukaja juu ya Elisha, 16naye akasema, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Chimbeni bonde hili lijae mahandaki.’ 17Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana: Hamtaona upepo wala mvua, lakini bonde hili litajaa maji, nanyi pamoja na ngʼombe wenu na wanyama wenu wengine mtakunywa. 183:18 Mwa 18:14; Yer 32:17, 27; Mk 10:27Hili ni jambo rahisi machoni pa Bwana. Pia ataitia Moabu mikononi mwenu. 19Mtaushinda kila mji wenye ngome na kila mji mkubwa. Mtakata kila mti ulio mzuri, mtaziba chemchemi zote, na kuharibu kila shamba zuri kwa mawe.”

203:20 Kut 29:41Kesho yake asubuhi, karibu na wakati wa kutoa dhabihu ya asubuhi, tazama, maji yakawa yanatiririka kutoka upande wa Edomu! Nayo nchi ikajaa maji.

21Basi Wamoabu wote walikuwa wamesikia kuwa wale wafalme wamekuja kupigana dhidi yao. Hivyo kila mtu, kijana na mzee, ambaye angeweza kushika silaha akaitwa na kuwekwa mpakani. 22Walipoamka asubuhi na mapema, jua likawa linamulika juu ya maji. Wamoabu waliokuwa upande wa pili wakaona maji ni mekundu, kama damu. 23Wamoabu wakasema, “Ile ni damu! Lazima hao wafalme wamepigana na kuchinjana wao kwa wao. Sasa Moabu, twendeni tukateke nyara!”

24Lakini Wamoabu walipofika kwenye kambi ya Israeli, Waisraeli wakainuka na kuwapiga mpaka wakakimbia. Nao Waisraeli wakaivamia nchi na kuwachinja Wamoabu. 253:25 Isa 16:7; Yer 48:31, 36Wakaiharibu miji, kila mtu akatupa jiwe juu ya kila shamba zuri mpaka likafunikwa. Wakaziba chemchemi zote na kukata kila mti mzuri. Kir-Haresethi peke yake ndio uliobaki na mawe yake yakiwa mahali pake. Lakini hata hivyo watu waliokuwa na makombeo wakauzunguka na kuushambulia vilevile.

26Mfalme wa Moabu alipoona kuwa vita vimekuwa vikali dhidi yake, akachukua watu 700 wenye panga ili kuingia kwa mfalme wa Edomu, lakini wakashindwa. 273:27 Za 106:38; Mik 6:7Ndipo akamchukua mwanawe mzaliwa wake wa kwanza, ambaye angekuwa mfalme baada yake, akamtoa kama dhabihu ya kuteketezwa juu ya ukuta wa mji. Ghadhabu ikawa kubwa dhidi ya Israeli; wakajiondoa kwake na kurudi katika nchi yao wenyewe.

New International Reader’s Version

2 Kings 3:1-27

Moab’s King Refuses to Obey Israel’s King

1Joram became king of Israel in Samaria. It was in the 18th year that Jehoshaphat was king of Judah. Joram ruled for 12 years. He was the son of Ahab. 2Joram did what was evil in the sight of the Lord. But he wasn’t as bad as his father and mother had been. Joram’s father had made a sacred stone used to worship the god named Baal. Joram got rid of it. 3But he kept on committing the sins of Jeroboam, the son of Nebat. Jeroboam had also caused Israel to commit those same sins. Joram didn’t turn away from them.

4Mesha raised sheep. He was king of Moab. He had to pay the king of Israel 100,000 lambs a year. He also had to pay him with the wool of 100,000 rams a year. 5After Ahab died, Moab’s king refused to obey the next king of Israel. 6So at that time King Joram started out from Samaria. He gathered together all of Israel’s troops. 7He also sent a message to Jehoshaphat, the king of Judah. Joram said, “The king of Moab is refusing to obey me. Will you go with me to fight against Moab?”

“Yes. I’ll go with you,” Jehoshaphat replied. “My men will go with you. My horses will also go with you.”

8“What road should we take to attack Moab?” Joram asked.

“The one that goes through the Desert of Edom,” Jehoshaphat answered.

9So the king of Israel marched out. The king of Judah and the king of Edom went with him. Their armies marched around the southern end of the Dead Sea. After seven days they ran out of water. There wasn’t any water for the men or their animals.

10“What should we do now?” exclaimed the king of Israel. “The Lord has called us three kings together. Did he do it only to hand us over to Moab?”

11But Jehoshaphat asked, “Isn’t there a prophet of the Lord here? Can’t we ask the Lord for advice through him?”

An officer of the king of Israel answered, “Elisha is here. He’s the son of Shaphat. Elisha used to serve Elijah.”

12Jehoshaphat said, “The Lord speaks through him.” So the king of Israel went down to see Elisha. Jehoshaphat and the king of Edom also went there.

13Elisha said to the king of Israel, “Why do you want to come to me? Go to your father’s prophets. Go to your mother’s prophets.”

“No,” the king of Israel answered. “The Lord called us three kings together. He did it to hand us over to Moab.”

14Elisha said, “I serve the Lord who rules over all. You can be sure that he lives. And you can be just as sure that I have respect for Jehoshaphat, the king of Judah. If I didn’t, I wouldn’t pay any attention to you. 15But now bring me someone who plays the harp.”

While that person was playing the harp, the Lord’s power came on Elisha. 16Elisha announced, “The Lord says, ‘I will fill this valley with pools of water.’ 17This will happen because the Lord says, ‘You will not see wind or rain. But this valley will be filled with water. Then you, your cattle and your other animals will have water to drink.’ 18This is an easy thing for the Lord to do. He will also hand Moab over to you. 19You will destroy every city that has high walls around it. You will destroy every major town. You will cut down every good tree. You will stop up all the springs of water. And you will cover every good field with stones.”

20The next day, the time came to offer the morning sacrifice. And then it happened! Water was flowing from the direction of Edom! In fact, the land was filled with water!

21Now all the people of Moab had heard that the kings had come to fight against them. So the king of Moab sent for all Moab’s fighting men. It didn’t matter whether they were young or old. He sent for everyone who could carry a weapon. All of them were stationed at the border. 22They got up early in the morning. The sun was already shining on the water. Across the way, the water looked red to the men of Moab. It looked like blood. 23“That’s blood!” they said. “Those kings must have fought and killed each other. Let’s go, Moab! Let’s take everything that has any value.”

24So the men of Moab went to the camp of Israel. Just as they arrived there, the men of Israel got ready to fight. They fought against the men of Moab until those men ran away. The men of Israel marched into the land and attacked it. They killed the people of Moab. 25They destroyed the towns. Each man threw a large stone on every good field. They did that until the fields were covered. They stopped up all the springs of water. And they cut down every good tree. The only town left with any stones in place was Kir Hareseth. But some of the Israelites armed with slings surrounded it. Then they attacked it.

26The king of Moab saw that the battle had gone against him. So he took with him 700 men who had swords. They tried to break through the battle lines to the king of Edom. But they couldn’t do it. 27Then the king of Moab took his oldest son. He was the son who would become the next king of Moab. But the king offered his son as a sacrifice on the city wall. That shocked and terrified the men of Israel. So they pulled back and returned to their own land.